Thursday, December 31, 2015

USICHOFAHAMU KUHUSU WHATSAPP HIKI HAPA

 Whatsapp-1
Screen Shot 2015-12-31 at 12.25.45 PM
Maeneo yaliyopata matatizo ya WhatsApp kutofanyakazi kwa mujibu wa DownDetector
Mtandao wa kijamii wa WhatsApp ulipata mushikeli kwa muda wa masaa kadhaa jana Alhamisi Desemba 31,2015 muda mfupi kabla ya kuingia mwaka mpya hali ambayo ilisababisha watumiaji wa mtandao huo sehemu mbalimbali duniani kushindwa kutuma na kupokea ujumbe wa Kheri ya Mwaka Mpya kama ilivyotarajiwa.

Kwa mujibu wa account ya twitter inayoonesha mwenendo wa WhatsApp umeonesha kuwa tatizo la jana lilishatokea katika nyakati tofauti tofauti ambazo ni Nov 8,2011,Des 1,5,2011,Machi 11,2012,Mei 8,2012,Agosti 29,2012,Oktoba 15 2013 na Feb 22,2014.

Kwa mujibu wa tovuti ya DownDetector, ambayo hujihusisha na kufuatilia matatizo yanayotokea kwenye mitandao imelezwa kuwa tatizo hilo lilionekana hasa katika nchi za Uingereza na Ujerumani huku ikielezwa kuwa tatizo hilo halikuwa kubwa nchini Marekani.

Jumla ya watu milioni 900 duniani wamejiunga na mtandao huo ambao unatumika katika simu za mikononi zenye mifumo endeshi ya iOS na Android huku kukiwa na utumaji wa ujumbe bilioni 10 kila siku.




SERIKALI YAPIGA MARUFUKU MATUMIZI YA BARUA PEPE ZA KAWAIDA KATIKA MAWASILIANO YAKE



Waziri Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (kushoto) akipokelewa na Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Serikali Mtandao Dkt. Bakari Jabiri leo alipofanya ziara ya kikazi katika Ofisi za Wakala hiyo jijini Dar es salaam. 
Waziri Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (katikati) akiwasili Ofisi za Wakala ya Serikali Mtandao kwa ziara ya kikazi leo jijini Dar es salaam.
Waziri Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (kulia) akitembelea maeneo mbalimbali ya Ofisi za Wakala ya Serikali Mtandao leo. Kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Serikali Mtandao Dkt. Bakari Jabiri leo alipofanya ziara ya kikazi katika Ofisi za Wakala hiyo jijini Dar es salaam. 
Mkurugenzi wa Uratibu wa Miundombinu ya TEHAMA wa Wakala ya Serikali Mtandao Bw. Benjamin Dotto akitoa ufafanuzi kwa Waziri Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (kulia) kuhusu kituo cha ufuatiliaji mifumo ya mawasiliano Serikalini leo jijini Dar es salaam. 



Waziri Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki akizungumza na Watendaji na baadhi ya Wafanyakazi wa Wakala ya Serikali Mtandao leo alipofanya ziara ya kikazi katika Ofisi za Wakala hiyo jijini Dar es salaam. 
 
Serikali imepiga marufuku matumizi ya Barua pepe za kawaida kwa watumishi wa umma wanaotuma au kupokea taarifa za Serikali na kuwataka watumishi hao kuhakikisha kuwa wanatumia mfumo rasmi wa Mawasiliano ya Barua Pepe Serikalini (GMS) ulioanzishwa na Serikali kwa lengo la kuimarisha mawasiliano kwa njia ya Mtandao. 

  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe.Angella Kairuki ametoa agizo hilo alipokuwa akizungumza na Watendaji na Watumishi wa Wakala ya Serikali Mtandao ( e Government Agency) wakati wa ziara yake ya kukagua utendaji na ufanisi wa matumizi ya TEHAMA Serikalini. 

