Thursday, December 15, 2016

YAHOO YASEMA WATUMIAJI BILIONI 1 WA MTANDAO HUO WAMEATHIRIWA NA WAVAMIZI WA MITANDAO



 Kampuni ya Intaneti ya Yahoo inasema wavamizi wa mitandao waliiba data za zaidi ya ya watumiaji wake bilioni moja. Tukio hilo linaaminika kufanyika mnano mwaka 2013. 
Katika taarifa yake, Yahoo inasema uvamizi huo wa taarifa muhimu ni tofauti na ule ulioripotiwa mwezi Septemba mwaka huu, ambapo wavamizi hao waliiba taarifa kutoka kwenye akaunti mbalimbali za watumiaji zaidi ya milioni mia tano.



Imeongeza kuwa data zilizoibiwa zinajumuisha majina, anuani, namba za simu,tarehe za kuzaliwa pamoja na nywila (namba za siri).

Lakini kadi za malipo sambamba na akaunti za benki hazikuingiliwa.

Wednesday, December 14, 2016

KAGOYA YASHAMBULIWA KIMTANDAO – TANZANIA NAYO YAASWA KUFUNGA MIKANDA

Kampuni Maarufu ya KAGOYA ya Nchini Japan Imeshambuliwa kimtandao ambapo taarifa binafsi na za kibenki za wateja wake zimedukuliwa.

Uhalifu huu umegundulika mwezi huu (Desemba, 2016) na tayari kampuni husika imesha toa taarifa kwenye vyombo vya usalama vya Nchini humo - Ambavyo pia vimeanza uchunguzi rasmi.

Kampuni hiyo imesema, Wateja wake waliotumia "Credit card " zao baina ya Aprili Mosi , 2015 hadi september 21, 2016 wameathiriwa na uhalifu huu na imewaasa wateja wake wafatilie taarifa za utoaji pesa wa kadi zao.

Taarifa binafsi takriban Elfu 50 pamoja na taarifa za kibenki takriban Elfu 21 zimeathirika katika shambulio hili la kimtandao.

Mjumuiko wa taarifa zilizo ibiwa ni, majina , barua pepe, Namba za simu, Namba za kadi za benki, maneno ya siri (Nywila) pamoja na taarifa nyingine za wateja wake.

Hii si mara ya kwanza kwa Nchi ya JAPANI kupata shambulio kubwa la kimtandao kwa mwaka huu (2016) pekee - Itakumbukwa, Mwezi May mwaka huu (2016) zaidi ya Yuan Bil. 1.5 sawa na Dola Milioni 13 ziliibiwa katika ATM zaidi ya 1400 ndani ya masaa mawili na nusu.



Aidha, TANZANIA hali ya uhalifu mtandao bado ni changamoto inayo hitaji suluhu ya kudumu. Kuibiwa kwa Fedha na Taarifa , Matumizi mabaya ya mitandao, Tovuti kudukuliwa ni miongoni mwa matukio yaliyo jitokeza kwa mwaka huu 2016.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (UUW) imeleza Waziri mwenye dhamana wa wizara hiyo ametaka kupatikana kwa mwarobaini wa wimbi la wizi mtandao unapatikana Nchini.
Akizungumza wakati wa uzinduzi Bodi ya TCRA (Mamlaka ya Mawasiliani Tanzania)  Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa ameitaka Bodi mpya ya TCRA, kuhakikisha wanapata mwarobaini wa kudhibiti ongezeko la wizi wa mitandao unaoendelea kukithiri hapa nchini.

Prof. Mbarawa amesema watanzania wameibiwa kwa muda mrefu kupitia njia ya ujumbe mfupi na kushawishiwa kutoa fedha kwa njia ya udanganyifu na hivyo kuitaka bodi hiyo kutofumbia macho changamoto hiyo.

“Changamoto ya wizi wa mitandao inagusa watanzania wengi, mkiwa na jukumu la kudhibiti mna wajibu wa kuwalinda wananchi”, amesema Waziri Prof. Mbarawa.

Ameongeza kuwa bodi hiyo ihakikishe inasimamia kwa karibu sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa katika kudhibiti ubora wa masuala ya mawasiliano ikiwa ni teknolojia inayokuwa kwa kasi kubwa.

Aidha Prof. Mbarawa ameitaka bodi hiyo kuendelea kudhibiti wimbi la meseji za uchozezi zinazotumwa na baadhi ya wananchi kwa kukosa maadili.

Katika kuimarisha huduma ya teknolojia ya habari na mawasiliano nchini Waziri Prof. Mbarawa ameikata TCRA kufanya maamuzi ya haraka na kuwa wabunifu ili kuweka mazingira endelevu ya kukuza sekta hiyo.

