Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia Profesa Makame Mbarawa amesema hajapokea maombi ya Chama
cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania nchini Tanzania (MOAT) kuhusu kusitisha
kurusha matangazo ndani ya mwezi mmoja kuanzia sasa kutokana na kushindwa
kumudu gharama za uendeshaji wanazodai zinatokana na urushaji wa matangazo kwa njia ya dijitali.
Kupitia kipindi cha Radio One asubuhi ya leo,Waziri Mbarawa amesema hajapokea ombi hilo ambalo hafahamu linaeleza nini na atakapolipokea wizara italifanyia kazi japo amesema wamiliki wa vituo vya televisheni nchini walikubaliana na wizara katika uhamishaji wa masafa ya utangazaji kutoka analojia kwenda dijitali mchakato ambao ulianza mwaka 2005 na vyombo hivyo vilikubali kutumia teknolojia hiyo.
Kabla ya kuanza kwa zoezi la kuzima mitambo ya analojia disemba 31,2012 vyombo vyote vya utangazaji viliitwa na kusaini makubaliano ya kuzima mitambo na kuanza kurusha kwa njia ya dijitali.
Nayo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema haitarudi nyuma kwenye suala
la kutumia mfumo wa matangazo kupitia njia ya dijitali na kwamba mfumo huo
utaendelea kutumika.
TCRA ilizima mitambo ya analojia na kuhamia dijitali, Desemba 31, mwaka jana
kitendo ambacho Chama
cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT) wanadai kimepunguza mapato yanayotokana na matangazo.
Popular Posts
-
Jeshi la Polisi Tanzania limeanza kunasa watu wanaodaiwa kutuma ujumbe wa matusi na wengine kupiga simu kwa spika wa Bunge la nchi hiyo Anne...
-
Kwa mara ya kwanza katika historia ya Afrika,Raia wa Afrika kutoka Congo-DRC Verone Mankou,amezindua simu aina ya smarthphone na k...
-
--> Mwenyekiti wa muda wa Chama cha Wamiliki wa Blog (TBN),Joachim Mushi akizungumza na waandishi wa habari Ofisa Uhusiano...
-
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yussuf Mwenda akibofya kompyuta kuzindua huduma ya WiFi ya bure kwenye Kituo cha Mabasi cha Sinza, wi...
-
Wamiliki wa vituo vya utangazaji vya televisheni nchini, wamesema watasitisha kurusha matangazo ndani ya mwezi mmoja kuanzia sasa kutokan...
-
Shehena ya Mizigo inayopitia bandari na mipaka ya Tanzania kwenda nchi za nje kuanzia mwakani itakuwa ikifuatiliwa kwa mfumo wa kielektronik...
-
ILI kuboresha utoaji huduma kwa umma hivi karibuni Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeanzisha utaratibu wa kupokea malala...
-
Polisi Wa kuzuia uhalifu Mtandao. Wakala unaofuatilia matumizi ya mitandao duniani (IAB) umebaini watumiaji wa intaneti nchini Ko...
-
Explore more visuals like this one on the web's largest information design community - Visually .