  Ameeleza kuwa kuna watumishi 7000 wanaotumia anwani za Barua pepe za Serikali ,idadi ambayo ni ndogo lazima iongezeke, hivyo serikali haiwezi kuendelea kuruhusu utumaji wa taarifa za Serikali kwa kutumia Barua Pepe nje ya mfumo huo huku akifafanua kuwa Serikali haijakataza matumizi ya barua pepe za kawaida kwenye mawasiliano binafsi. 

Amesema kwa kutambua umuhimu wa uimarishaji wa mawasiliano ya TEKINOHAMA Serikalini na kuongezeka kwa matumizi ya TEKINOHAMA katika utumaji wa taarifa kupitia mitandao mbalimbali ipo haja ya kuweka msisitizo kwa watumishi wa umma kutumia Barua Pepe za Serikali. 

Mhe. Kairuki amewataka watendaji wa Wakala hiyo kuhakikisha kuwa wanasimamia uratibu wa zoezi hilo ili kuhakikisha kuwa Wizara, Idara na Taasisi zote za umma zinaunganishwa na mfumo rasmi wa Serikali ili kuwa na mfumo mmoja wa Mawasiliano huku akitoa siku 60 kukamilika kwa zoezi hilo katika taasisi zingine.


Thursday, December 24, 2015

TTCL YAZINDUA TEKNOLOJIA YA 4G LTE

 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura (kushoto) na Ofisa Ufundi (IT) wa kampuni hiyo, Rehema Maswanya (kulia) kwa pamoja wakifungua pazia kuashiria uzinduzi wa teknolojia ya 4G LTE iliyozinduliwa leo jijini Dar es Salaam.

 
Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL) imezinduwa mtandao unaotumia teknolojia ya 4G LTE unaoanza kutoa huduma jijini Dar es Salaam. Mtandao huo wenye teknolojia mpya na ya kisasa wenye kasi kubwa utatoa huduma katika maeneo 11 ambayo ni pamoja na Uwanja wa Ndege wa Mwalimu J.K. Nyerere, Pugu Road, Posta Mpya, Upanga, Kinondoni, Ubungo, Oysterbay, Mwenge, Mbezi Tangibovu, Mbezi Exchange, Kunduchi Salasala, na Wazi Tegeta.

Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati akizinduwa rasmi teknolojia hiyo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk. Kamugisha Kazaura alisema licha ya kuzinduwa huduma hiyo katika maeneo 11 kwa sasa mafundi wa kampuni hiyo wapo kazini wakiendelea na awamu ya pili ya kufunga mitambo ili huduma hiyo itolewe pia katika maeneo mengine 14 ya jiji la Dar es Salaam.

Aliyataja maeneo mengine ambayo mitambo inaendelea kufungwa kwa sasa kuwa ni pamoja na Kigamboni, Masaki, Temeke, Kimara, Jangwani, Kariakoo, Chuo Kikuu, Kurasini, Mbezi Chini Gongo la Mboto, Tabata, Kibamba, Kongowe na Bunju.

Tuesday, December 8, 2015

POLISI ARUSHA KUTUMIA WHATSAPP KUDHIBITI UHALIFU


 Image result for whatsapp

Jeshi la Polisi mkoani Arusha na Kampuni za Ulinzi wameweka mkakati wa kushirikiana katika kupeana taarifa za uhalifu kwa kutumia mtandao wa kijamii wa WhatsApp.

Mpango huo umetangazwa na Mkuu wa Operation wa Jeshi la Polisi Arusha Edward Balele ambapo amesema awali taarifa zilikuwa zikiwafikia walengwa kwa mtindo wa ujumbe mfupi (SMS) lakini kwa kutumia mfumo wa kikundi cha WhatsApp ambacho kitapewa jina maalum,taasisi hizo zitakuwa zinapata na kutoa taarifa kwa pamoja ambapo kila mhusika atakuwa anachingia mawazo yake huku wanawachama wengine wa kikundi hicho wakiona maoni ama ushauri wa kila mchangiaji.


