Thursday, September 24, 2015

DAR ES SALAAM:BASATA LATAKA KUONDOLEWA/KUSITISHWA MARA MOJA KUCHEZWA KWA NYIMBO ZOTE ZILIZOKINYUME CHA MAADILI, SHERIA NA TARATIBU



 
Baraza la Sanaa la Taifa nchini Tanzania (BASATA) limetoa siku saba kwa wasanii,vituo vya radio,runinga wamiliki wa tovuti na wale wenye wasifu kwenye mitandao ya kijamii kuondoa nyimbo zote au maudhui yenye muelekeo unaoenda kinyume na maadili,  matusi  na kashfa mbalimbali.

Taarifa ya BASATA iliyotiwa saini na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo Godfrey Mngereza imevitaka  pia vyombo vya habari zikiwemo radio na luninga kuondoa na kuacha mara moja kucheza au kurusha nyimbo zote zenye maudhui hayo.

Mngereza amesema maudhui ya kashfa,matusi,kejeli,udhalilishaji zinatishia kuigawa jamii ya watanzania katika kipindi hiki ambacho taifa linaendelea na kampeni za kujiandaa na uchaguzi mkuu tarehe 25 mwezi wa kumi mwaka huu.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa  kifungu namba 118 [a-d] cha sheria ya bunge namba 9 ya mawasiliano ya mtandao ya mwaka 2010 vinaelekeza kuwa ni marufuku kwa njia yoyote kwa mtu au chombo chochote kutengeneza ujumbe ambao unamlengo wa matusi ,dharau,uzushi au jinai kwa lengo la kutukana ,kutisha, kusumbua au kushusha hadhi  ya mtu mwingine.



Popular Posts

Labels