Friday, October 11, 2013
TABITI ZAPUNGUZA SOKO LA KOMPYUTA
Kuna sababu nyingi za kushuka kwa kiwango cha uzalishwaji na utumiaji wa kopyuta za mezani,wengine wanatoa lawama kwa toleo jipya la Window 8,wengine wanatoa sababu za kushuka kwa soko kutokana na kudolola kwa uchumi duniani
Hata hivyo ukiangalia kiuhalisia waweza gundua kuwa kupungua kwa matumizi ya kompyuta za mezani kulianza katika robo ya pili ya mwaka 2010 na sababu kubwa inayoelezwa ni baada ya kuwa sokoni kwa kifaa cha mawasilino cha iPad .
Tovuti ya statista imeeleza kuwa toka kampuni ya Apple ilipoingiza sokoni tabiti kwa kutoa iPad ya kwanza Aprili 2010, usambazwaji wa kompyuta za mezani umeshuka PC ambapo sasa umeshuka na kufikia kiwango cha asilimia 8.6.
Apple ilifanikiwa kuuza iPad milioni 20 kwa mara ya kwanza ilipoingiza sokoni vifaa hivyo.
Mtandao wa Gartner umekadiria kuwa ukuaji wa usafirishaji wa tabiti duniani kote utakua kutoka tabiti milioni 76 kwa mwaka 2011 na itafikia mara tano zaidi ifikapo mwaka 2017
Katika robo ya tatu ya mwaka 2009, Toshiba ilisafirisha kompyuta za mezani milioni 4.01 duniani idadi ambayo ni sawa na ile ya robo ya kwanza ya mwaka 2013, Hewlett-Packard (HP) ndio iliyokuwa ikiongoza kwa kusafirisha idadi kubwa ambapo inakadiriwa kusafirisha komputa za mezani milioni 11.69 katika kipindi hicho cha mwaka.
Takwimu za awali zilionesha kuwa hadi kufikia robo ya nne ya mwaka 2012 inakadiriwa kuwa kompyuta zilizosafirishwa kwenda sehemu mbalimbali duniani toka kwa makampuni yanayozitengeneza zilikuwa milioni 90.
Tabiti zimewapa watumiaji wa kompyuta nafasi nyingine ya kuchagua njia mbadala ya matumizi sawa na yale wanayoweza kuyapata toka katika kompyuta hasa katika suala la matumizi binafsi na bei ya vifaa hivyo.
Popular Posts
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Kampuni ya simu Tanzania (TTCL) inatarajia kuzindua kituo kikubwa cha kuuzia intaneti Afrika Mashariki mwishoni mwa mwezi julai au Agosti mw...
-
Afisa wa Taasisi ya uwezeshaji na ujengaji uwezo kwa wateknohama nchini KINU, Catherinerose Barretto akimkabidhi cheti Ally Said toka P...
-
MASWALI NA MAJIBU KUHUSU KUVURUGA PROGRAMU YA WINXP 1 – PROGRAMU YA WIN XP KUVURUGIKA Sio ukweli kwamba programu ya win xp itavuruguka...
-
Meneja Uhusiano wa kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Thomas Mushi akizungumza na vyombo vya habari leo jijini Dar es Salaam...
-
Mamlaka ya Mawasilino Tanzania, TCRA, imesema watumiaji wa namba za simu ambazo hazikusajiliwa, watakatiwa mawasiliano ifikapo Juni M...
-
Mwishoni mwa juma lililopita pamegundulika hali mbaya ya kiusalama mtandao itakayo waathiri watumiaji wa kivinjari kijulikanacho kama...