Serikali ya Tanzania ipo katika hatua ya mwisho za kuandaa sheria ya kukabiliana na uhalifu wa kimtandao ambapo kwa sasa inajiandaa kuwasilisha muswaada wa sheria hiyo kwenye baraza la Mawaziri.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Sayansi na Teknolojia wa Tanzania Profesa Makame Mbarawa wakati akizungumza kwenye baraza la wafanyakazi wa Wizara hiyo.
Profesa Mbarawa amesema kuwa sheria tatu zinatarajia kutengenezwa kupitia mpango huo wa kukabiliana na uhalifu wa mitandao zitagusa maeneo muhimu yatakayotumia mitandao hususani huduma za fedha kwa mtandao
Ameitaja mikakati mingine inayofanywa na serikali katika kuboresha sekta ya mawasiliano na teknolojia kuwa ni pamoja na uwekezaji utaogharimu kiasi cha fedha shilingi ishirini na uendelezaji wa ujenzi wa mkongo wa taifa wa mawasiliano.
Aidha amewataka watumishi wa Wizara hiyo kujadili namna ya kuboresha utendaji kwenye wizara bila ya kuwa na vitengo vingi akiwataka kuunganisha idara zitakazoshabihiana katika utendaji bila kutanguliza maslahi binafsi.
Popular Posts
-
Katika ukurasa wake wa twitter Mhe Zitto Kabwe ametweet "Asanteni sana Wauza Mawese # TeamMawese leo kwenye uzinduzi wetu Kigoma Mj...
-
Wataalamu kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakitoa elimu jinsi ya kut...
-
Wanasayansi wa maabara ya Bristol Robotics Uingereza wamegundua njia ya kutumia mkojo kama chanzo cha kuzalisha umeme wa kuchaji bet...
-
Maelfu ya tarakirishi (kompyuta) za mitandao ya mashirika makubwa kadhaa duniani yamedukuliwa na kutekwa na watekaji wanadai malipo ...
-
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litaanza kutumia tiketi za elektroniki kwenye uwanja wa Azam uliopo Chamazi,Dar es salaam w...
-
Mwaka 2014 Umekua wenye changamoto nyingi sana kwenye upande wa mitandao ambapo wahalifu mtandao walifanikiwa kwa kiasi kikubwa san...
-
Afrika ni Bara la pili kwa kuwa na idadi kubwa ya watu ambapo inafikia takribani bilioni 1.2 (wengi wao wakiishi mijini) na inatarajiwa kon...
-
Maafisa wa utawala katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, wamebana matumizi ya ujumbe mfupi wa simu za mkononi baada ya kusema kuwa ni t...
-
Shirika la kujiolea la nchini Marekani linalojihusisha na utabibu na masuala ya haki za binadamu (PHR) limetengeneza program tumishi mp...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kuanzia sasa itakamata mtu yoyote anayesajili laini za simu kwa kuchakachua au bila kuf...