Serikali ya Tanzania imeweka mitambo ya aina tatu kukabili ulaghai na udanganyifu kwenye mawasiliano na miamala ya simu za mkononi.
Taarifa hiyo imetolewa hivi karibuni bungeni na Naibu Waziri wa Mawasiliano nchini Tanzania,Sayansi na Teknolojia,January Makamba.Amesema tayari watu watu watatu wamekamatwa kwa kutaka kuiibia serikali shilingi bilioni nane.
Makamba amesema upo mtambo wa kutambua kila kifaa kama vile simu,Ipad au komputa iliyotumika katika matukio ya kihalifu kwa kuizima na kufahamu umbali au eneo kilipo kifaa husika kinachotumika kutuma ujumbe wa matusi,Ulaghai au wizi wa fedha za wateja.
Waziri huyo amefafanua kuwa serikali imeanza kubana kampuni za simu kuhakikisha zinatoa huduma bora za usikivu wa simu,kushughulikia malalamiko ya wateja,kuhakikisha hakuna wizi wa fedha za wateja unaofanyika katika simu.
Popular Posts
-
Kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania Dr Godwin Lekundayo akiwaongoza viongozi wenzake katika maombi wakati wa ugawaji wa...
-
China imezifungia tovuti 110 ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kitaifa ya kuzuia masuala ya ngono kwenye mitandao.Imeeleza taarifa ya serikal...
-
Bunduki ya plastiki iliyotengenezwa kwa mashine ya 3D ikifyatua risasi wakati wa majaribio Photo credits: Screenshot from ATF Video Kam...
-
Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr Jakaya Mrisho Kikwete amezindua Mtambo Maalum wa Usimamizi na Uhakiki wa M...
-
Program Tumishi maarufu ya mawasiliano ya ujumbe wa papo kwa papo katika simu za BlackBerry inayojulikana kwa jina la BlackBerry Mes...
-
Mtandao wa kijamii wa Facebook umenunua programu tumishi ya huduma za ujumbe mfupi wa maneno ya WhatsApp kwa dola za marekani bilioni ...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya kati imewataka watangazaji wa radio, luninga na mitandao ya kijamii kuwa makini na hab...
-
Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL) jana imekabidhi mradi wa mawasiliano utaotumiwa katika mikoa 12 ya Tanzania kwa ofisi ya Mkaguzi na ...
-
Kampuni ya Google kupitia huduma yake ya kutafuta jambo sasa imeanzisha utaratibu wa kutoa majibu ya moja kwa moja kwa maswali kuhus...