Mahakama ya kimataifa ya ICC imetoa onyo kali kwa wanablogu nchini
Kenya,wanaotoa taarifa kuhusu mashahidi waliofika mbele ya mahakama ya
ICC.
Hii ni baada ya taarifa kuhusu shahidi wa kwanza mbele ya
mahakama hiyo kujitokeza kwenye mitandao hasa kwenye blogu, twitter na
Facebook kumhusu.
Blogu hiyo ya udaku pia ilichapisha picha ya mwanamke huyo
Baadhi
ya taarifa zilisema kuwa amewahi kutoa ushahidi wake ambao
haukutofautiana na alioiambia mahakama ya ICC, katika mahakama nchini
Kenya lakini ukapuuziliwa mbali na mahakama.
Mashahidi hao wanatoa
ushahidi wao ndani ya mahakama ila wamefichwa nyuso zao hatua
iliyochukuliwa ili kuwalinda kutokana na tisho lolote dhidi ya maisha
yao.
ICC huenda ikachukua hatua za kisheria dhidi ya wanaosambaza taarifa kuhusu mashahidi wanaofika mbele ya mahakama hiyo.
Jaji
anayeongoza vikao hivyo, Chile Eboe-Osuji, alisema kuwa ni makosa
kisheria kuwafichua mashahidi wakati mahakama imebana kuwatambulisha.
Shahidi
huyo ambaye wenye blogu wanasema wanamfahamu, ni mwanamke mwathiriwa wa
shambulizi dhidi ya Kanisa la Kiambaa ambako yeye na wanakijiji wenzake
walitafuta hifadhi wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi kutokota
katika mkoa wa Rift Valley.
Watu zaidi ya thelathini waliteketezwa wakiwa hai ndani ya kanisa hilo.
Chanzo:BBC
Popular Posts
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na wamiliki wa blog nchini humo inatarajia kuanzisha tuzo za umahiri kwa waandishi wa haba...
-
Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 25 ambaye alidukua komputa za Chuo Kikuu cha Birmingham na kuongeza alama za mtihani amefungwa...
-
Kampuni ya simu Tanzania (TTCL) inatarajia kuzindua kituo kikubwa cha kuuzia intaneti Afrika Mashariki mwishoni mwa mwezi julai au Agosti mw...
-
Serikali ya Tanzania imesema inatoza kodi ya shilingi 1,000 kwa mwezi kwa kila laini yenye namba ya simu.Umoja wa Makampuni ya mi...
-
Facebook ni mtandao wa kijamii ambao unaendelea kuongoza kwa kuwa na watumiaji wengi duniani hata hiyo utafiti unaonesha kuwa vijana ...
-
Google I/O ni kongamano linalofanyika kila mwaka California kwa kuwakutanisha Developers wa bidhaa za Google kama Android , Chrome , Chrom...
-
Afisa wa Taasisi ya uwezeshaji na ujengaji uwezo kwa wateknohama nchini KINU, Catherinerose Barretto akimkabidhi cheti Ally Said toka P...
-
Idadi ya watu wanaotumia huduma ya mtandao wa Intaneti nchini Tanzania imeongezeka kutoka watu 26,000 mwaka 2000 hadi kufikia watu mili...