Saturday, May 13, 2017

MAELFU YA KOMPYUTA YADUKULIWA NA KUTEKWA NA KIRUSI CHA 'WANACRYPT'


 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh80LERiKRNxgupfboh34qv2vVwytQNg36nJJ2TqSACXatR81N719A62ASHuzx8Hal9RSBjZGAIkc4Pp7SL10BO30EBafgOq1tUNZ4vp0haW5y_jkTzhsYhVXPgJQkP9o7bkG9M0p7dIvI/s320/27.jpg
Maelfu ya tarakirishi (kompyuta)  za mitandao ya mashirika makubwa kadhaa duniani yamedukuliwa  na kutekwa na watekaji wanadai malipo ili kuwarudishia wenye mitandao hiyo. 

Udukuaji huo umetumia program ya udukuaji iliyotengenezwa na shirika la usalama wa taifa la Marekani (US National Security Agency-NSA) ambalo nalo lilibiwa program hiyo na wajanja. 

Wadukuaji  hao wanaojiita The Shadow Brokers ndio wanaodai kuwa waliiba program hiyo na kuiweka hadharani katika mitandao ya internet. 

Kampuni ya Microsoft ilitengeneza ngao ya kuzuia udukuaji kwa kutumia program hiyo na kuiweka hadharani mwezi Machi, lakini ni wazi watu wengi hawakutumia nafasi kuweka ngao hiyo.  

Kampuni mbalimbali kutoka nchi 99 zinasemekana mitandao yao imetekwa, kumekuwa na malalamiko kutoka Uingereza, Marekani, China, Urusi, Hispania, Italia,Taiwan na nchi nyingi nyingine.

 Kampuni ya ulinzi wa mitandao (Cyber-security) ya Avast imesema imeweza kupata malalamiko 75,000 ya madai ya kuhusu kirusi cha WannaCrypt, kutoka karibu pande zote duniani. 

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiTrlBffM1nKydIZGMKwWyEMJ34zNsl9GJLQivbHq1GWun0rh0HqyPQ1Y175Zww_iS1QFrCUHhyphenhyphenPhTRfDDvWQg0bIuUEvVKfMvoI9Z3eB4qq06fDq0NsAO4bJmsrvxEIaEC9eUkhd4wfu4/s1600/_96034173_cryptor3.png
Hivi ndivyo kompyuta inavyosomeka ukishadunguliwa na kirusi cha Wannacry
Kati ya waliokumbwa na kadhia hii ni Taasisi ya Afya ya Uingereza (National Health Service), hali ambayo imeleta mkanganyiko mkubwa katika hospitali za nchini Uingereza, miadi imevurugwa, wagonjwa wamerudishwa nyumbani, waliokuwa wafanyiwe upasuaji shughuli zimeahirishwa kwani maelezo yote yako kwenye kompyuta na hazisomeki. 

Urusi imesema imeweza kugundua chanzo na inakishughulikia. Huko Ujerumani kampuni ya kuuza tiketi za treni imekubwa na kadhia hiyo wakati maabara ya chuo kikuu kimoja Italy imekutana na tatizo hilo. 

Spain imejikuta ikipata tatizo hilo kwenye kampuni yake kubwa ya simu ya  Telefonica, kampuni ya umeme ya Iberdrola na kampuni ya kusambaza gesi ya Gas Natural, wafanyakazi wa kampuni hizo walielekezwa kuzima kompyuta zote. 

Kampuni ya simu ya Portugal Telecom, na kampuni ya kusafirisha mizigo ya FedEx, ofisi moja ya serikali ya mtaa huko Sweden na kampuni ya simu za mkononi ya Megafon ya Urusi ni kati ya wahanga wa tatizo hili.

 Nani hasa waliosababisha hili? Wataalamu wengine wanasema wahusika inawezekana waligundua mapungufu katika program ya Microsoft, NSA waliliona hilo pia na walitengeneza program iliyokuwa inaweza kuteka kompyuta zote zinazotumia Microsoft, program hiyoikaibiwa na wezi wanaojiita (The Shadow Brokers), wezi hawa walianza kuinadi program hiyo katika mtandao na hatimae tarehe 8 April 2017, wakaigawa bure kwa kusambaza password mtandaoni. Wakidai wamefanya hivyo kama njia yao ya kumpinga Rais Donald Trump. 

Microsoft tayari wameshatengeneza program ambayo itakuwa inaweza kutoa taarifa kama kompyuta yako imeingiliwa na udukuzi wa WannaCrypt.
CHANZO:theiringa.blogspot.com

Friday, May 12, 2017

WANAOASAJILI LAINI ZA SIMU BILA UTARATIBU KUKAMATWA


 Related image

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kuanzia sasa itakamata mtu yoyote anayesajili laini za simu kwa kuchakachua au bila kufuata utaratibu na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria.

Agizo hilo pia limeelekezwa kwa kampuni ya simu ambayo itaunganisha laini ambayo haijasajiliwa itaunganishwa kwenye mashtaka na mtu aliyesajili laini feki.

Mwanasheria Mwandamizi Mkuu wa TCRA,Johanes Karungura amesema mamlaka iko makini katika kulinda usalama wa mitandao na usalama wa nchi.

Thursday, May 11, 2017

JINSI YA KUJILINDA NA SHAMBULIO LA KIMTANDAO KWA GOOGLE DOCS

WATUMIAJI BILIONI MOJA WA GMAIL HATARINI KUDHURIWA KIMTANDAO


Watumiaji wa Gmail takribani bilioni moja duniani wako hatarini  kudhuriwa na uhalifu mtandao aina ya Phishing ambao umelenga programu tumishi ya Google Docs.Yusuph Kileo mtaalamu wa makosa ya Kidigtali nchini Tanzania  anazungumza na BBC.

Popular Posts

Labels