Saturday, May 9, 2015

WAADVENTISTA WA SABATO NCHINI TANZANIA WATAKIWA KUTUMIA TEKNOLOJIA YA HABARI NA MAWASILIANO

Gideon Msambwa akihutubia kanisani Kirumba,Mwanza

Waumini wakimsikiliza Gideon Msambwa

Mkurugenzi wa mawasiliano wa Unioni Konferensi ya Kaskazini  mwa Tanzania ya Kanisa la Waadventista Wa Sabato Gideon Msambwa ametoa ushauri kwa washiriki kutumia teknolojia ya habari na mawasilino ili kuleta maendeleo ya kanisa hilo nchini.

Akizungumza jana  Mei 9 mwaka huu jijini Mwanza katika Kanisa la Waadventista wa Sabato Kirumba,Msambwa amesema Mataifa ya Asia na Kusini mwa Bara la Amerika yamepiga hatua kubwa katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano,hadi kufikia hatua ya kumiliki viwanda.

Akitoa mfano, amesema Kanisa la Waadventista wa Sabato Korea Kusini linamiliki viwanda vidogo 104,000 wakati Tanzania bado kanisa hili linamiliki kiwanda kimoja cha Uchapaji kilichopo mjini Morogoro.


Amesema pia kwamba, Korea Kusini kuna vyuo vikuu vitano vya Kimataifa,wakati hapa nchini Waadventista wa Sabato wanamiliki Chuo kikuu kimoja,University of Arusha.


Korea Kusini kanisa hili humikili kiwanda bora cha uchapaji,wakati nchini Brazil kanisa hili washiriki wake wamepiga hatua kubwa katika medani ya elimu na teknolojia.


Mkuu huyu wa Mawasiliano katika Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania,amesema asilimia 60 ya wabunge Brazil ni Waadventista wa Sabato,huku washiriki wa kanisa wameunganishwa katika Mfumo wa kiteknolojia wa kutunza kumbukumbu uitwao,Adventist Church Manegement System(ACMS),ambamo kumbukumbu zote za washiriki na wachungaji hutunzwa.


Kufuatia hali hiyo,Tanzania na Ghana zimechaguliwa na Konferensi Kuu(GC) kuandaa mfumo huu wa kutunza kumbukumbu.


Hadi sasa, Union 38 hapa duniani za kanisa hilo kumbukumbu zake zimehifadhiwa katika Mfumo huu wa ACMS.Jumla ya washiriki waliobatizwa wa Kanisa 7,500,313 kumbukumbu zao zinahifadhiwa katika mfumo huu duniani,miongoni mwa hawa 1,679 ni wa makanisa 1,735 ya Unioni ya Kaskazini mwa Tanzania.


Unioni ya Kaskazini mwa Tanzania(NTUC) ina jumla ya washiriki waliobatizwa 354,456 wakati washiriki wengi kumbukumbu zao zikiwa hazijaingizwa katika mfumo huu mahsus wa kumbukumbu.


Kufuatia hali hiyo,Idara ya Mawasiliano ya Unioni hii imewataka wachungaji na washiriki kuhakikisha kuanzia sasa hadi Disemba 2016 asilimia 50 ya kumbukumbu zote za washiriki ziwe zimeingizwa katika mfumo huu.


PROGRAM TUMISHI YA M-PESA YAWA MIONGONI MWA PROGRAM TUMISHI ZINAZOWAWEKA MAMILIONI YA WATU MTANDAONI KWA KUTUMIA SIMU

 Five Mobile Apps Bringing The Next Billion People Online

 Mwaka  2013, Mwenyekiti Mtendaji wa Google Eric Schmidt alikisia kuwa duniani kote watu watakuwa kwenye mtandao mwishoni mwa karne.

