Saturday, December 28, 2013

NAMNA YA KUWEKA ULINZI WA KUKIFUATILIA KIFAA CHAKO CHA MAWASILIANO CHA APPLE KILICHOPOTEA

Umepoteza  iPhone ama kifaa chochote cha mawasiliano cha  Apple iOS? Kabla yakutoa taarifa kwa vyombo vya usalama ama kufanya lolote unapaswa ufuate hatua za kiulinzi ambazo zimewekwa na Apple ili kukusaidia kufahamu iPhone, iPad na iPod iliyopotea.

 iPhone 5S iliyotoka mwaka huu imetengenezwa mfumo wa kiusalama wa utambuzi wa alama za vidole,inahitaji kidole cha mmiliki kufungua simu,mfumo huu unasaidia kuzuia mwizi kuifungua simu ili kuitumia,simu hiyo pamoja na vifaa vingine vya mawasiliano vya Apple vinapopotea waweza kufahamu vilipo kwa kufuata hatua zifuatazo

Hatua # 1 – Seti na uactivate “Find My iPhone” katika kifaa chako

Hatua hii inahitajika uifanye mara unaponunua kifaa chako iwe ni Iphone,Ipad n.k.
Hakikisha umepada ID yako ya Apple ambayo inahusiana na kitambulisho cha kifaa ulichokinunua,ID ambayo pia itakusaidia wakati wa matumizi katika iCloud na upakuaji wa program tumishi toka Apple.
Nenda Settings ==> iCloud ==> angalia kama “Find My App” iko ON


iphone_find_my_iphone


 ipad_find_my_iphone

Utakapoweka ON “Find My iPhone” kama kifaa chako kitaibwa ama kupotea kitakusaidia kukutafuta na kufahamu kilipo .

Hatua #2 – Jiunge na  iCloud.com kwa kutumia  Apple ID yako

Unaweza kukitafuta na kukipata kifaa chako kilipo kwa kutumia iCloud.com iwapo utakuwa umefanya setting ya kwanza ya hatua ya kwanza kwa kufungua tovuti hiyo kwenye komputa yako na kuingia kwa kutumia Apple ID ile uliyosajili kifaa chako.Inakubali katika komputa za Window na Mac


 sign_in_icloud

Hatua   #3 –Fungua “Find My iPhone” na chagua palipoandikwa Device to Track

Bofya kwenye alama ya  “Find My iPhone” katika ukurasa wa  iCloud.com


 icloud_find_my_iphone

Hatua # 4 – Tafuta eneo kilipo kifaa chako. Kama ni eneo la karibu na ulipokipoteza ama ni ofisini,nyumbani n.k bofya palipoandikwa "play sound to find"

Chagua picha ya miongoni mwa kifaa kilichopotea Iphone,iPad n.k mahali palipoandikwa  “My Devices”. Baada ya kuchagua hapo, itaonekana ramani ya mahali kifaa kilipo ama muda wa mwisho kifaa hicho kilipokuwa.
icloud_select_device

Hatua # 5 – Ruhusu “Lost Mode”. Subiri mlio wa simu na endelea kuifuatilia ilipo

Baada ya kuchagua  “Find My iPhone”  program tumishi kwenye  iCloud itakuonesha mwongozo mwingine wa hatua zifuatazo,
# Play Sound – Hapa kifaa kitaanza kitatoa mlio na kama umepoteza nyumbani,ofisini n.k utausikia mlio
# Lost Mode –Kama unauhakika kuwa umeisahau simu yako ya iphone mahali utakaoruhusu hatua hii itumike itakuomba uweke namba ya simu ambapo watu watakupata,ama unaweza kuweka sentensi ama kuacha vivyo hivyo na kubofya "Done" na ujumbe utatokea kwenye simu yako iliyopotea hata kama umeifunga na utasomeka "Hii Iphone imepotea tafadhari nipigie "Namba yako"
# Erase iPhone – Hatua ya mwisho.Kwa kutumia iCloud na Find My iPhone unaweza kufuta ama kuondoa taarifa zako katika kifaa chako kilichoibwa ambapo utaondoa email zako,program tumishi ulizoweka n.k Kumbuka hatua hizi zote zinahitaji upatikanaji wa intaneti




TFF KUANZA KUTUMIA TEKETI ZA ELEKTRONIKI

 
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litaanza kutumia tiketi za elektroniki kwenye uwanja wa Azam uliopo Chamazi,Dar es salaam wakati wa mechi za Ligi Kuu za Ashanti United na JKT Ruvu  zitakazopambana Januari Mosi 2014, kati moja ya mechi za kujaribio ya  matumizi ya mfumo huo nchini Tanzania.


Taarifa ya TFF kwa vyombo vya habari imeleza kuwa
Viingilio katika mechi hiyo itakayoanza saa 10 kamili jioni ni sh. 1,000 na sh. 2,000 ambapo tiketi zinapatikana kupitia M-Pesa na mawakala wa CRDB Fahari Huduma. Tiketi zitaendelea kuuzwa hadi kipindi cha kwanza cha mechi hiyo kitakapomalizika.


Mawakala 18 wa Fahari Huduma wanaouza tiketi hizo ni ABC Computer- Mtaa wa Samora, Abraham Anangisye Mwampetele- Maji Matitu, Apex Security Services- Mtaa wa Mibega, Kinyerezi, Athuman Fakhi Adam- Kongowe Mbagala, Fedha Investment Limited- Pamba Road na Fuya Godwin Kimbita- Tegeta Block.


Ghomme Health & Education Limited-Bahari Beach, Herman Arbogast Tarimo- Kigamboni, K- Finance Limited- Shekilango, Sinza, Koli Finance Limited- Mtaa wa Samora, LB Pharmacy- Mtoni Kijichi, Lista Phares Barnabas- Tabata Segerea na Maly Investment Company Limited- Mtaa wa Sikukuu, Kariakoo.


