Serikali ya Tanzania ipo katika hatua ya mwisho za kuandaa sheria ya kukabiliana na uhalifu wa kimtandao ambapo kwa sasa inajiandaa kuwasilisha muswaada wa sheria hiyo kwenye baraza la Mawaziri.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Sayansi na Teknolojia wa Tanzania Profesa Makame Mbarawa wakati akizungumza kwenye baraza la wafanyakazi wa Wizara hiyo.
Profesa Mbarawa amesema kuwa sheria tatu zinatarajia kutengenezwa kupitia mpango huo wa kukabiliana na uhalifu wa mitandao zitagusa maeneo muhimu yatakayotumia mitandao hususani huduma za fedha kwa mtandao
Ameitaja mikakati mingine inayofanywa na serikali katika kuboresha sekta ya mawasiliano na teknolojia kuwa ni pamoja na uwekezaji utaogharimu kiasi cha fedha shilingi ishirini na uendelezaji wa ujenzi wa mkongo wa taifa wa mawasiliano.
Aidha amewataka watumishi wa Wizara hiyo kujadili namna ya kuboresha utendaji kwenye wizara bila ya kuwa na vitengo vingi akiwataka kuunganisha idara zitakazoshabihiana katika utendaji bila kutanguliza maslahi binafsi.
Popular Posts
-
Apple wametoa Sasisho la Program Endeshi ya iOS 12.2 kwa ajili ya iPhone, iPad, and iPod toleo ambalo litawezesha wenye vifaa vya hivy...
-
Kitabu hiki kipo tayari. Wasiliana kwa namba 0713 309 314 au 0763 309 314 na Mushi Richard, Mpesa: 0755872462, Tigopesa: 0713643703 ...
-
Katika wiki chache zilizopita kulikuwa na msuguano kati ya serikali ya Marekani na China , Serikali ya Marekani inailaumu china kwa kufany...
-
Mamlaka ya mawasiliano nchini ,TCRA, imewaonya wale wote wanaotumia mitando kuchafua na kudhalilisha watu waache mara moja vinginev...
-
Mtandao wa Facebook umelaumiwa kwa kuwafanyia wateja wake utafiti wa kisaikolojia bila ya kuwajulisha. Nia...
-
Picha na Salim Kikeke Kuanzia sasa kudanganya kwamba mtu hakupata ujumbe wako wa WhatsApp itakuwa historia, au kud...
-
Bwana. Keriako Tobiko Mkurugenzi wa Mashtaka ya umma ya nchini Kenya Bwana. Keriako Tobiko ametangaza kuanzishwa kwa kitengo maalum...
-
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA TAARIFA KWA UMMA Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ni chombo cha...
-
Mtaalamu wa masuala ya usalama kwenye Mtandao Yusuph Kileo akiwasilisha mada Itakumbukwa katika mkutano uliofanyika mapema mwezi h...
-
Kuna Utapeli umeanza kusambaa saa chache zilizopita kupitia CRDB INTERNET BANKING . Anayefanya utapeli huu ametengeneza majina band...