Mahakama ya kimataifa ya ICC imetoa onyo kali kwa wanablogu nchini
Kenya,wanaotoa taarifa kuhusu mashahidi waliofika mbele ya mahakama ya
ICC.
Hii ni baada ya taarifa kuhusu shahidi wa kwanza mbele ya
mahakama hiyo kujitokeza kwenye mitandao hasa kwenye blogu, twitter na
Facebook kumhusu.
Blogu hiyo ya udaku pia ilichapisha picha ya mwanamke huyo
Baadhi
ya taarifa zilisema kuwa amewahi kutoa ushahidi wake ambao
haukutofautiana na alioiambia mahakama ya ICC, katika mahakama nchini
Kenya lakini ukapuuziliwa mbali na mahakama.
Mashahidi hao wanatoa
ushahidi wao ndani ya mahakama ila wamefichwa nyuso zao hatua
iliyochukuliwa ili kuwalinda kutokana na tisho lolote dhidi ya maisha
yao.
ICC huenda ikachukua hatua za kisheria dhidi ya wanaosambaza taarifa kuhusu mashahidi wanaofika mbele ya mahakama hiyo.
Jaji
anayeongoza vikao hivyo, Chile Eboe-Osuji, alisema kuwa ni makosa
kisheria kuwafichua mashahidi wakati mahakama imebana kuwatambulisha.
Shahidi
huyo ambaye wenye blogu wanasema wanamfahamu, ni mwanamke mwathiriwa wa
shambulizi dhidi ya Kanisa la Kiambaa ambako yeye na wanakijiji wenzake
walitafuta hifadhi wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi kutokota
katika mkoa wa Rift Valley.
Watu zaidi ya thelathini waliteketezwa wakiwa hai ndani ya kanisa hilo.
Chanzo:BBC
Popular Posts
-
Google imezindua simu ya kisasa ya bei rahisi barani Afrika. Simu hiyo, Hot 2 ambayo haina 'makorokoro' mengi itaanza kupati...
-
Maswala ya udukuzi yameendelea kushika kasi katika maeneo mbali mbali ulimwenguni ambapo mataifa mbali mbali yameamua kuunganisha nguvu ...
-
WAZIRI wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania, Profesa Makame Mbarawa, amesema uchumi wa Tanzania unaweza kukua kati ya asil...
-
Jeshi la Kujenga Taifa JKT limekanusha taarifa zinazosambazwa kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu za mkononina mitandao y...
-
Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es salaam wakiwa wamepanga foleni ili kununua umeme jana Huduma ya manunuzi ya umeme kwa njia ya miamala...
-
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dares Salaam leo. ...
-
Itakumbukwa Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huu katika hotuba yangu niliyo iwasilisha kwa wanausalama mitandao tulipo kutana jijini Johan...
-
Mtaalamu wa masuala ya usalama kwenye Mtandao Yusuph Kileo akiwasilisha mada Itakumbukwa katika mkutano uliofanyika mapema mwezi h...
-
Yusuph Kileo akitoa mada kwenye mkutano huo Mazungumzo ya awali kabla ya mkutano wa wanausalama mitandao uliokamilika jijini Johann...
-
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Kudumu za Serikali imebaini madudu yanayofanyika katika uwekezaji wa kampuni za simu nchini Tanzania ...