Serikali ya Tanzania imewatahadharisha wananchi kuzingatia matumizi sahihi ya Teknolojia ya
Habari na Mawasiliano (TEKINOHAMA) ili kuondoa vitendo vya uhalifu hapa
nchini.
Hayo
yamesemwa na Kaimu Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Serikalini Bi Prisca
Ulomi wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es
salaam.
Akifafanua Bi Prisca amesema kuwa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia kwa kutambua umuhimu wa TEKINOHAMA wameamua kuandaa muswada wa Sheria za Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao (Cyber Laws).
Akieleza
zaidi Bi Prisca amesema kuwa Muswada wa sheria hizo ni pamoja na
Muswada wa Sheria ya Kulinda Taarifa Binafsi (The Personal Data
Protection Bill), Muswada wa Sheria ya Biashara ya Miamala ya
Kielektroniki (Electronic Transaction Bill), na Muswada wa Sheria ya
Kuzuia Uhalifu kwa njia ya Kompyuta na Mtandao (Computer and Cyber
Crimes Bills).
“Sheria hizo zitasaidia kuimarisha matumizi ya
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano hapa nchini kwa kudhibiti uhalifu
kwa kutumia mitandao na kuwalinda watoto dhidi ya matumizi yasiyofaa ya
mitandao”. alisema Bi Prisca.
Bi Prisca aliongeza kuwa serikali
imetumia gharama kubwa kuweka miundombinu ya TEHAMA ambayo imesaidia
kuboresha na kuharakisha utoaji wa huduma mbalimbali na kubainisha kuwa
wapo baadhi ya watu wanatumia vibaya teknolojia hiyo, hivyo kuna umuhimu
wa kuwepo sheria zitakazodhibiti uhalifu kupitia mitandao.
Wizara
ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia imetoa rai kwa wananchi
kujiepusha na matumizi mabaya ya mitandao na badala yake watumie vizuri
mitandao hiyo kwa maendeleo yao na taifa kwa ujumla hali inayoweza
kuathiri ukuaji wa sekta hiyo nchini.
Tuesday, April 1, 2014
Popular Posts
-
Apple wametoa Sasisho la Program Endeshi ya iOS 12.2 kwa ajili ya iPhone, iPad, and iPod toleo ambalo litawezesha wenye vifaa vya hivy...
-
Kuna Utapeli umeanza kusambaa saa chache zilizopita kupitia CRDB INTERNET BANKING . Anayefanya utapeli huu ametengeneza majina band...
-
Mamlaka ya mawasiliano nchini ,TCRA, imewaonya wale wote wanaotumia mitando kuchafua na kudhalilisha watu waache mara moja vinginev...
-
Mtandao wa Facebook umelaumiwa kwa kuwafanyia wateja wake utafiti wa kisaikolojia bila ya kuwajulisha. Nia...
-
Picha na Salim Kikeke Kuanzia sasa kudanganya kwamba mtu hakupata ujumbe wako wa WhatsApp itakuwa historia, au kud...
-
Mmoja wa wafanyakazi wa Digital Brain Bi.Edith akifafanua jambo kuhusu kampuni hiyo ambayo imeanzisha program ya usimamizi wa hospital na ...
-
1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa Kulikuwa na wakati ambapo bei ya vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ...
-
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA TAARIFA KWA UMMA Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ni chombo cha...
-
Mtaalamu wa masuala ya usalama kwenye Mtandao Yusuph Kileo akiwasilisha mada Itakumbukwa katika mkutano uliofanyika mapema mwezi h...
-
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imezindua mfumo mpya wa kuongoza vyombo vya usafiri majini utakaotumia kompyuta kwa lengo la kuv...