Aidha, Mwenyekiti wa Bodi mpya ya TCRA Dkt. Jones Kilimbe amesema kuwa pamoja na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta hiyo, Bodi itahakikisha inapata suluhu ya changamoto hizo ndani ya muda mfupi.
Hatuna Budi kutambua kua janga la uhalifu mtandao ni kubwa na athari zake zimekua zikionekana situ kwa nchi zisizo na teknolojia nzuri ya kukabiliana na uhalifu mtao bali pia Nchi zilizo endelea zimekua wahanga wa janga hili.

Taifa la Tanzania halina budi bali kuanza na utayari uliombatana na kujipanga upya na vizuri kukabiliana na Wimbi la uhalifu mtandao nchini.

Changamoto za urasimu, matumizi makubwa ya pesa kwenye kampeni za kukuza uelewa zinazokosa matokeo chanya pamoja na kutojiongezea elimu ya mara kwa mara ya kukabiliana na uhalifu huu mtandao lazima ipaiwe suluhu.

Sheria Mtandao pekee haziwezi kutuvusha kwenye wimbi hili la ukuaji wa uhalifu mtandao nchini, Lazima mambo mengine muhimu ya kukabiliana na uhalifu mtandao yafanyiwe kazi.

Naziasa taasisi binasfi na za serikali kujenga tabia ya kutoa taarifa ya matukio ya kishambulizi mtandao mara tu yanapo gundulika ili iwe rahisi kupatiwa suluhu. Bila kufanya hivyo wahalifu mtandao wataendelea kupata nguvu.

Kwa sasa Tanzania, Hatujafikia pabaya sana kulinganisha na mataifa mengine – Ila, Kama hatua za haraka na za dhati za kujipanga na kufunga mikanda hazitachukuliwa mapema, Mbele yetu ni mbaya Mno.

Kumeonekana mapungufu makubwa maeneo mbali mbali Nchini ambayo yanaweza kupelekea taifa kutumbukia kwenye hali mbaya ya uhalifu mtandao ambapo taarifa na tafiti mbali mbali zinazo fanywa nchini na nje ya nchi zime baini mapungufu mabali mbali yanayoweza kupelekea wadukuzi kutuingiza matatizoni.
Na:Yusuph Kileo


Tuesday, December 6, 2016

TUZO ZA UMAHILI KWA WAANDISHI WA BLOG ZAJA


Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na wamiliki wa blog nchini humo inatarajia kuanzisha tuzo za umahiri kwa waandishi wa habari wa mitandao ya kijamii (blogs) nchini kuanzia mwaka 2017.

Katika hotuba yake ya kufunga Mkutano Mkuu na semina ya wanachama wa umoja wa waendeshaji wa blog nchini jijini Dar es salaam leo Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye (Pichani)amesema kuwa lengo la tuzo hizo ni kuzisaidia blogs za Tanzania kubobea katika nyanja tofauti ikiwemo kilimo, mifugo, viwanda, hifadhi ya jamii kwa nia ya kuipa heshima tasnia ya habari nchini.

Waziri Nape alisema kuwa tayari Serikali imeanza mazungumzo na   makampuni na taasisi mbalimbali kwa ajili ya kudhamini tuzo hizo ili kuhakikisha kuwa washindi wanapatikana kwa uwazi.
Waziri Nape pia amewataka wamiliki na watendaji wa blogs nchini kushirikiana na Serikali ili kuweza kuijenga nchi.

Monday, December 5, 2016

SERIKALI YAITAMBUA RASMI MITANDAO YA KIJAMII (BLOG)

Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji wa Serikali Dk. Hassan Abbas (kulia), akihutubia wakati wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Tanzania Bloggers Network (TBN), Dar es Salaam leo asubuhi. Kushoto ni Mwenyekiti wa muda wa TBN, Joachim Mushi.
Mwanahabari na Blogger  Frederick Katulanda (kulia), akiuliza swali.
Mwenyekiti wa muda wa TBN, Joachim Mushi (kushoto), akiwaelekeza jambo mablogger


Mkutano ukiendelea.

Mablogger kazini

Blogger Baraka kutoka Bukoba akiuliza swali.
Mwezeshaji wa mkutano huo Maxsence  Mello akitoa mada.

