Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia Tanzania Pro Makame Mbarawa ameitaka kampuni ya Simu ya SamSung na Vodacom kuhakikisha inazuia mifumo inayozuia kuonekana kwa tovuti zisizofaa katika mtandao wa intaneti ambao unaziunganisha shule za sekondari nchini Tanzania nchini ya mkongo wa taifa wa mawasiliano aliouzindua katika shule ya sekondari ya Kambangwa ilipo Kinondoni,Dar es salaam oktoba 22 mwaka huu.
"Nachukua fulsa hii kumwomba mwalimu Mkuu,Vodacom na Samsung kuhakikisha kuwa tovuti ambazo hazifai na zisizo na maslahi kwa watumiaji zinazuiwa kuonekanakwenye mfumo huo hilo halina mjadala"amesema waziri huyo
Amesema ni kosa kubwa kuingia katika mitandao ya ajabu na hivyo serikali ya Tanzania haitokubaliana na suala hilo na serikali iko tayali kushirikiana na walimu katika kuhakikisha suala hilo linazuiwa kwa kushirikiana na wataalamu wa wizara.
Kampuni ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na kampuni ya Samsung zimeungana katika kuunganisha shule za sekondari nchini Tanzania kupitia mkongo wa Taifa ambao utawezesha kupata mawasiliano ya intaneti kwa ajili ya kujifunza masuala mbalimbali ya kielimu ambayo baadhi yake hayawezi kupatikana darasani au kwenye vitabu na wameanza majaribio na shule ya sekondari ya Kambangwa .
Katika ufunguzi huo ambao ni sehemu ya mradi wa Tanzania ya Kesho Waziri Mbarawa aliwataka walimu na wanafunzi wote kutumia maabara za komputa zitakazoweka katika kutumika kwenye utaratibu huo.
Friday, October 25, 2013
Popular Posts
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Unapomblock mtu kwenye viber inamaana umezuia kuwasiliana na mtu yoyote kwa njia yoyote katika mtandao wa kijamii wa viber,huta...
-
ILI kuboresha utoaji huduma kwa umma hivi karibuni Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeanzisha utaratibu wa kupokea malala...
-
KAMA HAUKUJUA BASI JUA Na MBUKE TIMES Neno HACKER makusudio yake haswa sio kumaanisha mtu anayefanya vitendo vya kihalifu kwa kutu...
-
Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) inatarajia kuzima rasmi mitambo ya analojia ya urushaji wa matangazo ya televisheni katika miji ya ...