Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia Tanzania Pro Makame Mbarawa ameitaka kampuni ya Simu ya SamSung na Vodacom kuhakikisha inazuia mifumo inayozuia kuonekana kwa tovuti zisizofaa katika mtandao wa intaneti ambao unaziunganisha shule za sekondari nchini Tanzania nchini ya mkongo wa taifa wa mawasiliano aliouzindua katika shule ya sekondari ya Kambangwa ilipo Kinondoni,Dar es salaam oktoba 22 mwaka huu.
"Nachukua fulsa hii kumwomba mwalimu Mkuu,Vodacom na Samsung kuhakikisha kuwa tovuti ambazo hazifai na zisizo na maslahi kwa watumiaji zinazuiwa kuonekanakwenye mfumo huo hilo halina mjadala"amesema waziri huyo
Amesema ni kosa kubwa kuingia katika mitandao ya ajabu na hivyo serikali ya Tanzania haitokubaliana na suala hilo na serikali iko tayali kushirikiana na walimu katika kuhakikisha suala hilo linazuiwa kwa kushirikiana na wataalamu wa wizara.
Kampuni ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na kampuni ya Samsung zimeungana katika kuunganisha shule za sekondari nchini Tanzania kupitia mkongo wa Taifa ambao utawezesha kupata mawasiliano ya intaneti kwa ajili ya kujifunza masuala mbalimbali ya kielimu ambayo baadhi yake hayawezi kupatikana darasani au kwenye vitabu na wameanza majaribio na shule ya sekondari ya Kambangwa .
Katika ufunguzi huo ambao ni sehemu ya mradi wa Tanzania ya Kesho Waziri Mbarawa aliwataka walimu na wanafunzi wote kutumia maabara za komputa zitakazoweka katika kutumika kwenye utaratibu huo.
Friday, October 25, 2013
Popular Posts
-
Serikali ya Kenya imesema watu watakaopatikana na hatia ya kutuma ujumbe wa kingono kwa kutumia simu za kiganjani na intaneti watafungw...
-
Miongoni mwa changamoto inayoonekana kwa sasa katika teknolojia ya habari na mawasiliano (Teknohama) ni suala la ulinzi katika mitandao...
-
Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu ...
-
Yusuph Kileo baada ya kukabidhiwa tuzo Mtaalamu wa masuala ya usalama mtandaoni Yusu ph Kileo hivi karibuni alipata Tunzo ya ...
-
Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia imesema gharama za kupiga simu kutoka mtandao wa kampuni moja ya s...
-
Shule ya Msingi ya Mlimani iliyopo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuanzia wiki hii itaanza kunufaika na huduma ya intaneti bure inayofung...
-
Kampuni ya magari ya Fiat Chrysler kutoka Marekani imeyarudisha magari yake yapatayo milioni 1.4 baada ya watafiti wa usalama kuony...
-
Watumiaji wa programu ya komputa iitwayo Window XP wamepewa tahadhari na kampuni ya Microsoft ambayo ndiyo iliyotengeneza program hiyo ...
-
Na Brown Nyanza Wanasayansi wawili katika nchi ya Ujerumani wamegundua kalamu inayotoa alama pindi mwandishi anapokosea heruf...
-
Mkuu Kituo cha Teknohama cha Ushirikiano wa India na Tanzania (DIT), Dr. Amos Nungu akiwakaribisha wafanyakazi wa Shirika la Umoja w...