Bloggers wakifuatilia mada.
Mwendeshaji wa mtandao wa FullShangwe, John Bukuku akichangia jambo kwenye mkutano huo.
Maofisa wa Kitengo cha Uhusiano wa Benki ya NMB wakibadilishana mawazo. Kushoto ni Doris na Joyce Nsekela.
Blogger kutoka mkoani Arusha, Tumaniel Seria (kulia), akiuliza swali. Kusho ni William Malecela mmiliki wa mtandao wa Mwananchi na katikati ni mmiliki wa Blog ya Michuzi Issa Michuzi.



Mmiliki wa mtandao wa Kamanda wa Matukio, Richard Mwaikenda akichangia jambo.
Picha ya pamoja na mgeni rasmi.

Serikali  imetangaza rasmi kuitambua mitandao ya Kijamii (Bloggers) kuwa chombo cha habari nchini.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji wa Serikali Dk.Hassan Abbas Dar es Salaam leo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Tanzania Bloggers Network (TBN).

"Serikali sasa inaitambua rasmi mitandao ya kijamii kuwa ni chombo cha habari kama ilivyo vyombo vingine nchini hivyo nawaomba wakuu wa vitengo vya habari serikalini kushirikiana na wanamitandao hiyo katika kutoa taarifa mbalimbali" alisema Abbas.

Abbas alivitaka vyombo vya habari hasa magazeti pale wanapotumia picha kutoka mitandao ya kijamii kueleza chanzo cha picha hiyo tofauti na ilivyo hivi sasa ambapo picha zao zinatumika bila ya kutaja chanzo.

Katika hatua nyingine Abbas alisema Bloggers haina tofauti na vyombo vingine hivyo ni vema wanapotoa habari zao kuzingatia sheria na weredi wa kazi vinginevyo sheria itawakumba kama ilivyo kwa magazeti na vyombo vingine. 

Abass aliwataka wanamitandao hao kujiunga na TBN ili iwe rahisi kutatuliwa changamoto walizonazo kuliko kila mmoja kuwa kivyake.

Wanamitandao hao  wakizungumzia changamoto waliyonayo walimwambia mkurugenzi huyo kuwa  wamekuwa wakibaguliwa na maofisa habari wa serikalini ikiwa pamoja na kunyimwa 'Press Card' jambo linalokwamisha utendaji wao wa kazi.
Picha na Habari:Dotto Mwaibale


Sunday, December 4, 2016

YUSUPH KILEO MTANZANIA ALIYETWAA TUZO YA MWAKA YA USALAMA MTANDAONI


Yusuph Kileo baada ya kukabidhiwa tuzo


Mtaalamu wa masuala ya usalama mtandaoni Yusuph Kileo hivi karibuni alipata Tunzo ya "Cybersecurity expert of the year" Ikiwa ni katika kutambua mchango wake  katika mataifa ya Afrika.
 
Tuzo hizo zilitolewa Nairobi nchini Kenya ambapo Mgeni rasmi alikua ni PS au KM wa wizara ya mipango na Majimbo (Ugatuzi) - Kenya Mheshimiwa Saitoti Torome.Kwa ujumla zilitolewa tunzo 31 katika makundi tofauti.


CHAMA CHA WAMILIKI NA WAENDESHA MITANDAO YA KIJAMII KUFANYA MKUTANO WAKE MKUU

-->  
Mwenyekiti wa muda wa Chama cha Wamiliki wa Blog (TBN),Joachim Mushi akizungumza na waandishi wa habari
Ofisa Uhusiano wa NMB,Doris Kilale akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi Milioni 10 kwa Mwenyekiti wa muda wa Chama cha Wamiliki wa Blog (TBN),Joachim Mushi kwa ajili ya mkutano mkuu utakaofanyika Desemba 5 hadi 6 jijini Dar es salaam


 Chama cha Wamiliki/Waendeshaji wa Mitandao ya Kijamii nchini 'Tanzania Bloggers Network' (TBN) kitafanya mkutano wake kwa siku mbili kuanzia kesho jijini Dar es salaam ukiwahusisha wanachana wake toka mikoa mbalimbali nchini.

Akitoa taarifa ya mkutano huo iliyoambatana na upokeaji wa hundi ya shilingi milioni 10 toka NMB Mwenyekiti wa muda wa TBN Joachim Mushi amesema lengo la mkutano huo ni wanatasnia kupewa semina juu ya uendeshaji mitandao ya jamii kwa manufaa, upashaji habari kwa kutumia mitandao yao kwa kuziangatia maadili na namna ya kunufaika na mitandao hiyo kwa waendeshaji (kujipatia kipato) hasa ukizingatia kuwa wapo baadhi yetu tunaifanya kama ajira nyingine.
-->

Thursday, November 3, 2016

TTCL NA HUAWEI WAZINDUA MTANDAO WA 4.5 G

 


Kampuni ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ya Huawei Tanzania na Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) zimeungana na kuzindua mtandao wa 4.5 utakaokuwa wa kwanza kwa mitandao yote nchini Tanzania.