Kuna progam tumishi nyingi ambazo zimetengezwa na zinatengezwa zikijaribu kuwaweka watu karibu kwenye mitandao .
Ripoti iliyolewa hivi karibuni inaonesha kuwa kuna baadhi ya program tumishi ambazo zitasaidia kwa kiwango kikubwa kuwaweka mtandaoni mamilioni ya watu duniani  miongoni mwa program hizo maalufu ambazo zinaonekana kuongoza kupitia simu za mikononi ni;

1. M-Pesa
Hii ni Program tumishi kwa ajili ya malipo kupitia simu za mkononi ambayo inatumika barani Afrika huduma iliyoanzishwa mwaka 2007 na kampuni ya Safaricom ya nchini Kenya iliyomiongoni mwa makampuni ya  Vodafone,Mtumiaji anaweza tuma ama kupokea fedha kupitia ujumbe mfupi wa maneno,kulipa bili na kununua muda wa maongezi.Katika maeneo ambapo watu wanapata huduma chache za kibenki ama hakuna huduma hizo M-Pesa imekuwa ikipata umaarufu ambapo kwa sasa inaonesha kufikisha kiasi cha watumiaji milioni 18 wa huduma hiyo.


2. SoukTel
Ikiwa inatumika Mashariki ya Mbali, SoukTel ina program tumishi mbalimbali zinazowasaidia watu kupata taarifa kuhusu kazi na huduma za kijamii.Inajuikana hasa kwa kuhusianisha katika kutafuta kazi na inawaunganisha watu mbalimbali kupitia ujumbe mfupi wa maneno toka Jordan,Rwanda,Tunisia na nchi mbalimbali.Hivi karibuni SoukTel iliungana na Facebook na kuanzisha huduma ya elimu ya uchumi nchini Colombia.


3. Esoko
Mara nyingi huelezwa kuwa ni Facebook kwa ajili ya wakulima Esoko inawaunganisha wakulima na mashirika yasiyo ya kiserikali,makampuni ya biashara na wakala wa serikali .Soko ni neno la kiswahili linalotokana na sokoni na E ikisimama badala ya vifaa vya umeme.

Utumaji wa ujumbe mfupi wa maneno kwa kuhusianisha tovuti ambapo hutuma taarifa kuhusu hali ya hewa,taarifa za bei na matangazo.

4. Frogtek
Kwa kutumia program za simu za kisasa na tabiti, Frogtek inasaidia wafanya biashara wadogo hasa katika familia ndogo maarufu  mom-and-pop katika nchi za bara za Amerika ya Kusini na baadhi ya nchi zinazoendelea ambapo huwawezesha wafanyabiashara hao kufahamu bidhaa walizonazo na mauzo yaliyofanyika 


5. Ver Se’ Innovation
Imetengenezwa huko Bangalore, India,ni program tumishi ambayo ni maalum kwa taarifa na huduma za ndani ya India ambayo husaidia kutoa taarifa za kazi,umiliki wa vitu mbalimbali na matangazo ya masoko huku ikiwa na huduma ya malipo na manunuzi kwa njia ya mtandao.




SERIKALI YA TANZANIA YAWATAKA WANANCHI KUTOA MAONI YA KUBORESHA SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO 2015


 

Serikali ya Tanzania imewataka wananchi kutoa maoni yatakayoiboresha sheria ya makosa ya mitandao ya mwaka 2015 iliyosainiwa hivi karibuni na Rais Jakaya Kikwete ili yasaidie kuiboresha.
Imesema licha ya sheria hiyo kusainiwa na Rais, bado kuna umuhimu wa kuiboresha katika baadhi ya vipengele vyenye upungufu.

Kauli hiyo imetolewa Mei 8 mwaka huu jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa (Pichani) katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika ofisini kwake.

Mkutano huo uliandaliwa maalumu kwa ajili ya kuufahamisha umma kuhusu kusainiwa kwa sheria hiyo na rais wa Tanzania na kuelezea umuhimu wake, huku pia waziri huyo akiitumia fursa hiyo kukaribisha maoni ya wadau mbalimbali kwa ajili ya kuiboresha.


