Friday, May 12, 2017

WANAOASAJILI LAINI ZA SIMU BILA UTARATIBU KUKAMATWA


 Related image

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kuanzia sasa itakamata mtu yoyote anayesajili laini za simu kwa kuchakachua au bila kufuata utaratibu na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria.

Agizo hilo pia limeelekezwa kwa kampuni ya simu ambayo itaunganisha laini ambayo haijasajiliwa itaunganishwa kwenye mashtaka na mtu aliyesajili laini feki.

Mwanasheria Mwandamizi Mkuu wa TCRA,Johanes Karungura amesema mamlaka iko makini katika kulinda usalama wa mitandao na usalama wa nchi.

Popular Posts

Labels