Mkurugenzi Mtendaji wa Huawei Tanzania Bruce Zhang amesema uzinduzi huo unadhihirisha mafanikio ya TTCL kwenye safari ya mabadiliko ya kukua kibiashara nchini.

Hivi karibuni serikali ya Tanzania ilitangaza kumiliki hisa zote za TTCL baada ya kuchukua asilimia 35 zilizokuwa zinamilikiwa na Kampuni ya Bhart Aitel.

DAR ES SALAAM:RAIA WATATU WA PAKSTANI WAHUKUMIWA KWA KOSA LA KUMILIKI MITAMBO YA MAWASILIANO BILA LESENI

Raia watatu kutoka Pakstani wamehukumiwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kulipa faini ya shilingi milioni 120 na iwapo watashindwa watatumikia kifungo cha mwaka mmoja jela kutokana na kosa la kula njama,kuingiza nchi Tanzania vifaa vya kielektroniki vya mawasiliano bila kuwa na leseni ya TCRA,kuvisimika,kuendesha huduma za mawasiliano ya simu za kimataifa bila kibali kutoka TCRA,kukwepa malipo na kusababishia serikali na mamlaka hiyo hasara ya shilingi milioni 140,049,000.

Raia hao wa Pakstani ni Hafeez Irfan (32),Mirza Baig (41) na Irfan Baig (46) na wakidaiwa kutenda makosa hayo katika Hoteli ya Butterfly iliyoko Kariakoo,Wilaya ya Ilala katika chumba namba 905.
 

Wednesday, October 26, 2016

WATEJA WA TIGO PESA KUVUNA BILIONI 6.04 GAWIO LA KUMI LA ROBO MWAKA

Mkuu wa Huduma za Fedha kwa njia ya simu wa Tigo Ruan Swanepoel (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam kuhusu, Wateja Tigo Pesa kuvuna 6.04bn/- (dola 2,763,636) gawio la kumi la robo mwaka. Kulia ni Meneja Masoko na Usambazaji Huduma za Kifedha wa Tigo, Catherine Rutenge.
Meneja Masoko na Usambazaji Huduma za Kifedha wa Tigo, Catherine Rutenge (kulia), akizungumza katika mkutano huo.

Kampuni inayoongoza kwa mtindo wa maisha ya kidijitali Tigo imetangaza  gawio jingine  la robo mwaka la shilingi bilioni 6.04 (sawa na dola za Marekani 2,763,636)  kwa watumiaji wa Tigo Pesa  ikiwa ni mara ya kumi katika mfululizo wa kampuni hiyo ya simu kugawa faida hiyo kwa watumiaji wake wa huduma ya fedha kwa njia ya simu.

Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam  Mkuu wa Huduma za Fedha kwa njia ya simu wa Tigo Ruan Swanepoel alisema kwa ujumla  kampuni hiyo  imeshawalipa watumiaji wake wa huduma za fedha kwa njia ya simu  jumla ya shilingi bilioni 52.28 (sawa na dola za Marekani 23,763,636) ikiwa ni malipo ya  robo mwaka ya kumi  tangu  kuzinduliwa kwa huduma hiyo Julai 2014.

Hii ni mara ya tatu kwa mwaka huu kwa Tigo  kulipa  gawio kwa wateja wake.

 Swanepoel alisema kuwa katika robo ya tatu ya mwaka huu kiwango cha faida  kilipanda  na kufikia asilimia 9 ikiwa  kimepanda kwa asilimia 1 kutoka robo ya pili  ambako kumechangiwa  kwa kiwango kikubwa na kiwango kizuri cha riba katika mifuko ya dhamana  ndani ya  benki mbalimbali za biashara.


Aidha alidokeza  kuwa ongezeko kubwa katika kiwango cha gawio kumechangiwa na  kuongezeka kwa faida, kuboreshwa kwa mazingira ya soko na kukua kuliko imara kwa  idadi ya watumiaji wa Tigo Pesa kama nyenzo kuu katika ongezeko kubwa la kiwango cha faida  hususani katika  kundi la wafanya biashara. Tigo Pesa  hivi sasa  ina mtandao mkubwa wa wafanya biashara zaidi ya 50,000.

Mwaka 2014 Tigo Tanzania  ilikuwa kampuni ya kwanza ya simu duniani   kugawa faida iliyozalishwa na fedha za simu zilizopo katika Akaunti ya Udhamini kwa kipindi cha robo mwaka kwa wateja wake.


