Kampuni za Simu za mkononi za Tigo,Airtel na Zantel zimeunganisha huduma zao za kutoa,kutuma na kuweka fedha na sasa mteja anaweza kutuma fedha kutoka mtandao mmoja kupitia mwingine.
Taarifa ya pamoja iliyotolewa hivi karibuni na kampuni hizo imesema kuwa wote wanaotumia huduma hiyo wataweza kutumiana fedha kupitia simu zao za mikononi pasi na tatizo baada ya kampuni hizo kuunganisha huduma zao.
Huduma hiyo inayotajiwa kuanza kutumika mwishoni mwa mwezi huu itawafanya wateja wa mitandao hiyo kutumiana na kupokea fedha moja kwa moja kwenye akaunti zao tofauti na ilivyokuwa awali.
Matumizi ya simu za mkononi kufanya miamala ya kifedha yamezidi kukua kwa kasi nchini Tanzania,kwa mujibu wa Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia wa Tanzania Profesa Makambe Mbarawa hadi sasa kuna watumiaji wa huduma za kifedha kwa simu za mkononi 12,330,962
Saturday, June 7, 2014
Popular Posts
-
Bwana. Keriako Tobiko Mkurugenzi wa Mashtaka ya umma ya nchini Kenya Bwana. Keriako Tobiko ametangaza kuanzishwa kwa kitengo maalum...
-
Upungufu wa usalama wa herufi za siri za takriban simu milioni 900 umewapa wadukuzi fursa ya kudhibiti simu za android kote duniani...
-
Polisi Wa kuzuia uhalifu Mtandao. Wakala unaofuatilia matumizi ya mitandao duniani (IAB) umebaini watumiaji wa intaneti nchini Ko...
-
KAMA HAUKUJUA BASI JUA Na MBUKE TIMES Neno HACKER makusudio yake haswa sio kumaanisha mtu anayefanya vitendo vya kihalifu kwa kutu...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetangaza kuzima rasmi mitambo ya kurusha matangazo ya televisheni kupitia mfumo wa utangazaji wa a...
-
Kampuni ya ConnectMoja Technologies Wamezindua tovuti mpya iitwayo Mavazi Store ( www.mavazi.co.tz ) ambayo inajumuisha Mkusanyiko w...
-
Katika wiki chache zilizopita kulikuwa na msuguano kati ya serikali ya Marekani na China , Serikali ya Marekani inailaumu china kwa kufany...