JWTZ YATOA ONYO KWA WANAOPIGA PICHA NA KUZISAMBAZA KWENYE MITADAO YA KIJAMII


Mkurugenzi wa Habari  na Uhusiano  wa Jeshi la
Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa JWTZ-Kanali Ngemela Lubingo (Chanzo:Mwananchi)

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limetoa onyo kwa wananchi kutojihusisha na upigaji picha wa vifaa vya kijeshi na kuvisambaza katika mitandao ya kijamii.

Hatua hiyo inakuja kutokana na tukio la  Desemba 3,saa 1:15 jioni ambapo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius JK Nyerere jijini Dar es salaam wafanyakazi wa Shirika la kupokea mizigo la Swiss Port wakishirikiana na wale wa shirika la Ndege la Uholanzi (KLM) kupiga picha vifaa vya kijeshi na kuvisambaza katika mitandao ya kijamii

Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa JWTZ Kanali Ngemela Lubingo amewaambia Waandishi wa Habari jijini Dar es salaamu kuwa jeshi hilo limesikitishwa na  tukio hilo la watu kujichukulia maamuzi ya kupiga picha kitu ambacho hakikuwahusu na kusambaza picha kwenye mitandao ya kijamii na kusababisha kujitokeza kwa maoni ya kupotosha jamii


Friday, December 4, 2015

WAHALIFU MTANDAO WATIKISA ANGA YA WANAUSALAMA MITANDAO

Wakati bado mafanikio mbali mbali yakijadiliwa wahalifu mtandao wamegundulika kuja na uhalifu unaotafsiriwa kuwa ni wa kihistoria na uliofanyika kwa ubunifu na umahiri wa hali ya juu ambapo wahalifu mtandao wamefanikiwa kusambaza kirusi aina ya ModPOS kinacho athiri mashine zinazotumika kukamilisha miamala wakati wa manunuzi.
 
Kirusi cha ModPOS, kimegundulika Nchini Marekani wakati wa sherehe za “Thanks Giving” ambapo watu wengi hufanya manunuzi. Kirusi hicho Kimekua kikifanikisha upotevu mkubwa wa pesa wakati wa miamala.

Mara baada ya ugunduzi huo wa ModPOS, mijadala kupitia mtandao ilianza baina ya wanausalama mitandao ili kuweza kufanikisha mambo makubwa matatu. Moja ni kuweza kugundua chanzo na jinsi ilivyo fanikishwa kuwepo bila kugundulika (Inaaminika kimedumu muda – Taarifa ambazo bado zinafatiliwa) Pili, Ilikua ni kutafuta suluhu ya kirusi hicho ili kiweze kuondolewa na Tatu, ni kupanga namna ya kukuza uelewa wa namna ya kujikinga na janga hili la ModPOS.

Hadi sasa bado hapajapatikana suluhu na inahofiwa huwenda kutokana na sherehe za mwisho wa mwaka kirusi hicho kusambaa maeneo mengine huku mataifa yakitakiwa kuchukua tahadhari. Inakadiriwa kama kitaendelea kutopatiwa suluhu; pesa nyingi zitaishia mikononi mwa wahalifu mtandao na hasara itakayopatikana ni kubwa zaidi kupata kutokea.

Wakati hayo yakiendelea kuwa ni mjadala wa vuta nikuvute. Wahalifu wakadukua Kampuni ya VTech inayotengeneza midoli ya watoto ya kielektroniki kutumia TEKINOHAMA ambapo walifanikiwa kuiba taarifa zaidi ya milioni tano ikiwa ni pamoja na Picha za watoto, Mawasilianao ya watoto na wazazi wao, Sauti za watoto, na taarifa za miamala wakati wa manunuzi.

Inaaminika kutokana na umakini mkubwa wanausalama mtandao wamekua wakiweka juu ya kuwalinda watoto wawapo mtandaoni kitu ambacho kimepelekea kua na program ya kidunia maarufu kama “Child Online Protection – COP” yenye dhamira ya kuhakiki watoto wanabaki salama watumiapo TEKINOHAMA/ Mitandao, Wahalifu walitumia udukuzi wa VTech ili kuhamisha mawazo ya kukabiliana na ModPOS na badala yake nguvu kubwa ihamie kwenye udukuzi VTech.