Wengine ni Micu Enterprises- Mtaa wa Congo, Kariakoo, S&D Collection Company Limited- Mikocheni, Shoppers Plaza, Therry Investment Limited- Tegeta Kibaoni, TSHS Distributors Limited- Mtoni kwa Aziz Ali na Wemerick Independent Vehicle- Mtaa wa Boko.


Pia mshabiki anaweza kununua tiketi kwa njia ya simu- mtandao wa Vodacom kwa kupiga *150*03*02# ambapo atapata namba atakayoitumia kufanya malipo kupitia MPESA. Katika MPESA namba ya malipo kwa TFF ambayo ndiyo mshabiki ataitumia kufanya malipo ya tiketi (business number) ni 888800. Vilevile mteja wa CRDB aliye katika mtandao anaweza kufanya malipo kupitia CRDB simbanking.


Baada ya kufanya maombi kupitia njia yoyote ya hizo tatu; MPESA, Fahari Huduma na CRDB simbanking, mshabiki atapata namba ambayo ataitumia ku-print tiketi yake kupitia mashine maalumu za kuchapia Tiketi ya TFF zilizo katika ATM za CRDB kwenye maeneo yafuatayo;


Benki ya CRDB tawi la Azikiwe, tawi la Holland House ambapo kuna mashine mbili, tawi la Vijana, tawi la Kariakoo, ATM ya Mtaa wa Shaurimoyo ambapo kuna mashine mbili na ATM ya CRDB iliyoko kituo cha mafuta cha Kobil Sabasaba, Mtoni kwa Aziz Ali.

HACKER NI NINI?

 
KAMA HAUKUJUA BASI JUA
Na MBUKE TIMES
Neno HACKER makusudio yake haswa sio kumaanisha mtu anayefanya vitendo vya kihalifu kwa kutumia kompyuta, yaani kama vile kuiba password za watu, kusoma emails za watu n.k. Bali neno HACKER kiasili lina maana ya mtu mwenye uwezo wa kipekee wa kutafuta suluhu ya tatizo kwa haraka, kwa mbinu za ubunifu ambazo pengine si mbinu rasmi, ila zinaleta suluhu ya haraka.

--Hata hivyo kwakuwa HACKER ana ujuzi wa hali ya juu wa matumizi ya kompyuta na ni mtundu, basi wapo Hackers walioamua kutumia ujuzi huo kufanya uhalifu, na ndipo jina lilipoharibika.

--Hata hivyo jamii ya hackers na wanateknolojia wengi wameendelea kuelimisha matumizi sahihi ya jina HACKER na neno HACKING. Mifano ya wazi ni :-
1. Facebook: Kuta za ofisi za FB zimeandikwa neno HACK. Kusisitiza umuhimu wa kuandika codes kwa haraka na kutafuta kwa ubunifu na kwa haraka suluhu ya matatizo.
Hata mfumo mzima wa uendeshaji wa FB umepewa jina THE HACKER WAY.

2. Makampuni mengi yamekuwa yakiandaa mikutano ya siku moja au zaidi kwa ajili ya kukutanisha HACKERS ili kubuni bidhaa na kutatua matatizo mbalimbali. Mikutano hiyo huitwa HACKATHONS
-- Kwa maelezo zaidi search Google maneno HACKER, FACEBOOK THE HACK WAY na HACKATHONS.

UTAFITI:FACEBOOK YAKIMBIWA NA VIJANA HUKO UINGEREZA




Utafiti unaonesha kuwa Vijana kati ya miaka 16-18 nchini Uingereza wanaonekana kutovutiwa na mtandao wa kijamii wa facebook  kutokana na kukerwa na mtandao huo. 

Tovuti ya yahoo imesema kuwa Vijana hao sasa wameonekana kuvutiwa  Zaidi na mitadao ya kijamii mingine ambayo ni  Twitter, Instagram, Snapchat  na WhatsApp.

Profesa Daniel Miller kutoka Chuo Kikuu cha London ambaye alisaidia kufanya utafiti kuhusu jambo hilo amesema wakati ambapo wazazi wamekuwa na wasiwasi kuhusu watoto wao kujiunga na face book lakini watoto wanaeleza kuwa ni familia zao ndizo zinazosisitiza wawepo kwenye mtandao huo kwa ajili ya mawasiliano.

Utafiti huo ulifadhiliwa na umoja wa ulaya na kuwahusisha vijana wenye umri wa miaka 16-18 umeonesha kuwa mitandao mingine ya kijamii na program tumishi zinaonekana si bora katika miongozo ya namna ya  kuitumika  kuliko facebook.

Utafiti huo unaonesha kuwa Facebook inawaunganisha watumiaji vyema,inatoa mpangilio mzuri wa picha na mpangilio wa mahusiano miongoni mwa watumiaji.

 WhatsApp inaonekana ni bora kwa ujumbe wa maandishi ambapo kwa sasa inaonekana kuipiku facebook na kutokana na kuonekana bora katika huduma ya ujumbe mfupi wa maneno . 

Miongoni mwa vijana wengi nchini Uingereza  sasa wanatumia  Snapchat,ambao hukuwezesha kutuma picha ambazo huondoshwa sekunde chache baada ya kuzituma.

Kumekuwa na lawama kuhusu faragha katika mtandao wa facebook hasa baada ya mwaka huu kuelezwa kuwa Wakala wa Ulinzi wa Marekani (NSA) imekuwa ikifanya  udukuzi wa taarifa zilizoko katika mtandao huo.

Utafiti huo pia unaonesha kuwa vijana hao sasa wanajiunga na Instagram mtandao unaotoa huduma ya kubadilisha picha,Mike Butcher kutoka Techcrunch.com ameiambia Sky News kuwa Facebook ilikuwa mahali tulivu na faradha hasa kwa wanafunzi wa vyuo vikuu na wahitimu kwa ajili ya kutengeneza kipato na imekuwa maarufu.
Anaeleza kinachotokea sasa ni vijana kutafuta mitandao mbadala ambayo ni  Instagram na Twitter.