“Tunaomba wananchi tuipokee sheria hii kwa sababu ni nzuri na itasaidia sana kuwalinda, lakini pia kama kuna kifungu chochote ambacho kitaonekana kuwa na upungufu leteni ushauri au maoni wizarani, tutayatafakari na tutayafanyia kazi,” alisema Mbarawa.

Waziri Mbarawa amesema Tanzania si nchi ya kwanza kupitisha sheria ya aina hiyo kwa sababu ya uwepo wa maendeleo ya teknolojia ya mawasiliano kulikosababisha kuongezeka kwa uhalifu wa mitandao.


  Profesa Mbarawa amesema nchi za Uingereza, India, Malaysia, Uganda, Korea Kusini, Singapore, Mauritius, Afrika Kusini, Marekani na nyinginezo tayari zina sheria ya aina hii na inasaidia kuwapa wananchi haki wanapofanyiwa uhalifu wa mitandaoni.

Sheria ya Makosa ya Mitandao mwaka 2015 ni moja ya sheria zinazokosolewa  na wadau wa habari pamoja na makundi mbalimbali ya kijamii, kwa madai kuwa inalenga kubana uhuru wa vyombo vya habari pamoja na kubinya uwanja mpana wa ukusanyaji na utoaji habari kwa waandishi wa habari.

Saturday, May 2, 2015

TAHADHARI KWA WANAOANGALIA TOVUTI ZA PICHA ZA NGONO KATIKA SIMU ZAO


Watafiti toka kampuni ya utafiti ya  Zscalar  wamegundua kuwa,tovuti za kichina zenye picha za ngono zimekuwa zikisambaza virusi ambavyo vinasababisha simu za mikononi kushambuliwa na virusi vya komputa viitwavyo malware.
Utakapotembelea tovuti hizo na ukajaribu kuangalia video,tovuti itakuomba upakue sehemu ya program ya komputa ambayo kiuhalisia ni kirusi kiingine kiitwacho trojan.

Kirusi hicho cha Trojan kinajishajilisha chenyewe kwenye simu yako na kuifanya simu yako kuwa na uwezo wa kupokea matangazo yanayohusisha  ujumbe mfupi wa maneno (sms) ulioko kwenye simu yako.Jambo ambalo litasaidia wahalifu wa mtandao kudukua taarifa zako za kibenki kwenye simu iliyo na kirusi hicho kiurahisi.


MWANAFUNZI AFUNGWA JELA MIAKA MINNE KWA KOSA LA KUDUKUA KOMPUTA ZA CHUO KIKUU



Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 25 ambaye alidukua komputa za Chuo Kikuu cha Birmingham na kuongeza alama za mtihani amefungwa jela miaka 4.

Imran Uddin, ambaye alikuwa anasoma mwaka wa mwisho fani ya sayansi katika chuo hicho aliongeza alama za mtihani toka asilimia 57 hadi 73 kwa kuiba neno la siri la mfanyakazi kwa kutumia keybord inayodukua yenye uwezo kudukua komputa aliyoinunua baada ya kuitafuta kupitia mtandao wa ebay.



Kwa mujibu wa mahakama inaelezwa kuwa Uddin alipachika nyuma ya komputa  kifaa kinachoweza kuingia kwenye program ya komputa bila mhusika kutambua.



Tukio hilo lilitokea Oktoba 7 mwaka jana ambapo kifaa hicho kilikuwa kikichukua taarifa ya kila kilichofanywa na mtumiaji wa komputa hiyo  na baadaye ilionekana vifaa kama hivyo vilikuwa vimewekwa katika komputa tofautikati chuoni hapo.

