Thursday, March 31, 2016

WAHALIFU MTANDAO WADUKUA TOVUTI 20 ZA SERIKALI NCHINI ANGOLA

 

Kikundi cha kihalifu mtandao cha ‪#‎Anonymous‬ kimetekeleza mashambulizi mtandao dhidi ya Nchi ya Angola na kufanikiwa kudukua na kuangusha Tovuti 20 za serikali ya Nchi Hiyo.

Hatua hiyo ya kikundi hicho imefuatia baada ya kushinikiza serikali ya Nchi hiyo kuwaachia watu 17 waliokamatwa kutokana na uasi dhidi ya Serikali ya Rais Jose Eduardo dos Santo.


Tukio hilo la Mashambulizi limepokelewa kwa masikitikomakubwa na jumuia ya wana usalama mitandao huku usaidizi wa dhati kuimarisha usalama kwa tovuti za Nchi hiyo zikichukuliwa.


Matukio ya kushambulia Serikali za Nchi za Afrika kimtandao yamepata kuonekana mara kadhaa ambapo Ghana pia ilipata kua muathirika.

Thursday, March 3, 2016

WHATSAPP NAYO YATANGAZA KUTOTUMIKA KATIKA BAADHI YA MATOLEO YA SIMU DUNIANI IFIKAPO DISEMBA 2016

 WhatsApp

Baada ya Serikali ya Tanzania kuanzisha kampeni ya kuondosha matumizi ya simu zisizohalisi toka Disemba mwaka jana,ambapo simu hizo hazitaendelea kutumika ifikapo Juni mwaka 2016 huku ikielezwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kuwa kuna asimilia 40 ya simu zinazotumika nchini humo ambazo ni halisi. TCRA na Makampuni ya Huduma za Mawasiliano ya Simu za Mkononi Tanzania kwa sasa wanaendesha kampeni ya kuhakiki simu ya mtumiaji kama ni halisi ama si halisi kwa kutumia IMEI ya simu kuituma kwenda namba 15090.

Mtandao wa kijamii wa WhatsApp ulio na watumiaji bilioni moja duniani katika mawasilino miongoni mwao wakiwemo watanzania,nao hauko nyuma katika kutafuta kilichobora kwai umetangaza kuwa ifikapo Disemba 2016 hatutatumika katika baadhi ya simu zilizopo duniani.

Huduma ya WhatsApp haitatumika tena katika simu zinazotumia mifumo kadha ya programu endeshi ikiwemo Blackberry 10, Nokia Symbian S60 na Windows Phone 7.1.
Kampuni ya Facebook inayomiliki huduma hiyo imesema inataka kuangazia kustawisha “huduma katika mifumo inayotumiwa na watu wengi.

Kampuni hiyo imejitetea na kusema kwamba haijawatupa wateja wake ambao wamechangia sana katika ufanisi wake lakini ni kutokana na mabadiliko ya teknolojia.

Orodha kamili ya mifumo ya simu ambayo wateja hawataweza tena kutumia WhatsApp ni hii hapa:
  • Android 2.1 and Android 2.2
  • Blackberry OS 7 and earlier
  • Blackberry 10
  • Nokia S40
  • Nokia Symbian S60
  • Windows Phone 7.1
Kampuni hiyo imesema wakati wa kuanzishwa kwa WhatsApp mwaka 2009, asilimia 70 ya simu wakati huo zilikuwa za BlackBerry na Nokia."

Lakini sasa asilimia 99.5 ya simu zinatumia mifumo ya Google, Apple na Microsoft.
Chanzo:BBC

Popular Posts

Labels