Friday, June 20, 2014

VITAMBULISHO VYA KUPIGIA KURA TANZANIA KUTOLEWA KWA TEKNOLOJIA YA BIOMETRIC VOTER REGISTRATION



Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya uchaguzi nchini Tanzania Mh.Jaji Mstaafu Damian lubuva amesema tume hiyo  inatarajia kuboresha daftari la wapiga  kwa kutumia teknolojia mpya ya  “BIOMETRIC VOTER REGISTRATION” (BVR) ili kuwapatia watanzania vitambulisho vipya vya kupigia kura. 

Akizungumza wahariri wa vyombo vya habari katika ukumbi wa hoteli ya JB Belmonte jijini Dar es salaam juni 19 mwaka huu Lubuva  amesema tume ya uchaguzi  imeamua kufanya maboresho ya daftari la kudumu  la wapiga kura kwa kutumia teknolojia hii mpya ya biometric voter ili kwenda na wakati pia ni mfumo wa kuchukua na kupima taarifa  za mtu kibaiolojia au tabia ya mtu  na kuzihifadhi kwa ajili ya utambuzi ambapo alama za vidole  kumi, vya mikono, picha na saini  ndizo zitakazochukuliwa na kuhifadhiwa  kwenye kanzidata (database) ya wapiga kura.



Mh. Jaji pia amefafanua zaidi kwa kusema  “mfumo huu utasaidia sana kuwa na daftari  sahihi na linalotumika kwa ajili ya upigaji wa kura ya maoni  na uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 na kuwa mfumo huu utatumika tu kwa ajili ya  kuandikisha wapiga kura na si kwa ajili ya upigaji kura za kielektroniki(e-voting) au vinginevyo”

Amesema Lubuva amesema  uamuzi  kutumia mfumo huu umetokana na changamoto  zilizojitokeza  katika matumizi ya teknolojia ya optical mark recognition (omr) kwamba omr ilisababnisha daftari la kudumu kuwa na kasoro hivyo kusababisha wadau wa uchaguzi  uhalali wake.

Waapiga kura wote waliojiandikisha awali na wale wapya watalazimika  kujiandikisha  upya ili kuchukuliwa taarifa  za kibaiolojia  kwa waliopo kwenye daftari hata hivyo mpiga kura atatumia kitambulisho atakachopatiwa na tume baada ya kuandikishwa katika mfumo huu tu na si vinginevyo.

Popular Posts

Labels