Serikali ya Tanzania ipo katika hatua ya mwisho za kuandaa sheria ya kukabiliana na uhalifu wa kimtandao ambapo kwa sasa inajiandaa kuwasilisha muswaada wa sheria hiyo kwenye baraza la Mawaziri.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Sayansi na Teknolojia wa Tanzania Profesa Makame Mbarawa wakati akizungumza kwenye baraza la wafanyakazi wa Wizara hiyo.
Profesa Mbarawa amesema kuwa sheria tatu zinatarajia kutengenezwa kupitia mpango huo wa kukabiliana na uhalifu wa mitandao zitagusa maeneo muhimu yatakayotumia mitandao hususani huduma za fedha kwa mtandao
Ameitaja mikakati mingine inayofanywa na serikali katika kuboresha sekta ya mawasiliano na teknolojia kuwa ni pamoja na uwekezaji utaogharimu kiasi cha fedha shilingi ishirini na uendelezaji wa ujenzi wa mkongo wa taifa wa mawasiliano.
Aidha amewataka watumishi wa Wizara hiyo kujadili namna ya kuboresha utendaji kwenye wizara bila ya kuwa na vitengo vingi akiwataka kuunganisha idara zitakazoshabihiana katika utendaji bila kutanguliza maslahi binafsi.
Popular Posts
-
Mamlaka ya Mawasilino Tanzania, TCRA, imesema watumiaji wa namba za simu ambazo hazikusajiliwa, watakatiwa mawasiliano ifikapo Juni M...
-
Polisi kanda maalumu ya Dar es salaam wamezungumzia utapeli unaofanywa kwa kutumia simu za mkononi na kusema wengi wanaofanya hivyo husajili...
-
Google I/O ni kongamano linalofanyika kila mwaka California kwa kuwakutanisha Developers wa bidhaa za Google kama Android , Chrome , Chrom...
-
Afisa wa Taasisi ya uwezeshaji na ujengaji uwezo kwa wateknohama nchini KINU, Catherinerose Barretto akimkabidhi cheti Ally Said toka P...
-
Picha na Salim Kikeke Kuanzia sasa kudanganya kwamba mtu hakupata ujumbe wako wa WhatsApp itakuwa historia, au kud...
-
Microsoft is switching off its Windows Live Messenger service on 15 March. On that date Messenger log-ins will no longer work a...
-
Mwezeshaji wa kipindi cha Maisha na Teknohama cha Morning Star Radio,Johnson Mziray akichangia jambo kwenye warsha hiyo,pembeni yake mweny...
-
Idadi ya watu wanaotumia huduma ya mtandao wa Intaneti nchini Tanzania imeongezeka kutoka watu 26,000 mwaka 2000 hadi kufikia watu mili...
-
Masomo kwa njia ya mtandao(Online Studies) kwa miaka ya hivi karibuni yamekuwa yakitolewa bure na baadhi ya Vyuo Duniani. Mfano katika...