Kufuatia udukuzi huo kwenye kampuni ya VTech wanausalama mtandao walishauri Kampuni hiyo kusitisha huduma zake za mtandao mara moja na kuendelea kutafuta suluhu ya tatizo. Huku kampuni hiyo ikitakiwa kuhakiki taarifa zilizo dukuliwa hazipatikani/ kusambwazwa mitandaoni. Kampuni ya VTech tayari imechukua uamuzi wa kusitisha huduma zake mtandao.

Hayo yakijiri, Nchini Kenya nako wameshatoa Ripoti/taarifa za mwaka kuhusiana na uhalifu mtandao ambapo uhalifu mtandao umeonekana kukua zaidi. Taarifa ilifafanua uhaifu mtando umebadili taswira na kuwa si tu wa kudukua maneno ya siri bali ni taarifa zinazoweza kupelekea mabilioni ya dola kuishia kwa wahalifu mtandao. Jitihada za dhati zimeendelea nchini Kenya ili kukabiliana na uhalifu huu mtandao.

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Tanzania nayo haijabaki salama, Baada ya uhalifu mtandao maarufu kwajina la “vikoba” ulioshika kasi kipindi kifupi cha nyuma uliosababisha waathirika kuibiwa fedha zao na wahalifu mtandao. Baadae elimu juu ya uhalifu huo ilisambaa na hatimae kupungua sasa wahalifu mtandao wamekuja na aina mpya ya uhalifu mtandao wenye dhamira ya kuiba taarifa za watu baada ya kufanikiwa kutengeneza program yenye kuwashawishi watu kuingiza taarifa za wengine kwa madhumuni ya kudukua taarifa za watu binafsi.Ikumbukwe hili ni kosa na lazima wananchi wawe makini kwenye hili.

Aidha, wahalifu matandao wajakomea hapo, Kwa mujibu wa taarifa ya kampuni ya kiusalama mtandao ya “Symantec” imefanikiwa kugundua mbinu ambayo wahalifu mtandao wamekua wakitumia mtandao wa kijamii wa “LinkedIn” ambapo wahalifu wamekua waki dhamiria zaidi kuiba taarifa zinazopatikana kwenye mtandao huo baada ya kuweka ukaribu na watumiaji mtandao huo kwa kuwaomba urafiki na baadae kutumia taarifa zilizopo huko kufanya udukuzi.

Hili tayari Symantec kwa kushirikiana na LinkedIn imeanza opareheni funga akounti zozote zinazobainika kuwa ni za wahalifu mtandao na tunategemea kupata taarifa yake kamili hapo baadae.

Matukio hayo na mengine yanayowea kujitokeza watai tunaelekea mwisho wa mwaka ushauri mkubwa umeendelea kutolewa ku kuhakiki panakua na mpango endelevu wa kukuza uelewa wa matumizi salama ya mitandao (Cybersecurity awareness).

Pamoja na hilo mataifa yana aswa kua na tabia ya kuhakiki yanatambua kwa ukaribu sana viashiria vyovyote vya kihalifu mtandao ili kuweza kuweka mataifa yao salama kimtandao. Zaidi ni pamoja na kukuza nguvu kazi watu kwenye sekta ya usalama mtandao pamoja  na kua na matumizi ya watu sahihi katika kukabiliana na uhalifu mtandao.


Natoa wito wa kutambua uhalifu mtandao upo na una madhara makubwa katika sekta zote kuanzia Kiuchumi, Kijamii, Kisiasa, nakadhaika endapo hatua kuanzia ngazi ya mtu binafsi hazitachukuliwa ili kuhakiki pana patikana usalama katika mitandao. Tujenge tabia yay a kutafakari kabla ya kutumia mitandao ili kuhakiki hatusababishi madhara kwa kuanzia kwa mtu binafsi pamoja na kwa wengine.

