Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia Profesa Makame Mbarawa amesema hajapokea maombi ya Chama
cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania nchini Tanzania (MOAT) kuhusu kusitisha
kurusha matangazo ndani ya mwezi mmoja kuanzia sasa kutokana na kushindwa
kumudu gharama za uendeshaji wanazodai zinatokana na urushaji wa matangazo kwa njia ya dijitali.
Kupitia kipindi cha Radio One asubuhi ya leo,Waziri Mbarawa amesema hajapokea ombi hilo ambalo hafahamu linaeleza nini na atakapolipokea wizara italifanyia kazi japo amesema wamiliki wa vituo vya televisheni nchini walikubaliana na wizara katika uhamishaji wa masafa ya utangazaji kutoka analojia kwenda dijitali mchakato ambao ulianza mwaka 2005 na vyombo hivyo vilikubali kutumia teknolojia hiyo.
Kabla ya kuanza kwa zoezi la kuzima mitambo ya analojia disemba 31,2012 vyombo vyote vya utangazaji viliitwa na kusaini makubaliano ya kuzima mitambo na kuanza kurusha kwa njia ya dijitali.
Nayo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema haitarudi nyuma kwenye suala
la kutumia mfumo wa matangazo kupitia njia ya dijitali na kwamba mfumo huo
utaendelea kutumika.
TCRA ilizima mitambo ya analojia na kuhamia dijitali, Desemba 31, mwaka jana
kitendo ambacho Chama
cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT) wanadai kimepunguza mapato yanayotokana na matangazo.
Popular Posts
-
Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania itafanya sherehe maalumu za kutimiza miaka 50 ya Uhuru katika Wiki ya Sayansi ...
-
Wakulima nchini Nigeria wamepewa bure simu za mikononi,Ingawa vyama vya upinzani vinakandia hali hiyo wananchi wengi wanaamini huo ni...
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dares Salaam leo. ...
-
Miongoni mwa changamoto inayoonekana kwa sasa katika teknolojia ya habari na mawasiliano (Teknohama) ni suala la ulinzi katika mitandao...
-
SERIKALI YA TANZANIA YASEMA:KUTOA TAARIFA ZA SIRI KATIKA MAWASILIANO YA ELEKTRONIKI NI KOSA LA JINAITAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Jana na leo, Serikali ya Tanzania imeona kuzuka kwa tabia ya uvunjaji wa kanuni ya utunza...
-
Kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania Dr Godwin Lekundayo akiwaongoza viongozi wenzake katika maombi wakati wa ugawaji wa...
-
Baadhi ya Wataalamu wa Teknohama wa Taasis za Kanisa la Waadventista Wataalamu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Kanisa l...