Monday, December 16, 2013

TANZANIA IMEJIPANGAJE KATIKA KUKABILIANA NA UDUKUZI?

UDUKUZI NI NINI ?

Ni uchukuaji wa taarifa za mwingine kwa njia ambazo sio halali kwa kutumia vyombo vya mawasiliano anavyotumia mtu husika kama email , simu , kompyuta , tv na vingine vingi .

Taarifa hizi zinaweza kuwa kwa njia ya nyaraka zilizohifadhiwa , zinazofanyiwa kazi ( kama ziko shared ) , kusikiliza mawasiliano ya sauti kama kupiga au kupokea simu , ujumbe mfupi yaani sms na Mawasiliano ya email mtu anayofanya na watu wake au makundi .

Katika siku za karibuni wigo umepanuka kidogo sasa hivi mpaka kwenye anuani za watu kwenye mitandao ya kijamii kama facebook watu wanaouwezo wa kuiba taarifa au kuingia na kupotosha , kwenye majukwaa ya majadiliano pia watu wanaweza kuingia kuvuruga au kuiba taarifa za mtumiaji fulani bila wenye jukwaa kujua .

Kwa mataifa yaliyoendelea Aina hii ya Ujasusi ni njia moja wapo ya kujilinda dhidi ya adui wa nje na wa ndani , adui huyo anaweza kuwa gaidi , jasusi mwenzake , biashara za kimataifa , teknolojia , uuzaji na usambazi wa silaha , taarifa za afya , viwanda na nyingine nyingi .

MATUKIO MAARUFU YA UDUKUZI KIMATAIFA
1 – Miezi kadhaa iliyopita tumesikia na kusoma kwenye vyombo vya habari kuhusu Udukuzi uliokuwa unafanywa dhidi ya viongozi mbalimbali wa nchi za ulaya na amerika ya kusini na mashirika ya ujasusi ya kimarekani .

2 – siku kadhaa kabla ya mkutano wa G20 NA hata wakati mkutano huo unaendelea baadhi ya wajumbe walipokea barua pepe ambazo zilikuwa na program maalumu zilizojiingiza kwenye kompyuta zao na hapo hapo walianza kufuatiliwa na kuibiwa taarifa zao haswa kile walichokuwa wanafanya na kuandika kutumia kompyuta zao na simu , uchunguzi ulipofanyika iligundulika uvamizi huu ulitokea uchina .

3 – wajumbe wa mpango wa nyuklia wa irani walipoenda uingereza kwa ajili ya mkutano Fulani nao waliingiziwa virusi walipowasha tu vifaa vyao vya mawasiliano , virusi hivi vilisambaa mpaka kwao mpaka kwenye vinu vyao vya nyuklia matokeo yake ni kwa baadhi ya vitu kutokufanya kazi sawasawa .
Hili suala kwa Irani pamoja na vikwazo ndio limesababisha uongozi mpya kutaka muafaka na mataifa yaliyoendelea , pia lilisababisha baadhi ya wanasayansi wao kuuwawa kwa njia za kigaidi haswa wale waliokuwepo kwenye mradi huu .

MATUKIO MAARUFU YA UDUKUZI NCHINI
Kwa hapa nchini kuna matukio 3 ambayo ni maarufu lakini hayajawahi kuongelewa sana .
1 – Waziri mmoja na kundi lake walikuwa wanaenda nchi Fulani ya ulaya kwa ajili ya warsha na alitarajiwa kutoa msimamo Fulani , basi alivyofika hotelini kuwasha kompyuta yake kuanza kupekua vitu hapo maharamia wa mtandao walimvamia na kuharibu hiyo kitu aliyokuwa anafanyia kazi siku zote .

2 – Mara kadhaa kumewahi kutokea udukuzi kwenye taasisi zetu zinazosimamia maswala ya mawasiliano haswa TCRA na ilipochunguzwa ikagundulika waingiliaji wengi walitokea nchi ya China , china imekuwa nchi inayongaa ulimwenguni kwenye masuala ya Udukuzi .
3 – Udukuzi uliwahi kufanywa dhidi ya shirika moja la ndege nchini halafu wahalifu wakavamia kwa nia ya kuharibu utaratibu wa urushaji ndege na uhifadhi mwingine wa taarifa , hii ilisababisha ndege moja kukaa uwanjani bila kufanya safari kwa mwezi mmoja kwa sababu za kiusalama na ndege hiyo ilikuwa inaendeshwa na mitambo maalumu kutoka nchi nyingine .

HALI YA TANZANIA
Hali ya Tanzania kusema za ukweli sio ya kuridhisha sana kutokana na mambo 3 makuu .
1 – Sheria za Mawasiliano – Sheria zetu za mawasiliano hazijitoshelezi na wahalifu wengi wanatumia fursa hiyo kufanya uhalifu wao kutoka hapa kupiga wengine au kupitia hapa kupiga wengine wa mbali , tunapenda kuwa na sheria nzuri za mawasiliano zinazoendana na wakati wa sasa na kila idara serikalini itengeneze sheria zake kwa kunukuu sheria mama .

2 – Utumiaji wa Vifaa chakavu – Tunaona watu haswa wenye fedha zao wakinunua vifaa chakavu vya mawasiliano haswa toka nchi za mbali kwa ajili ya kuja kutumia hapa nchini vifaa hivi vingi vimesababisha utengenezwaji wa njia za kivamizi na kwa sababu teknologia zake za kizamani imekuwa rahisi wa wahalifu kuzichezea na kufanya wanachojua .
3 – Vifaa visivyokidhi viwango – Tumeona watu wananunua simu ambazo hazina viwango na kuzitumia kwenye shuguli za uhalifu , simu nyingine zinapunguzwa baadhi ya vitu ili ziweze kufanya kazi nchini , watu maofisini wanaingiza programu kwenye kompyuta zao ambazo hazina leseni au leseni bandia yote hii haitakiwi .