Friday, May 1, 2015

MFUMO WA UNUNUZI WA UMEME KUPITIA SIMU ZA MIKONONI WAVUNJWA

Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es salaam wakiwa wamepanga foleni ili kununua umeme jana

Huduma ya manunuzi ya umeme kwa njia ya miamala ya simu za mkononi nchini Tanzania imeanza kuwa kero kuanzia jana Aprili 30 mwaka huu baada ya kile kinachoelezwa kuwa ni kuvunjika kwa mkataba kati ya Shirika la Umeme Tanzania-Tanesco na mmoja wa watoa huduma hiyo ya ununuzi wa umeme yaani kampuni ya Selcom ambapo mteja hupatiwa namba ambazo huziingiza kwenye mita ya luku.

Katika mfumo huo mteja hununua umeme kupitia simu ya mkononi kupitia Mpesa, Tigo Pesa na Airtel jambo ambalo kuanzia jana haliwezekani kwa sasa ambapo kampuni ya Tigo ilianza kuwatumia ujumbe wateja wake kuwa imesitisha huduma hiyo kutokana na matatizo na wakala.

Hali ilivyokuwa:
  • Manunuzi yote ya luku yalikuwa yakifanyika kupitia mitambo ya makampuni mawili, Maxcom na Selcom.
  • Makampuni haya ndiyo yanayowapa wengine kama vile mitandao ya simu na mabenki uwezo wa kununua na kulipia huduma ya umeme -Luku
  • Hivyo mara nyingi pale ulipokuwa unapata shida kununua umeme inakuwa pale ambapo mfumo wa malipo unaotegemea mitambo ya moja ya hizi kampuni mbili unakuwa na hitilafu.
Tanesco kupitia amri ya WAZIRI wa Nishati na Madini, George Simbachawene,  na ushauri wa TRA wamevunja mkataba wa uwakala na Kampuni ya Selcom. Sababu kubwa zilizotolewa ni kutokana na mitambo yake ya kuuza umeme kwa njia hii kuwa na matatizo ikiwemo matatizo ya kisheria katika kulipa kodi.

Inasemekana kero nyingi za ukosekaji wa huduma ya manunuzi ya umeme wa LUKU ambayo imekuwa ikitokea hivi karibuni imekuwa ni kutokana na mitambo ya kampuni hii kusumbua.

Kwa kuwa kabla ya hili kutokea makampuni ya simu na baadhi ya mabenki yalikuwa yanatoa huduma hiyo ya ununuaji wa umeme kupitia mitambo ya Selcom kwa sasa utaendelea kukosa huduma hiyo.

Kwa sasa wanunuzi wa umeme kwa njia ya luku wataendelea kupata huduma hiyo kupitia vituo vya mauzo ya Luku vya Tanesco au sehemu inayouza umeme kupitia huduma ya MaxMalipo.

 credit:www.teknokona.com





Tuesday, April 21, 2015

PROGRAM TUMISHI ZA SIMU ZINAZOWAWEKA KARIBU WANANDOA






 http://wp.production.patheos.com/blogs/danpeterson/files/2014/10/black-couple-hugging.jpg
Mabadiliko ya teknolojia ya mawasiliano yanayotokea duniani yamekuwa yakileta athali chanya na hasi ndani ya jamii hasa katika maswala ya mawasiliano.
Wavumbuzi na wataalamu wa program tumishi duniani nao hawako nyuma katika kubuni programu ambazo zitawafanya wachumba ama wanandoa wanaotumia simu za kisasa na tabiti kuwa karibu zaidi katika masuala ya mawasiliano.
Kwa sasa kuna program tumishi nyingi ambazo ni maalum wa wapenzi ama wanandoa japo kuwa kuna zile ambazo zinaleta tija zaidi ya nyinginezo.
Couple
Kanuni iliyoko katika program tumishi ya Couple ni kwamba inawawezesha watu wawili kuwa na wigo wa mawasilino ya mahusiano yenye  faragha kwa kubadilishana picha,video,ama ujumbe wa sauti
Hii ni program tumishi ina huduma ya kutuma ujumbe wa papo kwa papo kama ilivyo katika mtandao wa kijamii wa WhatsApp,picha inaweza kutumwa ikiwa imewekwa katika mpangilio wa kutoweka baada ya muda fulani pia ina huduma ya kukupatia taarifa ya mahali pa faragha  ambapo mnaweza kwenda kwa ajili ya chakula ama maongezi ya wachumba ama wanandoa,ikiambatanisha na kalenda.
Mpaka sasa inatumiwa na wanandoa zaidi ya milioni mbili duniani ni moja ya program tumishi ambayo inaonekana kuwafaa wanandoa katika mawasiliano binafsi ya faragha.

