Serikali ya Tanzania imeweka mitambo ya aina tatu kukabili ulaghai na udanganyifu kwenye mawasiliano na miamala ya simu za mkononi.
Taarifa hiyo imetolewa hivi karibuni bungeni na Naibu Waziri wa Mawasiliano nchini Tanzania,Sayansi na Teknolojia,January Makamba.Amesema tayari watu watu watatu wamekamatwa kwa kutaka kuiibia serikali shilingi bilioni nane.
Makamba amesema upo mtambo wa kutambua kila kifaa kama vile simu,Ipad au komputa iliyotumika katika matukio ya kihalifu kwa kuizima na kufahamu umbali au eneo kilipo kifaa husika kinachotumika kutuma ujumbe wa matusi,Ulaghai au wizi wa fedha za wateja.
Waziri huyo amefafanua kuwa serikali imeanza kubana kampuni za simu kuhakikisha zinatoa huduma bora za usikivu wa simu,kushughulikia malalamiko ya wateja,kuhakikisha hakuna wizi wa fedha za wateja unaofanyika katika simu.
Popular Posts
-
Kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania Dr Godwin Lekundayo akiwaongoza viongozi wenzake katika maombi wakati wa ugawaji wa...
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
Mvumbuzi wa programu hii ya Kighana Herman Chinery-Hesse alitaka kuchukua hatua dhidi ya matukio ...
-
KAMA HAUKUJUA BASI JUA Na MBUKE TIMES Neno HACKER makusudio yake haswa sio kumaanisha mtu anayefanya vitendo vya kihalifu kwa kutu...