Friday, April 25, 2014

MITAMBO YA ANALOJIA KUZIMWA BUKOBA NA MUSOMA APRIL 30 MWAKA HUU

Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) inatarajia kuzima rasmi mitambo ya analojia ya urushaji wa matangazo ya televisheni katika miji ya Bukoba mkoani Kagera na Musoma,Mara mwishoni  mwa mwezi huu.
Naibu Mkurugenzi Idara ya Utangazaji wa Mamlaka hiyo,Frederick Ntobi amesema zoezi hilo la uzimaji wa mitambo hiyo na kuhamia dijitali katika miji hiyo litaendeshwa saa 6:00 usiku.
Kwa mujibu wa Ntobi,zoezi hilo litahusisha mitambo inayotumia mfumo wa satelaiti,matangazo kwa njia ya waya au mitambo ya radio. Amesema uzimaji wa mitambo hiyo ni awamu ya pili baada ya kwanza kuhusisha mikoa ya Dar es salaam,Mbeya,Tanga,Mwanza,Arusha na Mbeya.
Aliwataka wakazi wa wilaya hizo za Bukoba na Musoma kuhakikisha wananunua ving'amuzi ili waweze kuangalia vipindi mbalimbali vya kwenye televisheni.

Popular Posts

Labels