Couple Tracker

Imekuwa ni jambo la kuumiza kwa baadhi ya watu walioko kwenye mahusiano.Jambo hili limekuwa likileta lawama na kushutumiana katika suala kukosa uaminifu.

Couple Tracker ni program tumishi iliyokusudia kutatua tatizo la watu kutokuwa waaminifu  kwenye mahusiano na imekusudia kuwa na mkakati wa kusaidia kuboresha uaminishi kwenye mahusiano ya wachumba ama wenzi wa maisha.

Kinachofanywa na program hii tumishi ni kumwezesha mwanandoa kuona simu zilizopigwa,kupokelewa,ujumbe mfupi wa maneno,anachofanya mwanandoa mwenzake kwenye mitandao ya kijamii ya  Whatsapp, Facebook  na uwezo kutambua mahali simu ya mwanandoa ama mchumba mwenzako ilipo,japo kuwa ina sehemu fulani ya faragha hata hivyo mawasiliano yote ya masaa 24 katika siku saba yanaweza kuoneshwa kwa kupitia program hii.

Hata hivyo ni lazima uhakikishe kuwa kuna makubaliano rasmi ya wahusika wawili  kuitumia kwa sababu ya sheria zinazozuia udukuzi wa mawasiliano.

Our Groceries


Watalaamu wa mahusiano wanaeleza kuwa maisha ya ndoa baada ya fungate huwa yanachangamoto zake hasa katika masuala ya kipato katika matumizi mbalimbali ya fedha za kujikimu kwa wanandoa.
Kila mmoja analojukumu la kuhakikisha masuala ya manunuzi ama gharama za matumizi ya nyumbani mfano malipo ya umeme,maji ,malipo na manunuzi ya vifaa mbalimbali vya familia.
Our Groceries ni program tumishi ambayo inajaribu kutoa suruhisho la kutatua upangaji wa bajeti kwa wanandoa  na hivyo kuepusha manunuzi ambayo unaweza yafanya wakati ambapo mwenzi wako ameshayafanya kwa kuwa inakupa taarifa ya kile mwenzako alicho kinunua kabla.
Kwa kutumia progam hii unaweza kutayarisha orodha ya mahitaji unayopanga kununua ama kuyafanyia malipo na ukamshirikisha mwenzi wako kuona orodha hiyo  na utakapofanya malipo ama kununua chochote basi itatuma taarifa kwa kifaa cha mawasiliano cha mwenzi wako na kama unahitaji kutoa taarifa  anunue bidhaa yoyote unaweza fanya hivyo pia.

Avocado

Kama ilivyo program tumishi ya Couple, Avocado inawezesha kuwapatia wanandoa mawasiliano ya faragha na kuwaunganisha katika mawasiliano muda wote.
Unaweza kumtumia mwenzi wako ujumbe mfupi wa maneno,video,sauti na imewekewa kalenda ambayo hukumubusha matukio muhimu ya kuyakumbuka ikiwemo siku ya kuzaliwa,siku ya kufunga ndoa na mambo mengine muhimu kwa wanandoa.

