Serikali ya Tanzania imewatahadharisha wananchi kuzingatia matumizi sahihi ya Teknolojia ya
Habari na Mawasiliano (TEKINOHAMA) ili kuondoa vitendo vya uhalifu hapa
nchini.
Hayo
yamesemwa na Kaimu Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Serikalini Bi Prisca
Ulomi wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es
salaam.
Akifafanua Bi Prisca amesema kuwa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia kwa kutambua umuhimu wa TEKINOHAMA wameamua kuandaa muswada wa Sheria za Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao (Cyber Laws).
Akieleza
zaidi Bi Prisca amesema kuwa Muswada wa sheria hizo ni pamoja na
Muswada wa Sheria ya Kulinda Taarifa Binafsi (The Personal Data
Protection Bill), Muswada wa Sheria ya Biashara ya Miamala ya
Kielektroniki (Electronic Transaction Bill), na Muswada wa Sheria ya
Kuzuia Uhalifu kwa njia ya Kompyuta na Mtandao (Computer and Cyber
Crimes Bills).
“Sheria hizo zitasaidia kuimarisha matumizi ya
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano hapa nchini kwa kudhibiti uhalifu
kwa kutumia mitandao na kuwalinda watoto dhidi ya matumizi yasiyofaa ya
mitandao”. alisema Bi Prisca.
Bi Prisca aliongeza kuwa serikali
imetumia gharama kubwa kuweka miundombinu ya TEHAMA ambayo imesaidia
kuboresha na kuharakisha utoaji wa huduma mbalimbali na kubainisha kuwa
wapo baadhi ya watu wanatumia vibaya teknolojia hiyo, hivyo kuna umuhimu
wa kuwepo sheria zitakazodhibiti uhalifu kupitia mitandao.
Wizara
ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia imetoa rai kwa wananchi
kujiepusha na matumizi mabaya ya mitandao na badala yake watumie vizuri
mitandao hiyo kwa maendeleo yao na taifa kwa ujumla hali inayoweza
kuathiri ukuaji wa sekta hiyo nchini.
Tuesday, April 1, 2014
Popular Posts
-
MASWALI NA MAJIBU KUHUSU KUVURUGA PROGRAMU YA WINXP 1 – PROGRAMU YA WIN XP KUVURUGIKA Sio ukweli kwamba programu ya win xp itavuruguka...
-
MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLEMkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideo...
-
Mwishoni mwa juma lililopita pamegundulika hali mbaya ya kiusalama mtandao itakayo waathiri watumiaji wa kivinjari kijulikanacho kama...
-
Afisa wa Taasisi ya uwezeshaji na ujengaji uwezo kwa wateknohama nchini KINU, Catherinerose Barretto akimkabidhi cheti Ally Said toka P...
-
Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia ,Bw Charles Kitwanga ameyashawishi mataifa ambayo tayari yamejiunga na mfumo wa Digitali katika haraka...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kwa kuzingatia kifungu 5 (b) na (e) cha Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ya 2003 inatoa t...
-
Meneja Uhusiano wa kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Thomas Mushi akizungumza na vyombo vya habari leo jijini Dar es Salaam...
-
Mamlaka ya Mawasilino Tanzania, TCRA, imesema watumiaji wa namba za simu ambazo hazikusajiliwa, watakatiwa mawasiliano ifikapo Juni M...