Kampuni za Simu za mkononi za Tigo,Airtel na Zantel zimeunganisha huduma zao za kutoa,kutuma na kuweka fedha na sasa mteja anaweza kutuma fedha kutoka mtandao mmoja kupitia mwingine.
Taarifa ya pamoja iliyotolewa hivi karibuni na kampuni hizo imesema kuwa wote wanaotumia huduma hiyo wataweza kutumiana fedha kupitia simu zao za mikononi pasi na tatizo baada ya kampuni hizo kuunganisha huduma zao.
Huduma hiyo inayotajiwa kuanza kutumika mwishoni mwa mwezi huu itawafanya wateja wa mitandao hiyo kutumiana na kupokea fedha moja kwa moja kwenye akaunti zao tofauti na ilivyokuwa awali.
Matumizi ya simu za mkononi kufanya miamala ya kifedha yamezidi kukua kwa kasi nchini Tanzania,kwa mujibu wa Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia wa Tanzania Profesa Makambe Mbarawa hadi sasa kuna watumiaji wa huduma za kifedha kwa simu za mkononi 12,330,962
Saturday, June 7, 2014
Popular Posts
-
Mamlaka ya Mawasiliano nchini Tanzania (TCRA) kupitia Mkurugenzi wake Mkuu Profesa John Nkoma imesema namba za simu zilizosajiliwa nchini hu...
-
Mmoja wa wafanyakazi wa Digital Brain Bi.Edith akifafanua jambo kuhusu kampuni hiyo ambayo imeanzisha program ya usimamizi wa hospital na ...
-
Serikali kusambaza tabiti za kufundishia sekondari Yaanza kazi hiyo kwa kushirikiana na taasisi ya Marekani ya Opportunity Education Tr...
-
SERIKALI YA TANZANIA YASEMA:KUTOA TAARIFA ZA SIRI KATIKA MAWASILIANO YA ELEKTRONIKI NI KOSA LA JINAITAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Jana na leo, Serikali ya Tanzania imeona kuzuka kwa tabia ya uvunjaji wa kanuni ya utunza...