Kwa wale waliona mahusiano yanayotenganishwa na umbali inasaidia kukufanya uhisi kuwa karibu na umpendaye,pia inawezesha kutoa taarifa kwa mwenzi kuwa karibu betri ya kifaa cha mawasiliano itazima,programu hii pia inamwezesha mtumiaji kuona ujumbe,picha na taarifa zingine hata kama haujaunganishwa na upande mwingine wa mwenzi wako.
Inawezesha pia kuficha taarifa za mtumiaji ili mtu mwingine asizione ama kuzipata.

Hizi ni baadhi tu ya program tumishi nyingi ambazo zinaweza kusaidia kuwaweka karibu zaidi wanandoa na kuboresha mahusiano yao siku baada ya siku ..



Friday, April 17, 2015

WAHALIFU WATENGENEZA KIRUSI KINACHOWEZA KUDUKUA SIMU YA MKONONI IKIWA IMEZIMWA



 Malware That Can Spy On Your ‘Powered Down’ Phone

Watu wengi wameshaona filamu ambazo wahalifu  wakidukua simu  za mikononi hata kama zimezimwa.

Kama ilivyozoeleka kuwa watu wengi hufikiri mambo hayo ni ya kufikirika.

Hata hivyo hivi karibuni kampuni ya AVG inayojihusisha na masuala ya usalama katika simu za mikononi na imegundua virusi aina ya  malware kilichopewa jina la ‘PowerOffHijack,’ambavyo vinauwezo wa kuingilia mfumo wa kuzima simu na kuifanya simu ya mkononi iendelee kupatikana japo imezimwa..

Kirusi huyo mara ya kwanza ameonekana nchini China na kusambaa katika program tumishi za uchina na simu nyingi zimeshambuliwa na kirusi huyo hasa zilizotengenezwa kwa program endeshi za Android zenye zaidi ya toleo namba 5

Kirusi hicho kikiingia kwa simu ya mkononi simu itatoa ujumbe kuwa imezimwa na malware itawe kupiga simu,kupiga picha na kufanya mambo mbalimbali bila mwenye simu kutambua.

Wednesday, April 8, 2015

UTAFITI:SIMU ZINACHANGIA UMASKINI NA MIGOGORO KATIKA MAHUSIANO


 
Wataalamu wa Saikolojia kutoka Chuo Kikuu cha Pennsylvania na Chuo Kikuu cha Vijana cha Bringman nchini Marekani wamebaini kuwa matumizi ya simu ni chanzo cha kutofurahia maisha na kuongeza msongo.
Utafiti uliofanywa na wataalamu hao chini ya usimamizi wa Brandon McDaniel,Mkufunzi kutoka Chuo Kikuu cha Pennsylvania,ulibainisha kuwa watu wengi wanaongeza umaskini wa kujitakia kwa kutumia muda mwingi kwenye simu.
Wanazungumzia maisha ya watu,mafanikio yao,kushindwa kwao badala ya kuangalia vitu vitakavyowaingia fedha zaidi,inaeleza sehemu ya utafiti huo.
Utafiti huo ulibainisha kuwa mbali na umaskini wa kujitakia,matumizi ya simu kupita kiasi huchangia kwa asilimia 75 ndoa kuvunjika pia hatari ya kupata msongo wa mawazo.
Utafiti huo uliohusisha watu wazima 867 wenye umri wa miaka 30 hadi 45,ulibainisha kuwa kama wasingekuwa na simu,robo tatu ya watu hao wangekuwa wamefanya mambo mengi kuboresha maisha yao ikiwemo utendaji bora wa kazi.
Majibu ya utafiti huo yalionesha kuwa wanandoa wengi wangepata muda wa kujadili namna ya kumaliza tofauti zao,kufikia mafaniki,kutimiza malengo hata kuboresha penzi kama wasingetumia simu.
Takwimu za Mamlaka ya Mawasiliano nchini Tanzania (TCRA) zinaonesha kuwa mwaka 2014 kulikuwa na laini za simu za mkononi zipatazo 31,862,656,ikilinganishwa na laini 2,963,737 mwaka 2005,watumiaji wa intaneti wameongezeka hadi kufikia 11,000,000 Desemba mwaka 2014 kutoka 3,563 waliokuwepo mwaka 2008
Chanzo:Gazeti la Mwananchi