Monday, September 19, 2016

UTARATIBU WA KUTUMIA SIMU ZA MKONONI KUTAMBUA BAJAJI NA BODABODA WAJA

 Image result for bajaji na bodaboda

Simu za mikononi sasa zitatumiwa na abiria wa Bodaboda na Bajaji kwa ajili ya kuboresha sekta ya usafiri huo pamoja na kupunguza vitendo vya uhalifu.

Akizungumza wakati wa kuzindua mkakati huo Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam,Paulo Makonda amesema kuwa endapo itatokea jambo lolote,mtu atakuwa na uwezo wa kutumia simu yake ya mkononi kwa kuingiza namba maalum kama za huduma za kifedha na kwenda katika kipengele cha huduma ya Bodaboda na Bajaji Mkoa wa Dar es salaam,kisha kuingiza namba iliyoko katika sare ya dereva.

Baada ya kuingiza namba hiyo ataweza kupatiwa jina halisi la dereva,namba ya usajili wa pikipiki yake,eneo lake analoegesha,kiongozi wa eneo lake kwa upande wa bodaboda na namba zake za simu pamoja na za kiongozi huyo.

Pia boda boda na madereva wa bajaji mkoani Dar es salaam,watakuwa na sare maalum ambazo watagawiwa bure pamoja na kofia ngumu.

Utaratibu huu utatekelezwa kwa kusajiliwa wamiliki na waendesha bodaboda na bajaji kwa namba maalum zitakazokuwa zimeandikwa katika sare watakazo kuwa wanavaa

Monday, August 8, 2016

UDUKUZI: SIMU MILIONI 900 ZA ANDROID HATARINI.

 Simu ya kisasa ya Android

Upungufu wa usalama wa herufi za siri za takriban simu milioni 900 umewapa wadukuzi fursa ya kudhibiti simu za android kote duniani.

Upungufu huo unaowapa wadukuzi mlango wa nyuma wa kuiga herufi za siri uligunduliwa baada ya watafiti wa hali ya ubora wa programu Checkpoint walipojaribu kusuluhisha hitilafu iliyowezesha kirusi kuambukiza makumi ya mamilioni ya simu zilizokuwa na programu zilizoundwa na kampuni moja ya Marekani Qualcomm.

Kampuni hiyo inayounda programu za simu imeuza programu hiyo kwa watengenezaji wa simu milioni 900.

Aina ya simu zilizoathirika

  • BlackBerry Priv na Dtek50
  • Blackphone 1 na Blackphone 2
  • Google Nexus 5X, Nexus 6 na Nexus 6P
  • HTC One, HTC M9 na HTC 10
  • LG G4, LG G5, na LG V10
  • New Moto X ya Motorola
  • OnePlus One, OnePlus 2 na OnePlus 3
  • Samsung Galaxy S7 na Samsung S7 Edge
  • Sony Xperia Z Ultra

Mkuu wa kampuni hiyo ya kutathmini ubora wa programu katika kampuni ya Checkpoint Michael Shaulov, anasema kuwa
''hakuna ushahidi kuwa tayari simu hizo zimeathirika ila kwa mtizamo wetu ni kuwa mlango uko wazi kabisa mtu yeyote mwenye ufundi na ubora kama wangu hivi anafahamu waziwazi kuwa hakuna hata kizingiti cha kumuibia mtu herufi za siri katika simu hizo tulizotaja hapo juu''
 upungufu unamwezesha mtu wa tatu kumpokonya mmiliki wa simu udhibiti kwani anaweza hata akabadilisha herufi za siri bila yako wewe kujua''

''Ni hatari sana , ni kama mtu amejenga nyumba akaweka mle ndani mali ya thamani ya juu kisha akaondoka akiwa ameacha mlango wake wazi''alisema Shaulov.

Checkpoint tayari imeanza kutoa programu zenye uwezo wa kudhibiti simu hizo na tayari wameipa kampuni ya Qualcomm mbinu za kudhibiti simu hizo.

Njia moja ya kuimarisha usalama wa simu wanasema ni kununua programu kutoka kwa soko maalum la Google Play.

