Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia Tanzania Pro Makame Mbarawa ameitaka kampuni ya Simu ya SamSung na Vodacom kuhakikisha inazuia mifumo inayozuia kuonekana kwa tovuti zisizofaa katika mtandao wa intaneti ambao unaziunganisha shule za sekondari nchini Tanzania nchini ya mkongo wa taifa wa mawasiliano aliouzindua katika shule ya sekondari ya Kambangwa ilipo Kinondoni,Dar es salaam oktoba 22 mwaka huu.
"Nachukua fulsa hii kumwomba mwalimu Mkuu,Vodacom na Samsung kuhakikisha kuwa tovuti ambazo hazifai na zisizo na maslahi kwa watumiaji zinazuiwa kuonekanakwenye mfumo huo hilo halina mjadala"amesema waziri huyo
Amesema ni kosa kubwa kuingia katika mitandao ya ajabu na hivyo serikali ya Tanzania haitokubaliana na suala hilo na serikali iko tayali kushirikiana na walimu katika kuhakikisha suala hilo linazuiwa kwa kushirikiana na wataalamu wa wizara.
Kampuni ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na kampuni ya Samsung zimeungana katika kuunganisha shule za sekondari nchini Tanzania kupitia mkongo wa Taifa ambao utawezesha kupata mawasiliano ya intaneti kwa ajili ya kujifunza masuala mbalimbali ya kielimu ambayo baadhi yake hayawezi kupatikana darasani au kwenye vitabu na wameanza majaribio na shule ya sekondari ya Kambangwa .
Katika ufunguzi huo ambao ni sehemu ya mradi wa Tanzania ya Kesho Waziri Mbarawa aliwataka walimu na wanafunzi wote kutumia maabara za komputa zitakazoweka katika kutumika kwenye utaratibu huo.
Friday, October 25, 2013
Popular Posts
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia ,Bw Charles Kitwanga ameyashawishi mataifa ambayo tayari yamejiunga na mfumo wa Digitali katika haraka...
-
ILI kuboresha utoaji huduma kwa umma hivi karibuni Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeanzisha utaratibu wa kupokea malala...
-
Ted Wilson na mkewe Nancy Kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Ulimwenguni Ted N.C. Wilson ameziundua rasmi mawasiliano ...