Thursday, June 19, 2014

TEKNOLOJIA YA KUKABILIANA NA MADAWA YA KULEVYA YAONESHA MAFANIKIO UWANJA WA NDEGE WA JULIUS NYERERE



Waziri na waziri wa uchukuzi Dr Harrison mwakyembe  amesema kuwa Teknolojia ya kisasa inayotumika katika  uwanja wa ndege wa  kimataifa wa Julius Nyerere kukabiliana na dawa za kulevya imeonesha mafanikio  katika kuwabaini wanaojihusisha na usafirishaji  wa dawa hizo.


Dr Mwakyembe  ameyasema hayo  wakati akifungua  semina ya baraza la viongozi wa dini la kupambana na dawa za kulevya  Tanzania  iliyofanyika  jana jijini Dar es salaam.


Mwakyembe amesema wanatumia teknolojia  ya kisasa katika uwanja huo ambayo imesaidia kwa kiasi kikubwa  kupunguza  aibu ya watu  wanaokamatwa  na dawa za kulevya  katika nchi mbalimbali duniani  wakitokea Tanzania .


Taarifa zinaonesha kuwa  kwa kipindi cha kati ya ya januari  2013  na mei mwaka huu   jumla  ya kilogramu 85,840  za bangi  na kilogramu 18,202  za mirungi zilikamatwa.


Dr Mwakyembe ameyataja madawa mengine kuwa ni heroini kilogramu 1,547 , kokeini kilogramu 15.4  na kwamba watuhumiwa wakifikishwa katika vyombo vya sheria
.

Dr Mwakyembe ameongeza kuwa wizara yake ipo katika mchakato wa kutafuta kampuni yenye teknolojia ya kisasa zaidi itakayoimarisha ulinzi na kukabiliana na hila zote za wasafirishaji na kuomba  ushirikiano wa vyombo vya ulinzi  na usalama kubaini mtandao wa biashara hiyo ili kupambana na wimbi la usafirishaji wa dawa za kulevya dunia.


Popular Posts

Labels