Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia Profesa Makame Mbarawa amesema hajapokea maombi ya Chama
cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania nchini Tanzania (MOAT) kuhusu kusitisha
kurusha matangazo ndani ya mwezi mmoja kuanzia sasa kutokana na kushindwa
kumudu gharama za uendeshaji wanazodai zinatokana na urushaji wa matangazo kwa njia ya dijitali.
Kupitia kipindi cha Radio One asubuhi ya leo,Waziri Mbarawa amesema hajapokea ombi hilo ambalo hafahamu linaeleza nini na atakapolipokea wizara italifanyia kazi japo amesema wamiliki wa vituo vya televisheni nchini walikubaliana na wizara katika uhamishaji wa masafa ya utangazaji kutoka analojia kwenda dijitali mchakato ambao ulianza mwaka 2005 na vyombo hivyo vilikubali kutumia teknolojia hiyo.
Kabla ya kuanza kwa zoezi la kuzima mitambo ya analojia disemba 31,2012 vyombo vyote vya utangazaji viliitwa na kusaini makubaliano ya kuzima mitambo na kuanza kurusha kwa njia ya dijitali.
Nayo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema haitarudi nyuma kwenye suala
la kutumia mfumo wa matangazo kupitia njia ya dijitali na kwamba mfumo huo
utaendelea kutumika.
TCRA ilizima mitambo ya analojia na kuhamia dijitali, Desemba 31, mwaka jana
kitendo ambacho Chama
cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT) wanadai kimepunguza mapato yanayotokana na matangazo.
Popular Posts
-
Watafiti toka kampuni ya utafiti ya Zscalar wamegundua kuwa,tovuti za kichina zenye picha za ngono zimekuwa zikisamb...
-
Facebook wametangaza kitu kipya kwa simu za Android walichokipa jina la Home. Kwa muda mrefu kulikuwa na uvumi kuwa Facebook wana...
-
Semina kuhusu mfumo wa utunzaji wa taarifa za washiriki katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato (ACMS) imemalizika jijini Arusha Septem...
-
Baadhi ya Wataalamu wa Teknohama wa Taasis za Kanisa la Waadventista Wataalamu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Kanisa l...
-
Picha na Salim Kikeke Kuanzia sasa kudanganya kwamba mtu hakupata ujumbe wako wa WhatsApp itakuwa historia, au kud...
-
Serikali ya Tanzania imeomba mkopo wa Dola za Marekani milioni 154 ambazo ni takribani shilingi za kitanzania bilioni 246 kwa India kuwezesh...
-
Mwezeshaji wa kipindi cha Maisha na Teknohama cha Morning Star Radio,Johnson Mziray akichangia jambo kwenye warsha hiyo,pembeni yake mweny...
-
Mmoja wa wafanyakazi wa Digital Brain Bi.Edith akifafanua jambo kuhusu kampuni hiyo ambayo imeanzisha program ya usimamizi wa hospital na ...
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
Lagos, Nigeria - A little over a decade ago there were about 100,000 phone lines in Nigeria, mostly landlines run by the state-owned tel...