Na:Yusuph Kileo

Wednesday, November 25, 2015

VIKAO KAZI KWA WATENDAJI WA UMMA NCHINI TANZANIA SASA KUFANYIKA KWA KUTUMIA TEKNOHAMA



 

Serikali ya Tanzania  kupitia Menejimenti ya Utumishi wa Umma Ofisi ya Rais imesema haitagharamia gharama zozote za kuendesha vikao kazi na watendaji wake kuanzia sasa, badala yake vikao hivyo vitaendeshwa kwa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEKINOHAMA). 

Wahusika wakuu wa vikao kazi hivyo ni pamoja na Wakurugenzi, Makatibu Tawala wa Mikoa na Maafisa Utumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Florence Temba, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, amesema kuwa, kupitia utaratibu huo washiriki wa vikao hivyo watabaki katika maeneo ya kazi ambapo wataunganishwa na mtandao wa pamoja kwa mfumo wa kuonana na kuongea uso kwa uso.

Aidha amewatoa hofu watumishi Kuhusu miondombinu ya mawasiliano kwa kusema Mfumo huo ni salama hakuna haja ya kuhofia kuhusu kukatika kwa umeme au hali ya hewa kwani mpango huo unaratibiwa na serikali hivyo ikitokea hali kama hiyo kutakuwepo na umeme wa ziada au kwa kutumia mkongo wa Taifa wa mawasiliano.

Monday, November 16, 2015

WANAFUNZI WA VYUO KUFURAHIA HUDUMA YA KUPIGIANA SIMU BURE TOKA TIGO

Meneja Mauzo wa mkoa wa Tanga kutoka Tigo Bw.Daniel Mainoya akiongea na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali , kuhusu uzinduzi wa kifurushi kilichoboreshwa cha University Pack kutoka Tigo katika Uwanja wa chuo cha Utumishi wa Umma, Kange, mjini Tanga.
Mwanafunzi kutoka chuo cha Utumishi wa Umma, Kange,mjini Tanga, Bi.Stella Mwakiliku akiongea na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali  kuhusu vipi wanafunzi wamekikubali kifurushi hicho kilichoboreshwa cha University Pack kutoka Tigo.

  1. Mwanafunzi kutoka chuo cha Utumishi wa Umma, Kange, Bw.Albert Risala akiongea na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali kuhusu vipi wanafunzi wamekipokea kifurushi hicho kilichoboreshwa cha University Pack kutoka Tigo.
      Kikundi cha sarakasi  kikitumbuiza wanafunzi  katika uzinduzi wa kifurushi cha University pack kilichoboreshwa katika uwanja wa chuo cha Utumishi wa Umma,Kange, mjini Tanga.
Msanii wa kizazi kipya Roma Mkatoliki akiwatumbuiza wanafunzi wa chuo cha Utumishi wa Umma,Kange, mjini Tanga,katika uzinduzi wa kifurushi cha University pack kutoka Tigo kilichoboreshwa.


 Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo imezindua kifurushi maalum kinacho wawezesha wanafunzi, ambao ni wateja wa Tigo, kuweza kupigiana simu bure.

Huduma hii imeboreshwa zaidi baada ya kifurushi hicho kwa jina maarufu kama Tigo Uni Pack kuzinduliwa mwaka jana, ukilinganisha na kifurushi cha zamani, kifurushi hichi kipya cha wiki kitawapatia wanafunzi wepesi wa kujiunga wakiwa popote ndani ya nchi, hii ni kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari na kampuni ya Tigo leo.

Kinachohitajika ili wanafunzi waweze kutumia huduma hii,ni kuhakiki kwamba wamesajiliwa kama wateja wa Tigo katika Vyou vyao, ujumbe huo ulisema.

Akizungumzia kifurushi hicho kilichoboreshwa, Meneja wa Bidhaa kutoka Tigo Edwin Mgoa,alisema kifurushi hicho cha Uni Pack, kinadhirisha vipi Tigo inavyowasaidia wanafunzi kwa ajili ya kuwawezesha kuweza kupata huduma za mtandao za maisha ya kidijitali.

