Saturday, April 13, 2019

MAMBO 10 AMBAYO YAWEZA FANYWA NA SIMU JANJA

 Related image



1.Kutune Gitaa /Kutafuta Ufunguo wa Sauti ya Gitaa
Kulikuwa na wakati ambapo bei ya  vifaa vya umeme kwa ajili ya kutafuta ufunguo wa sauti za gitaa na vifaa vingine ilikuwa ghali ,kwa sasa unachotakiwa ni kupakua program tumishi sahihi kwa ajili ya simu yako ili kukupatia funguo za sauti mbalimbali za gitaa,muafaka wa sauti na maelezo ya kutumia.

2.Ufuatiliaji wa  Mtoto akiwa amelala

Program tumishi hizi zenye akili  zitakuwezesha kuiweka simu yako ndani ya chumba cha mtoto ambapo program hiyo itamfatilia  mtoto aliyelala  kwa  kumsikiliza kama anajongea ama kutoa sauti yake,Kama mtoto atajongea ama kutoa sauti program hii tumishi itagundua kisha itapiga namba kwa mwenyenayo na atafahamu kuwa mtoto ameamka kutoka usingizini.

3. Kipima Kasi

Programu tumishi  kadhaa za Mfumo wa Dunia wa Utambuzi wa Mahali ulipo GPS zinaweza kupima kasi yako kwa usahihi sana unapoendesha lako. Mara nyingi hupangwa kuwa na ufahamu wa kikomo cha kasi katika maeneo mengi na inaweza kukujulisha ikiwa unazidi kikomo hicho. Hii inaweza kuwa na manufaa sana ikiwa kasi ya gari katika gari yako imevunjika au isiyo sahihi mfano.

4. Kipasha joto Mikono

Amini au la, kuna programu tumishi ambazo unaweza kutumia ili kuipasha joto  mikono yako wakati wa baridi,Program hizi huiongoza processor ya simu yako ili simu ipate joto,Kumbuka tu ni kwamba program tumishi hizi zinatumia uwezo mkubwa wa betri ya simu yako,hivyo ni budi uweke tahadhali

6. Kufahamu matumizi ya pombe

Ingawa inaweza kuwa sio wazo bora kuweka imani yako yote katika programu kama hii, bado inaweza kuwa na manufaa kukusaidia kupata kufahamu kiwango cha pombe alichotumia mwendeshaji wa chombo cha moto  na kusaidia kuepusha ajali

7. Vizuizi vya mwendokasi

Aina hizi za programu zinategemea idadi ya watumiaji wanaohusika ili waweze kuwa na matumizi yoyote. Watumiaji wanaweza kutoa taarifa za maeneo yenye vizuizi  ya kasi ambavyo wanaviona katika eneo fulani, na kisha kutoa taarifa kwa watumiaji wengine watumiaji wengine katika eneo hilo. Kwa kutumia GPS, itaeleza  moja kwa moja mtumiaji akikaribia eneo ambapo kuna vizuizi vya mwendo kasi uliowekwa

8.Remote

Yawezekana u miongoni mwa wanaopoteza remote ya vifaa vya kielektroniki ikiwemo Televisheni,radio,dvd,jokovu nk .Baadhi ya program tumishi zinaiwezesha simu yako na kuifanya kuwa remote ambapo itakuwaidia katika vifaa hiyo.

9.Gari Janja

Kwa sasa kuna program tumishi  ambazo zinakuwezesha kutumia simu yako kuiongoza gari kwa baadhi ya mambo ikiwemo kuwasha gari ukiwa nje ,kuwasha na kuzima alamu,kufungua na kufungua milango.

10.Utambuzi wa Vyuma

Hii ni Program Tumishi ambayo inafanya kazi katika simu janja aina ya iPhones na iPads, kuwezesha kutambua vyuma ambavyo haviwezi kuonekana kwa macho kwa urahisi katika eneo husika


Friday, April 5, 2019

UCHUNGUZI WAONESHA TATIZO LA KIMFUMO LILISABABISHA AJALI YA BOEING 737 MAX 8

 Image may contain: aeroplane

Ripoti ya awali ya uchunguzi wa ajali ya ndege la Shirika la Ndege la Ethiopia safari namba 302 inaonyesha kwamba ajali hiyo ilitokana na tatizo la kimfumo katika ndege na kwamba marubani wa ndege hiyo walifanya kila walichoelekezwa na kufuata taratibu zote kwa mujibu wa watengenezaji wa ndege hiyo lakini hawakufanikiwa kuizuia isianguke.

Mfumo katika aina ya ndege iliyoanguka (Boeing 737 Max 8 ) umekuwa katika mjadala mkubwa kiasi cha kusababisha nchi nyimgi kuamrisha kusimamishwa kwa matumizi ya ndege hizo na Wizara ya Sheria, Mkaguzi Mkuu masuala ya Usafirishaji na Kamati za Bunge la Marekani vimeanzisha uchunguzi tofauti na maalum wa namna ambavyo kampuni hiyo ilivyofanya maboresho ya mfumo na walivyopata kibali cha uthibitisho wa ubora toka Mamlaka ya Anga ya Marekani.


Ndege hiyo iliyoanguka Machi 10, 2019 na kuua abiria wote 157, ilikuwa ni ya pili ya aina hiyo kuanguka ndani ya miezi 5 na hilo likazua hofu kwa wasafiri na wasafirishaji kuhusu usalama wa ndege hizo.


Ripoti kamili inatarajiwa kutoka baadae sana, lakini punde nitakapopata nakala ya awali ya ripoti hiyo nitaileta hapa ili kushiriki nanyi juu ya dondoo za uchunguzi huo.


Shirika la Boeing linalotengeneza ndege hizo lilitangaza kwamba lingefanya maboresho ya mfumo huo hivi karibuni lakini inaonekana wamesubiri matokeo haya ili kuhakikisha wanawathibitishia wateja wake kuwa wanaboresha kile kinachowatia hofu kutokana na ajali mbili za ndege zake.

Na: Mubelwa Bandio-Marekani

Thursday, March 28, 2019

APPLE YATOA SASISHO LA PROGRAM ENDESHI YA iOS 12.2


Apple wametoa Sasisho la Program Endeshi ya  iOS 12.2  kwa ajili ya  iPhone, iPad, and iPod toleo ambalo litawezesha wenye vifaa vya hivyo kunufaika za Apple zilizotambulishwa jumatatu ya Machi 25 mwaka huu nchini Marekani ikiwemo huduma ya kupata habari iitwayo Apple News+

 Apple pia wameongeza imoji,ambapo iOS 12.2 itamwezesha mtumiaji wa huduma ya  Siri  iliyopo katika vifaa hivyo kuongoza  Apple TV kwa kutumia  iPhone au  iPad. 

 Miongoni mwa madiliko yaliyokuja na sasisho la iOS 12.2 ni kukusianisha kwa Apple News+ na Apple  News iliyokuwepo mwanzo,
 ambapo huduma hii ya kulipia itawawezesha watumiaji wa vifaa vya Apple waliopakua sasisho hili jipya kupata zaidi ya magazeti mtandao 300,na machapisho mengine ya habari ya kidigitali.

Popular Posts

Labels