Tuesday, September 22, 2015

ARUSHA:TCRA YASEMA BADO KUNA MATATIZO YANAYOTOKANA NA WATUMIAJI WA MAWASILIANO


 

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) Dr. Ally Yahaya Simba(Pichani),amesema pamoja na mafanikio katika sekta ya mawasiliano nchini Tanzania lakini bado kuna matatizo  yanayojitokeza ikiwemo ukiukwaji wa kwa sheria za mawasiliano.

Ameyasema hayo jijini Arusha alipofanya ziara yake fupi ya utambulisho katika kanda ya kaskazini huku kaiwataka wadau wa mawasiliano na vyombo vya Habari nchini kumpa ushirikiano ili kuboresha sekta hiyo katika kipindi cha uongozi wake.

Dr. Ally Simba amesema pamoja mafanikio yaliyopo katika sekta ya Mawasiliano nchini lakini bado kuna matatizo yanayojitokea kutokana na  watumiaji wa huduma ya mawasiliano ikiwemo ukiukwaji wa masharti ya leseni na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii.

Aidha amewapongeza wadau wa Mawasiliano na vyombo vya habari kwa kuzingatia sheria na kanuni za utoaji wa Habari na utangazaji katika msimu huu wa kampeni za uchaguzi mkuu.



Popular Posts

Labels