Serikali ya Tanzania imeweka mitambo ya aina tatu kukabili ulaghai na udanganyifu kwenye mawasiliano na miamala ya simu za mkononi.
Taarifa hiyo imetolewa hivi karibuni bungeni na Naibu Waziri wa Mawasiliano nchini Tanzania,Sayansi na Teknolojia,January Makamba.Amesema tayari watu watu watatu wamekamatwa kwa kutaka kuiibia serikali shilingi bilioni nane.
Makamba amesema upo mtambo wa kutambua kila kifaa kama vile simu,Ipad au komputa iliyotumika katika matukio ya kihalifu kwa kuizima na kufahamu umbali au eneo kilipo kifaa husika kinachotumika kutuma ujumbe wa matusi,Ulaghai au wizi wa fedha za wateja.
Waziri huyo amefafanua kuwa serikali imeanza kubana kampuni za simu kuhakikisha zinatoa huduma bora za usikivu wa simu,kushughulikia malalamiko ya wateja,kuhakikisha hakuna wizi wa fedha za wateja unaofanyika katika simu.
Popular Posts
-
Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL) jana imekabidhi mradi wa mawasiliano utaotumiwa katika mikoa 12 ya Tanzania kwa ofisi ya Mkaguzi na ...
-
Miaka michache iliyopita kulikuwa na changamoto ya kuhifadhi vitu sehemu ambayo mtu anaweza kutumia akiwa popote duniani akiwa ame...
-
Ofisa Biashara wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, Thomas Lemunge akitoa ufafanuzi katika semina kwa wahariri juu ya mkongo wa taifa katika...