Mamlaka
ya mawasiliano Tanzania (TCRA) inatarajia kuzima rasmi mitambo ya
analojia ya urushaji wa matangazo ya televisheni katika miji ya Bukoba mkoani Kagera na Musoma,Mara mwishoni
mwa mwezi huu.
Naibu
Mkurugenzi Idara ya Utangazaji wa Mamlaka hiyo,Frederick Ntobi amesema
zoezi hilo la uzimaji wa mitambo hiyo na kuhamia dijitali katika miji
hiyo litaendeshwa saa 6:00 usiku.
Kwa mujibu wa Ntobi,zoezi hilo litahusisha mitambo inayotumia mfumo wa satelaiti,matangazo kwa njia ya waya au mitambo ya radio.
Amesema
uzimaji wa mitambo hiyo ni awamu ya pili baada ya kwanza kuhusisha
mikoa ya Dar es salaam,Mbeya,Tanga,Mwanza,Arusha na Mbeya.
Aliwataka
wakazi wa wilaya hizo za Bukoba na Musoma kuhakikisha wananunua
ving'amuzi ili waweze kuangalia vipindi mbalimbali vya kwenye
televisheni.
Popular Posts
-
Microsoft is switching off its Windows Live Messenger service on 15 March. On that date Messenger log-ins will no longer work a...
-
Watu wengi wameshaona filamu ambazo wahalifu wakidukua simu za mikononi hata kama zimezimwa. Kama ili...
-
Na Yusuph Kileo Nchi ya Tanzania yabahatika tena kwa mara ya tatu kuwa mwenyeji wa mkutano wa “Connect 2 Connect” ambapo kauli mbiu ya...
-
Kutoka Kushoto Gerald Masatu,Mtangazaji Maduhu,Brown Nyanza(IFM),Mama Kagize,Johnson Kuga Mzirai na Jonathan Mnyela Jonathan Mnyela ...
-
Imeelezwa kuwa wananachi wengi bado hawana uelewa wa kutosha juu ya haki zao za msingi katika huduma za mawasiliano wanazotumia, hali ambayo...
-
Wakati bado mafanikio mbali mbali yakijadiliwa wahalifu mtandao wamegundulika kuja na uhalifu unaotafsiriwa kuwa ni wa kihistoria na uliof...
-
Jeshi la Polisi Tanzania limeanza kunasa watu wanaodaiwa kutuma ujumbe wa matusi na wengine kupiga simu kwa spika wa Bunge la nchi hiyo Anne...