Saturday, September 7, 2013

FAHAMU KUHUSU TEKNOLOJIA YA VIBER-KUPIGA SIMU KWA BEI NAFUU

 

Viber ni teknolojia ya mawasiliano iliyoanzishwa kwa ajili ya mawasiliano ya papo kwa papo ya ujumbe wa sauti kupitia njia ya program tumishi ya sauti kupitia intaneti  VoIP kwa ajili ya simu za kisasa (Smartphone) na tabiti iliyobuniwa na Viber Media.

Pamoja na ujumbe wa mfupi wa maneno,watumiaji wanaweza kupigiana simu, kubadilishana picha,video na ujumbe wa sauti.Teknolojia hii yaweza tumika vifaa vya mawasiliano vinavyotumia progam tumishi zenye mifumo ya    Mac, Android, BlackBerry , iOS, Series 40, Symbian, Bada, Windows,Microsoft Windows Linux katika mitandao ya mawasiliano ya 3G/4G na Wi-Fi.

Takwimu zilizotolewa hivi karibuni na mtandao wa wikipedia zinaonesha kuwa mpaka kufikia Mei 7,2013 tayali watu milioni  200 million duniani wameshajiunga na Viber na tayali imeshaanza kutumika katika lugha 30 duniani.

 Viber  ilikubaliwa kutumika kwa mara ya kwanza katika  iPhone Disemba  2, 2010, ikiwa na ushindani na Skype.Baada ya hapo lilitolewa toleo jipya kwa simu za  Android mei  2011 lakini lilikuwa ni maalum kwa watumiaji  50,000 tu ndipo Julai 19,2012 lilipotolewa toleo la kutumiwa na watu wote 

 Viber kwa ajili ya BlackBerry na simu  Windows ilizunduliwa mei 8, 2012. Ambapo julai 24,2012 watu milioni 90 duniani  walikuwa wameshajiunga na teknolojia hii ya mawasiliano. million users on July 24, 2012,nakuongeza matumizi katika simu za  Android, iPhone, Nokia Series 40,Symbian na Samsung Bada

Mfumo wa mawasiliano wa sauti kupitia  Viber  katika simu za l Windows 8 ulianza kutumika  April 2, 2013.

Teknojia hii inakuwezesha mtumiaji kuwasiliana na mtu ambaye na  amejiunga kupitia namba yake ya simu ambapo unaweza kumpigia simu ikiwa simu zenu zinaina internet iwe ni katika nchi uliyopo ama nje ya nchi 


Viber Media ni kampuni iliyoko Cyprus ikiwa na vituo vyake Belarus na  Israel.Kampuni hii ilinzishwa na mmarekani mwenye asili ya Israeli mjasiriamali  Talmon Marco.


Kwa sasa kampuni hiyo haipatati mapato japo imetangaza kuwa itaanza kufanya hivyo mwaka 2013 kupitia matangazo ya biashara na mpaka kufikia mwezi mei mwaka 2013 jumla ya dola za kimarekani milioni 20 sawa na shilingi bilioni 30 za kitanzania zimeshawekezwa katika kampuni hiyo.


Kama unatabiti ama smartphone tafuta program tumishi inaitwa Viber ipakue na uiweke kwenye tabiti ama simu yako na fuata maelekezo,waweza tembelea hapa viber ama hapa viber.


.

Popular Posts

Labels