Mahakama ya kimataifa ya ICC imetoa onyo kali kwa wanablogu nchini
Kenya,wanaotoa taarifa kuhusu mashahidi waliofika mbele ya mahakama ya
ICC.
Hii ni baada ya taarifa kuhusu shahidi wa kwanza mbele ya
mahakama hiyo kujitokeza kwenye mitandao hasa kwenye blogu, twitter na
Facebook kumhusu.
Blogu hiyo ya udaku pia ilichapisha picha ya mwanamke huyo
Baadhi
ya taarifa zilisema kuwa amewahi kutoa ushahidi wake ambao
haukutofautiana na alioiambia mahakama ya ICC, katika mahakama nchini
Kenya lakini ukapuuziliwa mbali na mahakama.
Mashahidi hao wanatoa
ushahidi wao ndani ya mahakama ila wamefichwa nyuso zao hatua
iliyochukuliwa ili kuwalinda kutokana na tisho lolote dhidi ya maisha
yao.
ICC huenda ikachukua hatua za kisheria dhidi ya wanaosambaza taarifa kuhusu mashahidi wanaofika mbele ya mahakama hiyo.
Jaji
anayeongoza vikao hivyo, Chile Eboe-Osuji, alisema kuwa ni makosa
kisheria kuwafichua mashahidi wakati mahakama imebana kuwatambulisha.
Shahidi
huyo ambaye wenye blogu wanasema wanamfahamu, ni mwanamke mwathiriwa wa
shambulizi dhidi ya Kanisa la Kiambaa ambako yeye na wanakijiji wenzake
walitafuta hifadhi wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi kutokota
katika mkoa wa Rift Valley.
Watu zaidi ya thelathini waliteketezwa wakiwa hai ndani ya kanisa hilo.
Chanzo:BBC
Popular Posts
-
Mkurugenzi Msaidizi anayeshughulikia masuala ya Simu katika Wizara ya Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano Ndugu John Mwera akizungumza ...
-
Kanisa la Waadventista Wa Sabato mwaka huu litashiriki mkutano wa Waadventista watalaamu wa mawasilino ya Intaneti duniani (GAiN) kwa k...
-
Mkuu wa Huduma za Fedha kwa njia ya simu wa Tigo Ruan Swanepoel (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam...
-
Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa JWTZ-Kanali Ngemela Lubingo (Chanzo:Mwananchi) Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) lime...
-
Shule ya Msingi ya Mlimani iliyopo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuanzia wiki hii itaanza kunufaika na huduma ya intaneti bure inayofung...
-
Imeelezwa kwamba kadri teknolojia inavyoongezeka, inatengeneza fursa ya kukua kwa Shirika la Posta Duniani. Hayo yamesemwa na Kai...
-
Mkuu wa wa Kitengo cha Huduma za Kifedha wa Tigo, Ruan Swanepoel (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es ...
-
Na Yusuph Kileo Nchi ya Tanzania yabahatika tena kwa mara ya tatu kuwa mwenyeji wa mkutano wa “Connect 2 Connect” ambapo kauli mbiu ya...
-
Wapiga kura 2,845,256 wameandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapigakura kwa mfumo wa kielektroniki wa utambuzi wa mwili wa binada...