Tuesday, September 22, 2015

MICROSOFT YAWATAKA WATUMIAJI WA KOMPYUTA KUTUMIA PROGRAM ZENYE VIWANGO


 

Kampuni  ya Microsoft imesema kuwa watumiaji wa program za kompyuta, wanapaswa kutumia program zenye viwango na kujiepusha na zisizo na viwango.

Akizungumza hii leo katika mkutano wa matumizi ya program za kompyuta,Afisa mtendaji na msimamizi wa Hakimiliki wa COSOTA, Dorine Sinare amesema kuwa, kutumia program za kompyuta zilizo bora zitasaidia kuepuka uharamia katika mitandao na serikali kuweza kuongeza mapato yaliyotokana na program hizo.

Dorine amesema kuwa wameanza kushirikiana na Microsoft katika kuweza kutoa elimu juu ya matumizi ya program ambazo halisi na kuachana na ambazo si halisi kwani zinaweza kuharibu program zingine.

Njiru ameongeza kuwa Microsoft inafanya kazi katika kuhakikisha watu wanapata mawasiliano yenye kiwango kutokana na utoaji wa huduma za program za komputa zenye kiwango.

Popular Posts

Labels