Kampuni ya Simu za Mkononi ya Airtel Tanzania imesema kuwa imeshazima laini za simu 200,000 ikiwa ni utekelezaji wa sheria ya posta na mawasiliano ya kielektroniki ya mwaka 2010 ikimbatana na muda wa mwisho wa kusajili laini za simu nchini Tanzania kuwa ni julai 10,2013 uliowekwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Usimamizi wa Sheria wa Airtel Tanzania Beatrice Singano amesema waliwajulisha wateja wao mapema kusajili laini zao za simu ili kuepuka kufungwa kwa laini za wateja wao.
Amesema kuanzia julai 10 mwaka huu kama mamlaka ya mawasiliano Tanzania ilivyotangaza Aprili mwaka huu kwa sasa jumla ya wateja 200,000 wa kampuni hiyo wamefungiwa laini zao kutokana na kutosajili.
Ili kufahamu laini ya simu imesajili mmiliki wa simu anapaswa kuhakiki usajili huo kwa kupiga *106#.
Usajili wa namba za simu kama ilivyo katika nchi mbalimbali duniani umekuwa ukiendelea na kwa miaka michache katika nchi za Afrika Mashariki lengo likiwa ni kudhibiti matukio ya uharifu yanayofanywa ama kuanzishwa na watumiaji wa simu za mikononi katika nchi hizo.
Popular Posts
-
Mamlaka ya Mawasilino Tanzania, TCRA, imesema watumiaji wa namba za simu ambazo hazikusajiliwa, watakatiwa mawasiliano ifikapo Juni M...
-
Polisi kanda maalumu ya Dar es salaam wamezungumzia utapeli unaofanywa kwa kutumia simu za mkononi na kusema wengi wanaofanya hivyo husajili...
-
Google I/O ni kongamano linalofanyika kila mwaka California kwa kuwakutanisha Developers wa bidhaa za Google kama Android , Chrome , Chrom...
-
Afisa wa Taasisi ya uwezeshaji na ujengaji uwezo kwa wateknohama nchini KINU, Catherinerose Barretto akimkabidhi cheti Ally Said toka P...
-
Picha na Salim Kikeke Kuanzia sasa kudanganya kwamba mtu hakupata ujumbe wako wa WhatsApp itakuwa historia, au kud...
-
Microsoft is switching off its Windows Live Messenger service on 15 March. On that date Messenger log-ins will no longer work a...
-
Mwezeshaji wa kipindi cha Maisha na Teknohama cha Morning Star Radio,Johnson Mziray akichangia jambo kwenye warsha hiyo,pembeni yake mweny...
-
Kumetokea matukio kadhaa ya wizi kwa njia ya mtandao unaohusisha simu za mikononi katika utoaji wa fedha ingawa pesa nyingi zimetolewa kwa ...
-
Idadi ya watu wanaotumia huduma ya mtandao wa Intaneti nchini Tanzania imeongezeka kutoka watu 26,000 mwaka 2000 hadi kufikia watu mili...