Qualcomm imenyamaza kimya kuhusu ripoti hii iliyotolewa na Checkpoint.
Chanzo:BBC

Wednesday, August 3, 2016

KIPINDI CHA MAISHA NA TEKNOHAMA JUMA HILI-USALAMA MTANDAONI

Thursday, June 16, 2016

MWANZA:KAMATI YA MAWASILIANO MKOA YATOA ELIMU KWA WATUMIAJI WA HUDUMA ZA MAWASILIANO


Mwenyekiti wa Kamati ya Mawasiliano Mkoa wa Mwanza, Jonathan Abdallah Kasibu, akizungumza katika Semina kwa Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano Jijini Mwanza iliyofanyika jana katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Mwanza.
Katika semina hiyo, watumiaji wa hudumza za mawasiliano ikiwemo simu pamoja na vyombo vya habari ambao waliwakilisha makundi mbalimbali kama vile wanahabari, wajasiriamali na walemavu, walipewa elimu juu ya uwepo wa Kamati hiyo pamoja na uwepo wa Baraza la Ushauri la Watumiaji wa huduma za Mawasiliano kutoka Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA-CCC).

Pia walielimishwa juu ya mwongozo wa kuwasilisha malalamiko ya watumiaji wa huduma za mawasiliano, haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za mawasiliano pamoja na sheria ya makosa ya mitandao ya mwaka 2015.

Semina hiyo pia ilihudhuriwa na viongozi wa Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano, kutoka Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA-CCC) ambapo iliambatana na viongozi wa Kamati ya Mawasiliano mkoani Mwanza kujitambulisha kwa baraza hilo.

Watumiaji wa huduma za mawasiliano walielezwa kwamba ni wajibu wao kuwasilisha malalamiko yao ikiwa wanapokea huduma zilizo chini ya kiwango ama ikiwa wana malalamiko ya aina yoyote kuhusu huduma za mawasiliano.

Walihimizwa kuwasilisha malalamiko yao kwa kuanza na mtoa huduma, yasiposhughulikiwa wanawayawasilisha katika Kamati ya Huduma za Mawasiliano mkoa, yasipotatuliwa yatawasilishwa katika Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano kutoka TCRA na hata ngazi nyingine zaidi hadi pale utatuzi utakapofanyika.

Semina hiyo ilionekana kuwafungua ufahamu watumiaji wa huduma za mawasiliano jijini Mwanza kwani baadhi yao walieleza kuwa awali walikuwa hawatambui haki na wajibu wao katika kutumia huduma za mawasiliano.
Baadhi ya Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano Jijini Mwanza, wakiwa katika semina ya kuwaelimisha juu ya Matumizi ya Huduma za Mawasiliano.

Tuesday, May 24, 2016

UfUNGWAJI WA SIMU BANDIA JUNI 16, 2016

Hadi kufikia juni 16 mwaka 2016 , Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) itakua imeshafunga simu nyingi bandia pamoja na vifaa vingine vya mawasiliano ambavyo havikidhi viwango na mahitaji ya soko la tanzania . Kama mtanzania kuna mambo kadhaa unatakiwa kujua kuhusu simu bandia na  vifaa vya mawasiliano

Simu zote na vifaa vyake wakati vinatengenezwa mpaka kupitishwa kutumiwa huwa vinapitia katika taratibu kadhaa zinazohusu ubora na mahitaji ya kibinadamu ambayo hayaleti madhara yoyote kwa afya na mazingira . Simu bandia hazipitii utaratibu huu wala ukaguzi na wala hazijulikani watengenezaji wake wala zilipotoka ili kufuatilia . matokeo yake zinaweza kuleta athari za kiafya na mazingira kama nilivyosema hapo awali .

Kama simu itakuletea madhara ya kiafya ina maana utatumia muda na gharama nyingi kujipatia matibabu yaliyotokana na madhara kadha wa kadha hapo sio kila mtu ana uwezo wa kugharamia au kugharamiwa , kama ulikua umajiajiri basi biashara au mengine yanaweza kufa kwa sababu ya matibabu na mengine lakini ungekua na kifaa kizuri shida hii usingeweza kuipata kwa sababu ingekua na viwango vya kutosha .

Hapo pia kuna suala la kupeleka simu kwa fundi mara kwa mara kwa sababu ya ubovu au mengine ambayo simu haiwezi kufanya kutokana na viwango vyake havifu kwa mwananchi wa kawaida hii pigo kwake , wengine wanaweza kuamua kununua nyingine tu maana gharama zake pia ni nafuu kulinganisha na zile halisi zenye vitu vinavyolingana .

Simu bandia na vifaa vyake huingizwa nchini kupitia njia za panya maana kama zikikaguliwa zitagundulika na kuharibiwa na wahusika kufikishwa katika vyombo vya sheria , hii ina maana serikali ina kosa mapato kutokana na kodi , ajira zinapungua na huduma nyingine zinakosekana kutokana na hujuma kama hii .

