Serikali ya Tanzania imeweka mitambo ya aina tatu kukabili ulaghai na udanganyifu kwenye mawasiliano na miamala ya simu za mkononi.
Taarifa hiyo imetolewa hivi karibuni bungeni na Naibu Waziri wa Mawasiliano nchini Tanzania,Sayansi na Teknolojia,January Makamba.Amesema tayari watu watu watatu wamekamatwa kwa kutaka kuiibia serikali shilingi bilioni nane.
Makamba amesema upo mtambo wa kutambua kila kifaa kama vile simu,Ipad au komputa iliyotumika katika matukio ya kihalifu kwa kuizima na kufahamu umbali au eneo kilipo kifaa husika kinachotumika kutuma ujumbe wa matusi,Ulaghai au wizi wa fedha za wateja.
Waziri huyo amefafanua kuwa serikali imeanza kubana kampuni za simu kuhakikisha zinatoa huduma bora za usikivu wa simu,kushughulikia malalamiko ya wateja,kuhakikisha hakuna wizi wa fedha za wateja unaofanyika katika simu.
Popular Posts
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Unapomblock mtu kwenye viber inamaana umezuia kuwasiliana na mtu yoyote kwa njia yoyote katika mtandao wa kijamii wa viber,huta...
-
ILI kuboresha utoaji huduma kwa umma hivi karibuni Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeanzisha utaratibu wa kupokea malala...
-
KAMA HAUKUJUA BASI JUA Na MBUKE TIMES Neno HACKER makusudio yake haswa sio kumaanisha mtu anayefanya vitendo vya kihalifu kwa kutu...
-
Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) inatarajia kuzima rasmi mitambo ya analojia ya urushaji wa matangazo ya televisheni katika miji ya ...