Mamlaka
ya mawasiliano Tanzania (TCRA) inatarajia kuzima rasmi mitambo ya
analojia ya urushaji wa matangazo ya televisheni katika miji ya Bukoba mkoani Kagera na Musoma,Mara mwishoni
mwa mwezi huu.
Naibu
Mkurugenzi Idara ya Utangazaji wa Mamlaka hiyo,Frederick Ntobi amesema
zoezi hilo la uzimaji wa mitambo hiyo na kuhamia dijitali katika miji
hiyo litaendeshwa saa 6:00 usiku.
Kwa mujibu wa Ntobi,zoezi hilo litahusisha mitambo inayotumia mfumo wa satelaiti,matangazo kwa njia ya waya au mitambo ya radio.
Amesema
uzimaji wa mitambo hiyo ni awamu ya pili baada ya kwanza kuhusisha
mikoa ya Dar es salaam,Mbeya,Tanga,Mwanza,Arusha na Mbeya.
Aliwataka
wakazi wa wilaya hizo za Bukoba na Musoma kuhakikisha wananunua
ving'amuzi ili waweze kuangalia vipindi mbalimbali vya kwenye
televisheni.
Popular Posts
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Unapomblock mtu kwenye viber inamaana umezuia kuwasiliana na mtu yoyote kwa njia yoyote katika mtandao wa kijamii wa viber,huta...
-
ILI kuboresha utoaji huduma kwa umma hivi karibuni Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeanzisha utaratibu wa kupokea malala...
-
KAMA HAUKUJUA BASI JUA Na MBUKE TIMES Neno HACKER makusudio yake haswa sio kumaanisha mtu anayefanya vitendo vya kihalifu kwa kutu...
-
Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) inatarajia kuzima rasmi mitambo ya analojia ya urushaji wa matangazo ya televisheni katika miji ya ...