Mahakama ya kimataifa ya ICC imetoa onyo kali kwa wanablogu nchini
Kenya,wanaotoa taarifa kuhusu mashahidi waliofika mbele ya mahakama ya
ICC.
Hii ni baada ya taarifa kuhusu shahidi wa kwanza mbele ya
mahakama hiyo kujitokeza kwenye mitandao hasa kwenye blogu, twitter na
Facebook kumhusu.
Blogu hiyo ya udaku pia ilichapisha picha ya mwanamke huyo
Baadhi
ya taarifa zilisema kuwa amewahi kutoa ushahidi wake ambao
haukutofautiana na alioiambia mahakama ya ICC, katika mahakama nchini
Kenya lakini ukapuuziliwa mbali na mahakama.
Mashahidi hao wanatoa
ushahidi wao ndani ya mahakama ila wamefichwa nyuso zao hatua
iliyochukuliwa ili kuwalinda kutokana na tisho lolote dhidi ya maisha
yao.
ICC huenda ikachukua hatua za kisheria dhidi ya wanaosambaza taarifa kuhusu mashahidi wanaofika mbele ya mahakama hiyo.
Jaji
anayeongoza vikao hivyo, Chile Eboe-Osuji, alisema kuwa ni makosa
kisheria kuwafichua mashahidi wakati mahakama imebana kuwatambulisha.
Shahidi
huyo ambaye wenye blogu wanasema wanamfahamu, ni mwanamke mwathiriwa wa
shambulizi dhidi ya Kanisa la Kiambaa ambako yeye na wanakijiji wenzake
walitafuta hifadhi wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi kutokota
katika mkoa wa Rift Valley.
Watu zaidi ya thelathini waliteketezwa wakiwa hai ndani ya kanisa hilo.
Chanzo:BBC
Popular Posts
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
Huduma ya ujumbe Whatsapp imetangaza kuwa itayalinda mawasiliano ya wateja wake kuanzia hapo siku ya Jumanne April 5,mwaka huu Huk...
-
Serikali ya Tanzania inapenda kuufahamisha umma wa Watanzania kuwa hivi karibuni kumezuka kundi la Watu wadanganyifu ambao wamekuwa wakit...
-
Serikali ya Kenya imesema watu watakaopatikana na hatia ya kutuma ujumbe wa kingono kwa kutumia simu za kiganjani na intaneti watafungw...
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Benki ya CRDB imewaonya wateja wake kuwa makini na baadhi ya mitandao inayoibuka na kulaghai kwa kuwataka wananchi,kutoa taarifa zao muhimu ...
-
ILI kuboresha utoaji huduma kwa umma hivi karibuni Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeanzisha utaratibu wa kupokea malala...
-
Kuwa na Akaunti ya Facebook ni kwa manufaa yako na manufaa ya Facebook Facebook ambayo kwa sasa inapatikana katika lugha 70 ul...
-
Maofisa wa WAMOJA ICT Consulting Limited Mtangazaji Maduhu na WAMOJA ICT Consulting Limited Kampuni ya WAMOJA ICT Consulting Li...