Tuesday, March 21, 2017

UBALOZI WA MAREKANI WATOA MAFUNZO KWA BLOGGERS

Blogger katika picha ya pamoja na wawezeshaji  wa Ubalozi wa Marekani

 Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania kupitia kitengo chake cha Mawasiliano ya Umma leo Machi 21,2017 kimetoa mafunzo kwa baadhi ya waandishi na wamiliki wa Blog nchini Tanzania kupitia Mtandao wa Bloggers nchini Tanzania (TBN)ikiwa ni katika kuwajengea uwezo wa kuandika habari zenye weledi kwenye mitandao ya kijamii.

Mafunzo hayo yaliyohusu Uandishi wa Habari kwa kutumia teknolojia mpya yamefanyika ulipo Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania yaliendeshwa na Mwandishi wa Habari,Mpiga picha na Blogger  raia wa Marekani Ricci Shryock anayeishi na kufanyakazi zake kwa sasa mjini Dakar Senegal.

Monday, March 20, 2017

TANAPA INAVYOTUMIA TEKINOHAMA KUTOA HUDUMA ZAKE KWA UMMA

Huu ni mfululizo wa  vipindi vya Serikali Mtandao hapa utaona kwa namna gani TANAPA inavyotumia TEHAMA katika utoaji huduma kwa umma.


Tuesday, March 14, 2017

SERIKALI YA TANZANIA YASISITIZA MATUMIZI YA MITANDAO YA KIJAMII KWA OFISI ZAKE ZA UMMA

Serikali yasisitiza matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano hasa Mitando ya Kijamii katika ofisi mbalimbali za Umma nchini Tanzania katika kutoa habari na taarifa mbalimbali.

Popular Posts

Labels