Kampuni ya Simu za Mkononi ya Airtel Tanzania imesema kuwa imeshazima laini za simu 200,000 ikiwa ni utekelezaji wa sheria ya posta na mawasiliano ya kielektroniki ya mwaka 2010 ikimbatana na muda wa mwisho wa kusajili laini za simu nchini Tanzania kuwa ni julai 10,2013 uliowekwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Usimamizi wa Sheria wa Airtel Tanzania Beatrice Singano amesema waliwajulisha wateja wao mapema kusajili laini zao za simu ili kuepuka kufungwa kwa laini za wateja wao.
Amesema kuanzia julai 10 mwaka huu kama mamlaka ya mawasiliano Tanzania ilivyotangaza Aprili mwaka huu kwa sasa jumla ya wateja 200,000 wa kampuni hiyo wamefungiwa laini zao kutokana na kutosajili.
Ili kufahamu laini ya simu imesajili mmiliki wa simu anapaswa kuhakiki usajili huo kwa kupiga *106#.
Usajili wa namba za simu kama ilivyo katika nchi mbalimbali duniani umekuwa ukiendelea na kwa miaka michache katika nchi za Afrika Mashariki lengo likiwa ni kudhibiti matukio ya uharifu yanayofanywa ama kuanzishwa na watumiaji wa simu za mikononi katika nchi hizo.
Popular Posts
-
Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na wamiliki wa blog nchini humo inatarajia kuanzisha tuzo za umahiri kwa waandishi wa haba...
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
Kampuni ya simu Tanzania (TTCL) inatarajia kuzindua kituo kikubwa cha kuuzia intaneti Afrika Mashariki mwishoni mwa mwezi julai au Agosti mw...
-
Serikali ya Tanzania imesema inatoza kodi ya shilingi 1,000 kwa mwezi kwa kila laini yenye namba ya simu.Umoja wa Makampuni ya mi...
-
Facebook ni mtandao wa kijamii ambao unaendelea kuongoza kwa kuwa na watumiaji wengi duniani hata hiyo utafiti unaonesha kuwa vijana ...
-
Afisa wa Taasisi ya uwezeshaji na ujengaji uwezo kwa wateknohama nchini KINU, Catherinerose Barretto akimkabidhi cheti Ally Said toka P...
-
Idadi ya watu wanaotumia huduma ya mtandao wa Intaneti nchini Tanzania imeongezeka kutoka watu 26,000 mwaka 2000 hadi kufikia watu mili...
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 25 ambaye alidukua komputa za Chuo Kikuu cha Birmingham na kuongeza alama za mtihani amefungwa...