Monday, April 28, 2014

SHULE YA TASS YAPATA KOMPUTA 50

Shule ya sekondari ya Waadventista Wa Sabato  {Tass} imepokea jumla ya komputa hamsini zitakazotumika katika mafunzo ya utafiti kivitendo katika maabara ya kisasa ya sayansi iliyozinduliwa hivi karibuni.
 

Hayo yamesemwa na mkuu wa shule hiyo mwl joseph kehengu wakati akiwasilisha taarifa ya shule kwa mgeniRasmi,wanahabari,wanafunzi na wazazi kwenye mahafali ya kwanza ya kidato cha sita Tangu shule ianzishwe mwka 1999.Bwana joseph alisema kuwa computa hizo zilizotolewa na mmiliki wa shule hiyo ambaye ni kanisa la waadventista wasabato Tanzania zitaleta mwamko mkubwa na hamasa kwa wanafunzi kupenda masomo ya sayansi na zitawezesha utafiti wa maswala ya kisayansi kufanyika kwa ufanisi zaidi.
 

Kwa upande mwingine akijibu risala ya wanafunzi pamoja na taarifa ya mwalimu mkuu wa shule katika mahafali ya kwanza ya kidato cha sita yaliyofanyika jana April 27 /2014 Mgeni rasmi katika mahafali hayo ndugu Wilson Kabwe mkurugenzi wa jiji la 
Dar es salaam awaasa wanafunzi wahitimu kutoridhika na kiwango walichofika badala yake awasonge mbele zaidi kielimu.

           

Popular Posts

Labels