4 – Kutokufuata taratibu za manunuzi – Hapo juu nimesema hatuna sheria za mawsiliano na tumezoea kununua vifaa chakavu , tukiwa na hivyo viwili tutaweza kuwa na utaratibu mzuri wa kununua vifaa haswa vya mawasiliano maofisini na kwenye idara za serikali utakaofuata vitu hivyo viwili .

NINI KIFANYIKE
Ni wakati mzuri sasa kwa Taasisi muhimu nchini kama Mabenki , Polisi , Tume ya mawasiliano , Kampuni za Mawasiliano ya Simu na Intaneti , taasisi za elimu kama vyuo na shule kuwa na taratibu za kufundisha watu matumizi salama ya vifaa vya mawasiliano , ununuzi mzuri wa vifaa vya mawasiliano na uuzaji mzuri wa vifaa vya mawasiliano .

Tufanye hivi huku tukingoja sheria mama wa mawasiliano iboreshwe na wengi wataboresha masomo yao kuzingatia sheria mama ya mawasiliano nchini kulingana na hali tuliyonayo .

Ningependa kuona sheria mama ikiandikwa kutokana na mila na tamaduni za mtanzania sio nje ya hapo , hata pale mtu akisoma itoe harufu ya utanzania au uafrika mashariki .

Kupambana na udukuzi wote sio rahisi lakini tunaweza kupunguza uwezo wa kufanyiwa udukuzi kwa kuhakikisha tuna vifaa vizuri vya mawasiliano na kufuata taratibu za utumiaji .
YONA FARES MARO
0786 806028

Saturday, December 14, 2013

MUONGOZO WA KUTENGENEZA TOVUTI HUU HAPA

 

Kitabu hiki kipo tayari. Wasiliana kwa namba 0713 309 314 au 0763 309 314 na Mushi Richard, Mpesa: 0755872462, Tigopesa: 0713643703 lipia kitabu chako mtumie email yako kisha akihakiki hela imeingia anakutumia kitabu kilicho katika mfumo wa Soft Copy. Ni TSHS. ELFU KUMI NA MBILI TUU (12,000/=). Hata kama upo mkoani.

MICROSOFT KUWASAIDIA WANAFUNZI WA VYUO KUPITIA STUDENT ADVANTAGE




Kampuni ya Microsft Corporation imeanzisha programu mpya ambayo itawawezesha wanafunzi kufanya mazoezi yote wanayopewa shuleni kupitia teknolojia ya habari na mawasiliano.

Kampuni hiyo imebuni programu mpya ya Student Advantage ambayo itawawezesha wanafunzi kupeana kazi za shule,mazoezi ya nyumbani na masuala yote muhimu ya kitaaluma.

Mpango huo uliotangazwa hivi karibuni wakati kampuni hiyo ikitambulisha programu ya Microsoft Office 365 Education ambayo inakadiriwa kutumiwa na zaidi ya wanafunzi milioni 110 wa vyuo 35,000,idara na wahadhiri mbalimbali duniani.

Programu hiyo itawapa fursa wanafunzi kuitumia kupitia huduma zilizopo ambazo ni Microsoft Word na OneNote ambazo zinafanana na huduma za PowerPoint na Excel.

Mpango huo umeanza rasmi Desemba Mosi mwaka huu,huku vyuo mbalimbali duniani vikipewa leseni ya Office 365 ProPlus kwa wanafunzi wahadhiri pamoja na wakuu wa idara watakuwa wanatumia programu yenye leseni ya Office Proffesional Plus bila gharama zozote.Huduma hizo zote zitawapa wanafunzi nafasi wanafunzi kupata maarifa mbalimbali kupitia mtandao wakiwa nyumbani na huduma nyingine ambazo zipo kwenye programu hiyo yenye vitu vingine vitakavyomwezesha mwanafunzi kuwasiliana na wanafunzi wengine waliopo katika vyuo mbalimbali duniani.

Mkuu wa Kampuni hiyo katika nchi za Afrika Mashariki na Kati Mark Chaban anasema wamefanikiwa kutembelea vyuo 30 binafsi na vya umma pamoja na Wizara mbalimbali za elimu ili kutoa mafunzo kuhusu utumiaji wa programu hiyo ambayo ipo chini ya International Data Corporation (IDC) ambayo itakuwa ikikusanya taarifa za maendeleo ya wanafunzi watakaokuwa wakitumia ili waweze kupata ajira na kuboresha maisha yao.

Kampuni hiyo imesema inakusudia kufuatilia uwezo wa wanafunzi katika kutumia huduma hiyo ambapo watakaoonekana kuwa na kiwango cha juu watachukuliwa na kupelekwa kwenye makampuni mbalimbali na kulipwa mishahara minono.

Microsoft imepanga kutengeneza ajira kwa asilimia 28 ifikapo mwaka 2020 ambapo miongoni mwa wanafunzi milioni 115 watakaoajiriwa kwa vigezo vilivyowekwa .

Monday, November 25, 2013

MAADHIMISHO YA MIAKA 10 YA MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA: MIAKA 10 YA MAPINDUZI YA MAWASILIANO TANZANIA

 

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inasheherekea maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwake huku yakiwemo mafanikio makubwa dhahiri na ya kujivunia katika sekta ya mawasiliano nchini.
 
TCRA ilianzishwa rasmi mnamo tarehe 23 mwezi Novemba mwaka 2013 ili kusimamia Sekta ya Posta na Mawasiliano ya Elektroniki ikkiwemo simu, utangazaji, wavuti pamoja na huduma za Posta. TCRA ilkianzishwa kwa Sheria Na. 12 ya mwaka 2003 iliyoziunganisha Tume ya Mawasiliano Tanzania (TCC) na Tume ya Utangazaji Tanzania (TBC).


Mkakati mahususi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ni “Kuboresha Maisha ya Watanzania kupitia mfumo makini na thabiti ili kuhakikisha kunakuwa na huduma za mawasiliano kwa wote nchini”. Katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, Tanzania imeshuhudia kukua kwa kasi kwa Sekta ya Mawasiliano. Mamlaka ilianzisha mfumo wa leseni za Muingiliano mnamo tarehe 23 Februari 20005. 