Thursday, April 2, 2015

DAR ES SALAAM:MATANGAZO YA TV YA ANALOJIA MWISHO JUNI 17,2015 NCHINI



Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) na Shirika la umoja wa mataifa la Mawasiliano ya simu ulimwenguni ITU kwa  pamoja wameridhia makubaliano ya kusitisha Mfumo wa utangazaji wa televisheni unaotumia teknolojia ya analojia  katika miundombinu ya minara ifikapo juni 17,2015 na kuanza kutumia mfumo wa utangazaji wa kidijitali pekee.


Akizungumza na waandishi wa habari  hii leo jijini Dar es salaam Meneja mawasiliano wa TCRA Innocent  Mungy  amesema  makubaliano hayo ya jumuiya za ushirikiano wanchi mbalimbali zimechukua hatua za pamoja kuhakikisha uhamaji kutoka mfumo wa utangazaji wa anolojia kwenda dijitali unafanikiwa.


Mungy amesema Tanzania imekuwa nchi ya kwanza kutekeleza maazimio ya nchi wanachama na uzimaji wa mitambo ya televisheni inayotumia teknolojia ya analojia  Tanzania Bara ilianza kufanyika desemba  31,2012 .

Amekuwa Mamlaka kwa kushirikiana na Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Wizara ya Habari Utamaduni na michezo na  wadau wengine itaendelea kutoa elimu kwa umma ili kuhamasisha uhamaji pamoja na kuwaelewesha watumiaji haki zao za msingi.  

KAMATI YAPENDEKEZA SERIKALI KUONGEZA ADHABU KWA WATAKAOTUMA TAARIFA ZA UONGO KWENYE MITANDAO

Kamati ya kudumu ya Bunge ya miundombinu imependekeza kwa serikali iongeze adhabu ya faini kutoka shilingi milioni tatu na kifungo kisichopungua miezi sita na kuwa faini ya shilingi milioni tano na kifungo kisichopungua miezi sita kwa wale wote watakaotuma katika mtandao taarifa za uongo.

Aidha kamati hiyo ilipendekeza katika adhabu kwa watu wanaonyanyasa wenzao kupitia mtandaoni adhabu yao iongezwe kutoka kifungo cha cha mwaka mmoja na kuwa kifungo cha miaka mitano.

Awali akiwasilisha maelezo ya muswada huo,Waziri wa Mawasilino,Sayansi na Teknolojia Profesa Makame Mbarawa alisema kutokana na kukua kwa matumizi ya teknolojia ya Habari na Mawasiliano kumesababisha kuwepo kwa changamoto mbalimbali ikiwemo kuibuka kwa makosa ya mtandao.

Alitaja makosa ya mtandao yaliyokithiri kwa sasa kuwa ni makosa dhidi ya faragha,usalamana upatikanaji wa taarifa za kompyuta na mifumo ya kompyuta,makosa yanayohusu maudhui,makosa dhidi ya mifumo ya kompyuta na makosa ya kawaida yanayofanywa kwa kutumia mitandao.

Profesa Mbarawa alisema kuwa takwimu kutoka jeshi la polisi zinaonesha kuwa makosa ya uhalifu wa mtandao yaliyoripotiwa na kuchunguzwa kati ya mwaka 2012 hadi Agosti mwaka jana ni 400.

Alisema katika kipindi cha mwaka 2000 hadi mwaka 2013,makosa ya uhalifu wa mitandao yalisababisha hasara ya zaidi ya shilingi bilioni 9.8 kwenye taasisi za fedha.
 


Popular Posts

Labels