Friday, October 25, 2013

MKONGO WA TAIFA WAINUFAISHA SERIKALI YA TANZANIA

 
Zaidi ya shilingi bilioni 41.4 zimepatikana kutokana na malipo ya huduma za Mkongo wa Taifa ambapo hadi Agosti mwaka huu kampuni 16 zikiwamo 9 za nje zimeunganishwa kwenye mtandao huo imara kwa mawasiliano.

Pia mipango inafanywa kuunganisha vituo mbalimbali vya luninga na raedio kwenye huduma hiyo.Hayo yamebainishwa kwenye juzi na Ofisa Mtendaji wa Kampuni ya Simu ya Tanzania (TTCL),Kamugisha Kazaura katika taarifa yake aliyoitoa kwa Kamati ya Bunge la Tanzania ya Miundombinu.

Amesema ni kampuni saba pekee za ndani zilizounganishwa ni kampuni hizo ni TTCL yenye jukumu la kusimamia mkongo huo,zingine ni Zantel,Simbanet,Airtel,Tigo,Infinity Africa na Vodacom.

Kampuni za nje ni pamoja na MTN-Zambia hadi Malawi,MTN-Rwanda,Airtel Rwanda,KDN,RDB,Econet,BCS na UCOM-Burundi

chanzo:Gazeti la Mwananchi

Popular Posts

Labels