Mfumo huu wa leseni za muingiliano (Convergence Lisensing Framework) umekuwa chachu ya kuongezeka kwa miundombinu mbalimbali ya mawasiliano, huduma mbalimbali kwa kutumia mtandao wa mawasiliano ikiwemo wavuti (internet) na utangazaji.

Makampuni ya simu yameongezeka kutoka kampuni moja ya simu TCRA ilivyoanzishwa mwaka 2003 hadi kufikia makampuni saba (7) yenye wateja wenye laini za simu takribani milioni 28 kulinganisha na idadi iliyokuwepo miaka kumi iliyopita. Huduma za simu za mkononi zimebadilisha maisha ya Watanzania kutokana na huduma mbalimbali zinazopatikana kupitia simu za mkononi. Kuanzia huduma za kutuma fedha kupitia simu, malipo ya Ankara mbalimbali na huduma nyingine nyingi zilizobadilisha maisha na uchumi wa wananchi wa taifa hili. 

Sekta ndogo ya Posta nayo haijabaki nyuma kwani kumekuwepo na ongezeko la watoa huduma kutoka mmoja hadi zaidi ya hamsini wenye kutoa hduma ndani nan je ya Tanzania. Tunatarajia mabadilikjo makubwa kwa watanzania hasa baada yan kukamilika kwa mradi wa anwani mpya za makazi na misimbo ya Posta.


Hali kadhalika, yako mabadiliko makubwa sana katika msekta ndogo ya utangazaji. Kutoka nchi yetu kuwa na Radio moja hadi Zaidi ya redio 85. Aidha kutokuwepo kwa Kituo cha Utangazaji wa Runinga hadi vituo vya utangazaji vipatavyo 26. Watumiaji wa wavuti (intanet wameongezeka kutoka watumiaji million moja hadi takribani milioni 8 na ushee. Sekta ya Mawasiliano imekuwa chimbuko la maendeleo ya nchi kwa kutoa ajira kwa watanzania wengi na hali kadhalika kuongeza mapata ya serekali kwa tozo na kodi mbalimbali zinazotolewa katika sekta.. 


Mamlaka ya Mawasiliano imeshinda tuzo mbalimbali katika masuala ya Udhibiti na Usimamizi Bora wa Huduma za mawasiliano nchini katika kipindi cha kuweko kwake miaka kumi iliyopita. Nchi mbalimbali zimekuja Tanzania kujifunza udhibiti na usumamizi wa masuala nyeti ya mawasiliano kama vile masuala ya uhamaji kuelekea mfumo mpya wa utangazaji wa dijitali, Mifumo ya uanzishwaji wa anwani za makazi na misimbo ya posta, Usimamizi mzuri wa masafa na namba za mawasiliano na mambo mengine mengi. 


MATUKIO MBALIMBALI KATIKA MAADHIMISHO TANGU 25 – 29 NOVEMBER 2013

Katika kusheherekea miaka kumi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, kutakuwa na maadhimisho ya wiki nzima yenye matukio mbalimbali. Tukianzia na mkutano huu na waandishi wa habari uliokusudia kutoa taarifa kwenu na kwa wananchi kuhusu maadhimisho haya, kutakuwa na matukio kadha wa kadha kuelekea kilele cha sherehe za maadhimisho yanayotarajiwa kufanyika tarehe 29 Novemba 2013.Maadhimisho haya yanafanika chini ya kauli mbiu ya; Miaka 10 ya TCRA: Miaka Kumi ya Mapinduzi Katika Sekta ya Mawasiliano


Kesho tarehe 26 Novemba 2013 kutakuwa na tukio maalumu kwa wafanyakazi wa mamlaka ambapo wale waliokuwepo tangu wakati wa kuanzishwa kwa TCRA watatunukiwa vyeti pamoja na zawadi mbalimbali kutambua mchango wao kwa taasisi.


Aidha siku ya tarehe 27 Novemba 2013; kutakua na sherehe ya kutoa udhamini kwa wanafunzi wanaosoma vyuo vya elimu ya juu wanaochukua masomo ya mawasiliano, sayansi na teknolojia. TCRA kwa kipindi cha miaka miwili mfululizo imekuwa ikitoa udhaminim katika masomo hayo kwa wanafunzi mahiri kwa nia ya kukuza weledi na kuboresha utumishi katika sekta ya mawasiliano chini ya kinachoitwa “TCRA ICT SCHOLARSHIPS” kwa wanafunzi wa digrii ya kwanza, digrii za Uzamili na Uzamivu.

 
Kuanzia tarehe 27 – 29 Novemba, kutakuwa na maonesho maalumu katika viwanja vya ukumbi wa mikutano wa Mlimani City ambapo watoa huduma mbalimbali za mawasiliano nchini wataonesha mafanikio yao na huduma wanazotoa kwa wananchi. Napenda kuchukua fursa hii kuwasihi waandishi wa habari kuhudhuria maonesho haya ili kujifunza na kutumia fursa hiyo kuelimisha jamii ya watanzania kuhusu huduma mbalimbali za mawasiliano zinazopatikana nchini ili wachangamkie fursa.


Hali kadhalika, katika maadhimisho haya, TCRA imeandaa washa maalumu ya siku mbili wa wadau wa mawasiliano kujadili fursa, changamoto pamoja na namna gani kwa pamoja tunavyoweza kufanya mawasiliano kuwa bora Zaidi nchini mwetu. Warsha hiyo itafanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City na itafunguliwa rasmi tarehe 28 mwezi huu na Mhe.Dr Mohammed Gharib Billal Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na utaendelea hadi tarehe 29 Novemba 2013. 

 
Wadau mbalimbali wa Mawasiliano kama vile kituo cha Habari cha Tanzania Network Information Centre (tzNIC), Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote - (UCSAF), Wamiliki wa Vyombo Vya Habari -(MoAT), na Umoja wa Makampuni ya Simu  (MoAT-Mobile Telephony Companies), Africa Media Group, Agape Associates and TTCL watawasilisha mada mbalimbali.


