Serikali ya Tanzania ipo katika hatua ya mwisho za kuandaa sheria ya kukabiliana na uhalifu wa kimtandao ambapo kwa sasa inajiandaa kuwasilisha muswaada wa sheria hiyo kwenye baraza la Mawaziri.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Sayansi na Teknolojia wa Tanzania Profesa Makame Mbarawa wakati akizungumza kwenye baraza la wafanyakazi wa Wizara hiyo.
Profesa Mbarawa amesema kuwa sheria tatu zinatarajia kutengenezwa kupitia mpango huo wa kukabiliana na uhalifu wa mitandao zitagusa maeneo muhimu yatakayotumia mitandao hususani huduma za fedha kwa mtandao
Ameitaja mikakati mingine inayofanywa na serikali katika kuboresha sekta ya mawasiliano na teknolojia kuwa ni pamoja na uwekezaji utaogharimu kiasi cha fedha shilingi ishirini na uendelezaji wa ujenzi wa mkongo wa taifa wa mawasiliano.
Aidha amewataka watumishi wa Wizara hiyo kujadili namna ya kuboresha utendaji kwenye wizara bila ya kuwa na vitengo vingi akiwataka kuunganisha idara zitakazoshabihiana katika utendaji bila kutanguliza maslahi binafsi.
Popular Posts
-
Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imeingilia kati wizi wa fedha kwa kutumia mashine za kutolea fedha (ATM), ambao umeibua hofu kubwa katika s...
-
Itakumbukwa Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huu katika hotuba yangu niliyo iwasilisha kwa wanausalama mitandao tulipo kutana jijini Johan...
-
Upungufu wa usalama wa herufi za siri za takriban simu milioni 900 umewapa wadukuzi fursa ya kudhibiti simu za android kote duniani...
-
Wabunge wa Tanzania wameibana serikali wakiitaka iboreshe muswada wa sheria ya mifumo ya malipo ili kuzibana kampuni za simu na mabenki,kuto...