Kumbuka kwamba wauzaji wote wa vifaa vya mawasiliano kama simu husajiliwa TCRA ambapo ada yake kwa mwaka ni laki 5 kwahiyo huwa na kibali Fulani , kama mtu hana kibali cha kuuza vifaa hivi maana yake unatakiwa kuwa na mashaka nae ni vizuri ukafikisha taarifa kwa mamlaka ya mawasiliano haraka ili hatua kuchukuliwa .

Kiusalama wa kawaida pia matumizi ya simu bandia na vifaa vyake yanaweza kuleta mambo mengi mfano ni suala la wizi wa mtandao kwa kuwa simu inakua haina mfumo mzuri na wa uhakika wa kujilinda na kwa hizi za kisasa hata antivirus na nyingine hautaweza kuweka , mhalifu anaweza kuingilia kwa urahisi hata kutokea maeneo mengine .

Kuna tukio lilitokea Saudi Arabia mwaka jana ambapo gaidi alifanikiwa kuingia katika kambi ya polisi akajitoa mhanga na kuua wengine 30 . katika tukio hili iligundulika kwamba gaidi huyu na mtandao wake walikua wanatumia simu bandia na kujisajili line kutumia majina ambayo sio yao na matokeo yake ni kufanikiwa kupita vizuizi vyote mpaka eneo nyeti la kambi ya polisi .

Kuanzia tukio hilo Serikali ya Saudi Arabia ilitoa tangazo la kufungwa wauzaji wote wa simu bandia na laini zisizosajiliwa .
Tukio kama la Saudi Arabia linaweza kutokea hata Tanzania na maeneo mengine mengi kama matumizi ya simu bandia na vifaa vyake yakiendelea bila kikomo .

Mwanzo wa Mwaka 2016 , Benki moja maarufu ilitaka kuibiwa milioni 900 kwa njia ya mtandao baada ya kununua kifaa bandia cha mawasiliano ya kiofisi , wahalifu walitumia kifaa hiko kuingilia akaunti za benki ili kuhamisha fedha ila kuna vitu walikwama na miongoni ni ujuzi wao katika matumizi ya Lugha lakini suala ni ununuzi wa kifaa bandia cha mawasiliano .

Pia suala la Ushindani wa kibiashara na Ubinifu hupotea na kufa kabisa katika maeneo ambayo biashara za vitu bandia hushamiri , mtu mwenye simu bandia ya Nokia 200 kwa mfano atauza shilingi 4 wakati ile halisi ni 8 hii ina maana baada ya muda mfupi Yule wa 8 anaweza kufunga biashara yake na kufuta wafanyakazi waliobuni kifaa husika , kukijaribu , kukitafutia masoko na mengine mengi . sasa muwekezaji hatapenda kuwekeza Tanzania akijua kuna soko kubwa la vitu bandia .

Kama unafanya kazi zako kutumia simu , ukiwa na simu bandia utaweza kuona ubora  wa picha , sauti , cover , kioo na vitu vingine unavyokua mbaya kulinganisha na vile vilivyoko katika simu original yenye ubora wa uhakika . kwahiyo utaweza kukosa kazi kwa kuharibu kazi kwa kutumia vifaa bandia visivyokidhi mahitaji .

Suala la vitu bandia liko katika vitu vingi tu ambavyo tunajua madhara yake kama spea za magari ambazo huchangia katika ajali za mara kwa mara , vifaa vya ujenzi ambavyo huchangia majengo kuporomoka au kuwaka moto .

Vita dhidi ya vifaa bandia viko dunia nzima , sio Tanzania tu , kwahiyo tuunge mkono jitihada hizi za serikali chini ya TCRA , POLISI , TBS na mamlaka nyingine zenye uwezo huo kisheria ili kulinda nchi na watu wake .

Mwandishi wa makala hii hana uhusiano na kampuni yoyote ya simu wala mamlaka ya mawasiliano tanzania . Ulichomaliza kusoma ni kwa ajili ya kujifunza ili kuelimika kisha usaidie wengine .
YONA FARES MARO
0786 806028

Sunday, April 24, 2016

WIZARA YA UJENZI ,UCHUKUZI NA MAWASILIANO YAENDELEA NA MCHAKATO WA UKUSANYAJI MAONI JUU YA UBORESHAJI SERA YA TAIFA YA (TEHAMA)MKOANI MBEYA


Mkurugenzi Msaidizi anayeshughulikia masuala ya Simu katika Wizara ya Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano Ndugu John Mwera akizungumza na wanahabari katika viwanja vya Chuo Cha Uhasibu jijini Mbeya( TIA ) juu ya zoezi la uchukuaji maoni na ushauri kwa wadau katika kuboresha sera ya Taifa ya Habari ,Teknologia na Mawasiliano (TEHAMA).