Vyombo vya Habari vinakaribishwa katika shughuli zote za maadhimisho ya Miaka 10 ya TCRA ili kutoa elimu kwa umma lakini pia kama fursa ya kujionea mafanikio ya sekta ya mawasiliano katika kipindi cha miaka kumi iliyopita ili kuwawezesha wananchi kufahamu tulikotoka, tunakoenda na fursa zilizoko katika sekta ili kuboresha maisha yao. 

Imetolewa na: 
Mkurugenzi Mkuu 
25th November 2012

Tuesday, November 19, 2013

JAMII PRODUCTION-DAKIKA 90 ZA DUNIA:HATARI YA BUNDUKI ZA KUCHAPISHWA NCHINI MAREKANI

Bunduki ya plastiki iliyotengenezwa kwa mashine ya 3D ikifyatua risasi wakati wa majaribio
Photo credits: Screenshot from ATF Video
Kama tulivyoripoti katika ripoti hii ya Septemba 21, mauaji ya kutumia bunduki ni kati ya matatizo makubwa nchini Marekani.
Lakini pia, uwezo wa nchi hiyo katika teknolojia umesaidia kupunguza madhara ya vifo hivyo kwa kuwezesha kukamatwa kwa silaha kabla hazijafanya madhara.
Hii inajumuisha pia kutumia vifaa maalum vya kugundua vitu vya chuma ambavyo mtu anaweza kuwa ameficha. Hata hivyo, kukua huko kwa teknolijia pia kuna athari katika mapambano dhidi ya uhalifu.
Wiki hii, kitengo kinachojishughulisha na udhibiti wa Pombe, Tumbaku, Bunduki na Milipuko nchini Marekani (ATF) kimetoa ripoti kuhusu athari ama madhara yanayoweza kusababishwa na bastola za plastiki zinazochapishwa katika umbo halisi (3D Guns)

Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).
Bahati Alex (L) Capital Radio Jijini Dar es Salaam na Mubelwa Bandio (R) wa Jamii Production Washington DC
Hii ilikuwa ripoti ya Novemba 16, 2013

Kwa maoni, ushauri, nk usisite kutuandikia jamiiproduction@gmail.com

Monday, November 18, 2013

GOOGLE NA MICROSOFT KUDHIBITI PICHA ZA KUDHALILISHA WATOTO



Kampuni za Google na Microsoft zinazoongoza duniani kwa mitandao yao kutumika kutafuta taarifa mbalimbali zimekubaliana kuchukua hatua za kuhakikisha inakuwa vigumu kupata picha zinazowadhalilisha watoto katika mitandao.

Maombi kufikia 100,000 yakitafuta picha hizo, hayatapata matokeo yoyote ya utafutaji picha za kudhalilisha watoto na taarifa nyingine zilizo kinyume cha sheria.

Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron, ambaye alitoa wito kwa kampuni hizo kuchukua hatua za kuwanusuru watoto kutokana na udhalilishaji huu, amepongeza hatua hiyo.

Lakini ameonya kuwa lazima hatua hiyo itoe matokeo mazuri, vinginevyo ataleta sheria mpya ya kuyabana makampuni hayo ya mawasiliano.

Mwezi Julai, 2013, Bwana Cameron alizitaka kampuni za Google na Microsoft ambazo kwa pamoja zinachangia asilimia 95% ya utafutaji wa taarifa mbalimbali kwa njia ya mtandao, kuchukua hatua zaidi ili kuzuia watu kupata picha mbaya.

Alisema kwamba wlitakiwa kuhakikisha kuwa maombi yanayotumwa kutafuta taarifa ambazo zinalenga kupata picha chafu, yasitoe majibu yoyote.

Kwa sasa kampuni zote mbili zimeanzisha "programu mpya ya kompyuta" ambayo itazuia utafutaji wa picha zinazowadhalilisha watoto.

Akiandika katika gazeti la Uingereza la Daily Mail, mwenyekiti mtendaji wa Google Eric Schmidt amesema: "Mabadiliko haya yameondoa maombi zaidi ya 100,000 ambayo huenda yalihusishwa na udhalilishaji wa watoto.

"Likiwa jambo muhimu, hivi karibuni tutaweka mabadiliko haya katika zaidi ya lugha 150, hivyo matokeo ya hatua hii kuwa ya dunia nzima."

Ameendelea kueleza kazi ya kuzuia picha za udhalilishaji watoto, kwa kusema:"Sasa tunaonyesha - kutoka mtandao wa Google na mengine, juu ya chumba cha kutolea maombi ya kutafuta taarifa mbalimbali kwa maombi zaidi ya 13,000.

"Maonyo haya yanaonyesha wazi kwamba udhalilishaji wa watoto ni kinyume cha sheria na kutoa ushauri wa mahali pa msaada."

Jumahili, kampuni mbili hizo za Google na Microsoft zitaungana na kampuni nyingine za internet katika ofisi za waziri mkuu wa Uingereza zilizopo Downing Street, kwa ajili ya Kikao cha Usalama wa Internet.
chanzo:BBC

Friday, November 15, 2013

MAMBO MANANE YA KUZINGATIA JUU YA MATUMIZI YA MITANDAO YA JAMII


 

Siku hizi, katika kila watu kumi wanaotumia mtandao, basi angalau watano kati ya hao wanatumia mitandao jamii. Kuna baadhi ya watu wamegeuza mitandao hii kuwa kama ni sehemu ya mawasiliano, ama ya mtu kwa mtu au ya kibiashara. Siku hizi, si kitu cha kushangaza kusikia mtu maarufu au kiongozi fulani atakuwa kwenye Facebook saa fulani kwa ajili ya kujibu maswali ya wananchi / mashabiki wake. Mitandao hii ni kama vile Facebook, Twitter, Jamiiforums nk, hivyo basi, hatuwezi kuepuka ushawishi wa mitandao jamii katika jamii yetu.

