Friday, September 20, 2013

VYUO VIKUU VYA UINGEREZA KUTOA ELIMU BURE KWA NJIA YA TEKNOHAMA




Vyuo Vikuu 23 nchini Uingereza kwa kushirikiana na taasisi 3 zinazojihusisha na masuala ya siasa na utamaduni wa nchi hiyo vimeanzisha mafunzo ya bure kwa watu wote duniani kwa kwa njia ya teknohama ( elimu mtandao) ambayo yataanza Oktoba 2013.

Utaratibu huo unaojulikana kwa jina la .future Learn utatoa mafunzo ya Ujasiriamali,Teknohama,Afya,Mazingira,Siasa,Sayansi,Usimamizi wa Biashara na  masuala ya kurekodi muziki,mafunzo hayo ni mwendelezo wa vyuo hivyo wa kutoa elimu masafa kwa kipindi cha miaka 40 iliyopita.

Mafunzo haya yatakuwa yakitolewa bure kwa njia ya mtandao kupitia kompyuta,tabiti na simu za mkononi zenye uwezo wa kupata intanet.

Kujiunga na mafunzo hayo bofya hapa futurelearn

Popular Posts

Labels