Mhandisi  Enock Mpenzwa Idara  Mawasiliano  toka Wizara ya Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Forest jijini Mbeya waliofika kwa ajili ya zoezi la utoaji maoni na ushauri juu ya uboreshaji wa sera mpya ya Taifa ya TEHAMA katika viwanja vya Chuo Cha Uhasibu TIA jijini Mbeya April 22 ,2015.

Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Forest jijini Mbeya wakiwa katika foleni ya kujiandikisha ili kutoa maoni yao na ushauri juu ya uboreshaji wa sera ya Taifa ya TEHAMA,zoezi ambalo limefanyika katika viwanja vya Chuo Cha Uhasibu Mbeya (TIA) April 22 ,2015.

Mwanafunzi shule ya sekondari Forest jijini Mbeya Mariam Jordan akijiandikisha kwa ajili ya kutoa maoni yake katika zoezi la uboreshaji wa sera ya Taifa ya TEHAMA zoezi ambalo limeratibiwa na Wizara ya Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano ,katika viwanja vya Chuo Cha Uhasibu Jijini Mbeya( TIA)

Baadhi ya wanafunzi wa Chuo Cha Uhasibu Jijini (TIA)wakijibu baadhi ya Maswali kama sehemu ya ukusanyaji maoni ili kuboresha sera ya TEHAMA .



Baadhi ya wanafunzi wa Chuo Cha Uhasibu Jijini (TIA) na wadau mbalimbali kutoka Mkoani Mbeya wakijibu baadhi ya Maswali kama sehemu ya ukusanyaji maoni ili kuboresha sera ya TEHAMA .


Wizara ya Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano nchini Tanzania  imetoa wito kwa wananchi na wadau mbalimbali kuendelea kutoa maoni na mapendekezo ili yatumike kuboresha Sera mpya ya Taifa ya Habari  Teknologia ya Mawasiliano(TEHAMA) ya (2016) ili kuisaidia serikali kutatua changamoto za upatikanaji wa habari na mawasiliano katika jamii
Wito huo umetolewa jijini Mbeya  na Mkurugenzi Msaidizi anayeshughulikia maswala ya simu katika Wizara ya Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano Ndugu John Mwera wakati wa zoezi la uchukuaji maoni lililofanyika katika viwanja vya chuo cha Uhasibu (TIA) jijini Mbeya .
Amesema Teknolojia ya habari na mawasiliano hapa nchini imekuwa ikikua kwa kasi kubwa katika kipindi cha miaka kumi tangu serikali ilipotunga sera kwa mara ya kwanza mwaka 2003.
  Amesema hali hiyo imechangia kuwepo kwa miundombinu ya huduma za mawasiliano   kila mahala  na kufanya matumizi kuwa makubwa ambapo zaidi ya watu milioni 39 wanatumia mawasiliano ya simu hivyo kufanya kuibuka kwa changamoto mbalimbali katika sekta hiyo.
Amesema ili kufahamu changamoto wanazo kutananazo wananchi pamoja na mtizamo wao  katika utumiaji wa mawasiliano,  wizara hiyo imeamua kuweka utaratibu wa kuweka vituo vya kukuza ubunifu katika jamii katika kila mkoa ambapo kila mwananchi anakuwa huru katika kutoa maoni yao na ushauri ili kuisaidia serikali katika kupanga mikakati ya kuweza kuzitatua changomoto hizo. 
Huwezi kukaa ofisini ukatunga sera ambazo haziwahusu mwananchi wa kawaida hivyo lazima twende  kwa wananchi na kujua wanahitaji nini ili kutunga sera na kuweza kuzitatuaAlisema Mwela .
Aidha amesema kuwa kila maoni yanayotolewa na wananchi serikali inayathamini katika kuweza kutoa muelekeo wa sekta ya mawasiliano kwani sekta hiyo bado inamchango mkubwa sana katika kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi.
Hata hivyo amesema bado wizara inakabiliwa na changamoto mbalimbali  ikiwa ni elimu ndogo kwa waanchi juu ya utunzaji wa miundombinu ya sekta ya mawasiliano hususani mkongo wa taifa sanjali na wizi wa mafuta kwenye minara ya simu hivyo amewataka wananchi kuwa walinzi wa miundombinu hiyo ili kuendelea kukuza sekta hiyo sanjali na kulahisisha upatikanaji wa huduma kwa jamii.
Amesema zoezi hilo la uchukuaji maoni kwa wananchi juu ya uboreshaji wa sera ya TEHAMA itaendelea inchi nzima katika mikoa yote ya Tanzania bara na Visiwani.

Popular Posts

Labels