Matumizi bora ya mitandao jamii huweza kuleta faida nzuri sana, ila huwa kinyume pale inapotumika sivyo, ama kwa kutokujua ama kwa kuamua. Hivyo leo hii tuangalie mambo kadhaa ya kuepuka unapotumia mitandao jamii.


1. EPUKA KUJIACHA WAZI KWENYE MITANDAO JAMII.



Kuna baadhi ya watu wamegeuza mitandao jamii ni dunia yao nyingine kabisa, wao kila kitu wanachokifanya utakiona kwenye mitandao jamii, kala nini, anamchumbia nani, kavaa nguo gani nk. Mitandao jamii ni uigaji (Simulation) ya maisha ya halisi.Tukiwa kwenye maisha halisi, sio watu wote wanaoweza kujua maisha yako kwa undani,kwani kuna vikomo, kuanzia wale mulio nyumba moja, munaofanya kazi pamoja nk.


Ingawa kwenye mitandao jamii wengi wanaweza kuchunga kwa kutumia michungo ya ufaragha (Privacy setting) lakini si wote wanaojua hilo, pia tumeona mamia ya akaunti za watu zikivamiwa na wavamizi wa mtandao (Hackers) na kuweka hadharani taarifa zao nyingi. Hivyo epuka kuweza kila kitu kwenye mitandao jamii, kula na kikomo na pia anza kuchunga marafiki zako juu ya nani anaweza kuona nini. Unaweza kuangalia Video HAPA jinsi ya kuchunga ufaragha kwenye Facebook.


2. JICHUNGE KWENYE UTUMAJI.
 
Je ushawahi kusikia mtaani wanasema jamaa ana gubu (anaongea sana?), kwenye mitandao jamii pia kuna watu wana gubu, wanachonga sanasana. Hawa ni wale watu ambao kila dakika wametuma kitu kipya, hii sio tu hufanya kupoteza mvuto kwa wanaokufuatilia, bali pia umuhimu wa makala zako hupungua. Binafsi huondoa watu aina hii kwenye mlisho wa maboresho (activities feeds) bila hata kujiuliza.

Hivyo, ili kuepuka kutengwa au kuonekana unachonga sana, chunga idadi ya maboresho unayotuma kwa siku.


3.EPUKA KUTUMA MAKALA ZA NGONO, DINI AU SIASA KAMA WEWE SI MUHUSIKA.


Hivi ni vitu ambavyo huathiri watu wengi sana, chukulia mfano wewe ni rafiki wa bwana X, unafungua Facebook au Twitter yako unakutana na picha ya ngono imejaa kwenye mlisho wa maboresho toka kwa rafiki yako. Ukweli ni kuwa utajisikia vibaya mno ama kama na wewe ni wa aina hiyo. Hii pia ni sawa na kwa mambo ya dini na siasa.


Tanzania ikiwa ni nchi isiyo na dini, ila watu wake wamechanganyika mnomno, kwenye kila marafiki zako wawili, kuna mmoja ni wa dini nyingine, hivyo epuka kutuma makala za dini zinazoudhi, zenye kebehi au kuudhi wengine. Jaribu kuwa mtu ambaye utaweza kuishi na watu wote. Mfano huu pia tuuchukue kule uraiani, kuna baadhi ya watu hukimbiwa, hivyo chukua tahadhari kabla ya kukimbiwa.

4. USIHAMISHIE HASIRA ZAKO KWENYE MITANDAO JAMII.
Kuna baadhi ya watu, wakishauziwa nyumbani, hasira zinaishia kwnye mitandao jamii,amini usiamini, mitandao jamii haiwezi kukusaidia kutuliza hasira zako zaidi ya kukupotezea muda na kujidhalilisha. Ni sawa na yule mtu mwenye ugomvi na mke / mume wake halafu anapita kila nyumba kutangazia mapungufu ya mwenza wake, jamii nzima inajua, siku mutakaporudiana, watu wote washajua mapungufu ya mwenza wako, je utafuta toka kwenye vichwa vyao? Kwenye mitandao jamii vilevile, kuna baadhi ya watu kuhifadhi kila unachotuma na siku ya siku watatumia kuja kukashambulia. Kaa mbali na mitandao jamii kama unaona hauwezi kuchunga mhemuko (emotion) wako.


5.SIYO KILA MTU LAZIMA AWE RAFIKI YAKO.


Chukulia mfano mitaani tunamoishi, kuna watu wa aina mbalimbali, na siyo kila mtu ni rafiki yako, kuna baadhi ya watu hata hautaki kuwasogelea kutokana na tabia zao, hii ni sawa kwenye mitandao jamii. Epuka kukubali maombi ya urafiki toka kwa kila mtu, haswaa ambao hauwafahamu. Marafiki sio tu huweza kutumika kujenga taswira yako, bali kuna baadhi ya marafiki si marafiki, hivyo chunga marafiki zako la sivyo ipo siku utakuja kujuta.

6 . UHIFADHI WA HISTORIA
Uhifadhi wa historia - Ni vizuri kujua kila unachofanya kwenye mitandao ya kijamii haswa kutumia account yako kama ni email au nini kinahifadhiwa sehemu , kama umekashifu mtu , kama umejiunga kwenye vikundi vya kiharamia au kama umetafuta kitu kinachohusiana na ugaidi au kutengeneza mabomu yote hii huwa inahifadhiwa usishangae siku moja ukagongewa mlango kuonyeshwa kile ulichokuwa unafanya na rumande moja kwa moja .

7.KUJIUNGA KWENYE VIKUNDI AU UKURASA
Kuna watu wanapenda kulike kurasa za facebook za watu , vikundi na nyingine nyingi bila kufuatilia vizuri , unaweza kulike leo kwa nia nzuri tu kwa sababu ana habari nzuri baada ya siku kadhaa kupata watu wengi mtu huyu au kikundi kinaweza kuanza kuweka mambo yake yaliyojificha na inaweza kukuweka katika nafasi mbaya kama ni katika familia , kazini , utumishi wa umma au sehemu za harakati ingawa una uhuru wa kuchagua .

8 - KUHUSU TABIA ZA MTU 
Kutumia mitandao ya kijamii kama facebook na myingine unaweza kujua tabia za mtu , vile anavyopenda , rafiki zake , wanafamilia wake , mke wake , mume , watoto , wafanyakazi wenzake na tabia nyingine za ajabu au nzuri na vile vile kwenye tekinologia ya mawasiliano siku hizi kuna mfumo wa tabia za watu kujulikana - kile ambacho unapenda kutafuta au kuongelea ndicho utakachokuta kwenye email yako kama tangazo au kurasa yako ya facebook kama TAG 
Hayo ni mambo muhimu kwa ajili ya afya ya utumiaji wa mitandao jamii, usisahau kulike Kurasa yetu ya Facebook kwa makala mbalimbali za IT kila wiki https://www.facebook.com/dudumizi
  

Imeandikwa na Yona Msuya toka tovuti ya dudumizi na Yona Maro wa wanabidii forum

TCRA - WANAOVUJISHA MAWASILIANO YA WATU WASHITAKIWE

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na kampuni za simu za mikononi, zimewataka wateja watakaokumbwa na tatizo la kuvujishwa kwa taarifa za simu, kuripoti kwenye vyombo vya dola ili hatua zichukuliwe.

Aidha imeelezwa kuwa ingawa kumekuwa na mashine za kuzuia taarifa za siri za simu za mikononi kutovuja, baadhi ya wafanyakazi wa kampuni za simu wasio waaminifu wamekuwa wakihujumu wateja kinyume cha sheria kwa kuchezea teknolojia isivyopaswa.

Hadhari hiyo imekuja kukiwa na wimbi la matumizi mabaya ya simu za mkononi nchini Tanzania, ikiwemo matumizi ya teknolojia kutoa 
hadharani mawasiliano ya siri ya watu.

Miongoni mwa matukio ya hivi karibuni, ni taarifa zilizoanikwa kwenye mitandao ya kijamii dhidi ya Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Kabwe Zitto, zikionesha mawasiliano ya siri anayodaiwa kufanya na watu mbalimbali yakidaiwa kuwa ni ya kuhujumu chama chake.

Matumizi mengine ni aliyodai kufanyiwa Mbunge wa Arusha, Godbless Lema, ambapo pamoja na namba za simu kadhaa kudai zinamtumia ujumbe wa matusi, pia alidai upo ujumbe wa matusi unaotumwa kwa watu na namba inayojitokeza ikionesha ni ya mbunge huyo suala alilosema juzi limemchafua kisiasa na kijamii.

Akizungumza jana na mwandishi juu ya matukio hayo, Meneja Uhusiano wa TCRA, Innocent Mungy, alisema kampuni za simu zinaongozwa kwa mujibu wa sheria hivyo hakuna itakayokubali kutoa taarifa za siri za mteja kwa kuwa ni hatari kwao.

Sheria husika ni ile ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta ya mwaka 2010 inayotoa kinga kwa mteja.

“Ninachojua ambacho kinaweza kuonekana na kupatikana kutoka katika kampuni hizo tena kama zikiombwa na Polisi ama vyombo vya usalama kufanya hivyo kwa kulinda usalama wa taifa, ni kuelezwa siku fulani uliwasiliana na nani na saa ngapi na kampuni zinaweza kuchapa taarifa hiyo na kuitoa bila kueleza kilichozungumzwa wazi wazi,” alisema Mungy.

Mungy alisema kampuni za simu zina utaratibu wa mafundi wake kuingia chumba cha kuhifadhi taarifa za siri, na ikiwa mtu ana uhakika namba ya kampuni fulani imetumiwa visivyo, anapaswa kutoa taarifa Polisi ili hatua zichukuliwe kwa kuwa hilo ni kosa la uhalifu wa mtandaoni.

“Naomba ieleweke kwamba haiwezekani mtu asikilize maongezi ya mtu na mtu, ama kusoma ujumbe mfupi wa simu za mkononi, ingekuwa hivyo wafanyabiashara wakubwa wasingefanya biashara wala taarifa za ulinzi na usalama wa nchi zisingekuwa siri leo, watu waondoe hofu na ikiwa mtu katendewa hivyo kweli, aende Polisi kupata haki yake,” alisisitiza Mungy.

Ofisa Mawasiliano wa Kampuni ya simu ya Zantel, Monica Ekelege akizungumzia suala hilo, alisema mafundi katika kampuni za simu wana uwezo wa kuona mawasiliano ya mtu na mtu ikiwa wanatafuta kitu na kujua namba ya mtu, lakini hawawezi kutoa mawasiliano hayo kwa kuwa kampuni nyingi zina mashine ya kuzuia siri.

“Huu ni uhalifu kama uhalifu mwingine, mtu anaweza akachokonoa chokonoa na kuibuka na njia nyingine ya kuvujisha taarifa za mtu, huyu akibainika, sheria haimwachi lakini kwanza kwa kuwa sisi tunafanyakazi chini ya sheria inayomlinda mteja na siri zake, ana mamlaka ya kutushitaki lakini lazima awe na uthibitisho na kuanzia Polisi,” alisema Ekelege.

Ekelege alisema uhalifu mwingi wa simu wanaoufanya watu, wanatumia udhaifu wa baadhi ya mawakala waliozembea kutumia vielelezo stahiki katika kusajili namba za simu, na sasa baadhi wanatumia mwanya huo kufanya uhalifu.

Kuhusu watu wanaotumia simu kutuma ujumbe wa matusi au kufanya uhalifu mwingine kama vile utapeli, Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando, alisema mara nyingi wanaofanya vitendo hivyo ni wenye simu ambazo hazijasajiliwa kwa kufuata utaratibu unaopaswa.

Alisisitiza waathirika wa vitendo hivyo kutoa taarifa Polisi na kampuni yao itatoa ushirikiano kubaini wahusika ili hatua zichukuliwe.

Popular Posts

Labels