Baadhi ya huduma za kidijitali zinazotelewa na Tigo ni upatikanaji wa muziki bila kikomo kwa kupitia huduma ya Tigo Music, Facebook ya Kiswahili, Tigo Pesa App, Tigo Backup- huduma inayowawezesha wateja wa Tigo kuweza kurudisha simu na  zinapoibiwa au kupotea.

Kujisajili kwa kifurushi cha Uni Pack, mwanafunzi atahitajika kupiga *148*01*20#, namba ambazo kwa mujibu wa taarifa hiyo, imejumuisha vifurushi vingine muruwa kutoka Tigo.

VODACOM YAPELEKA SOMO LA ICT SHULE ZA SEKONDARI VIJIJINI


Baadhi ya Kompyuta zilizotolewa na Kampuni ya Vodacom kama msaada wa shule ya sekondari ya Shimbwe iliyopo wilayani Moshi vijijini.
Mkuu wa Vodacom kanda ya Kaskazini ,Henry Tzamburakisi akizungumza jambo na mkuu wa shule ya sekondari Shimbwe,Jacob Costantine alipotembelea darasa la Kompyuta shuleni hapo.
Mmoja wa wafanyakazi wa shirika lisilo la kiserikali la Learning Insync  akijaribu kuunganisha nyaya katika darasa la kompyuta lilopo shule ya sekondari Shimbwe iliyopo Uru wilaya ya Moshi vijijini.
Mkuu wa Vodacom kanda ya Kaskazini,Henry Tzamburakisi (kushoto) akiwa katika darasa la Kompyuta katika shule ya Shimbwe Sekondari ,wengine ni baadhi ya walimu katika shule hiyo ambao wamepatiwa mafunzo ya kompyuta.
Lisa Wolker akitoa maelekezo kwa walimu na wanafunzi.
Walimu na wanafunzi katika shule hiyo wakisikiliza kwa makini.
Mafunzo juu ya matumizi ya Programu maalumu ya kufundishia na kujifunzia yakiendelea katika darasa la Kompyuta katika shule ya sekondari ya Shimbwe.
Mkuu wa Vodacom Kanda ya Kaskazini Tzamburakisi akielekeza jambo kwa wanafunzi.
Jumla ya Kompyuta 30 zimetolewa na Vodacom kupitia mfuko wa Vodacom Foundation kwa shule ya sekondari Shimbwe ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa wataalamu wanao toa mafunzo ya matumizi ya Programu maalumu za kufundishia katika shule hiyo.

Wednesday, November 4, 2015

ALICHOANDIKA RAILA ODINGA MASAA SABA YALIYOPITA KWENYE TWITTER NA FACEBOOK KUHUSU RAIS MSTAAFU BENJAMINI MKAPA



SERIKALI YA TANZANIA YAKANUSHA TAARIFA ZA UZUSHI KUHUSU RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA



Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Assah Mwambene amekanusha taarifa zinazosambaa katika mitandao ya kijamii kuhusu Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa kuwa amefariki Dunia. 

Akizungunza na waandishi wa habari Hii leo katika ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es Salaam, Mwambene amesema Rais Mkapa yupo salama na mzima wa afya na hakuna maradhi yoyote yanayomsumbua.

Mwambene amewaasa watumiaji wa mitandao mbalimbali hasa Blogs kuacha kuitumia mitandao hiyo kwa kupotosha umma na kuandika mambo yasiyo na ukweli ili kuepusha mifumuko ya habari za upotishaji.

Aidha amesema Serikali italishughulikia hili na tayari imeshaanza kukamata baadhi ya watu mbalimbali ambao wanatoa taarifa za uongo zinazopelekea umma kupotoka.

Amesema kuwa vyombo vya habari vifanye kazi kwa uweredi ili kazi ya uandishi wao iwe ya usawa na kufuata misingi ya uandishi, jambo ambalo wengi hukiuka kutokana kutofuata weredi wa kazi zao.

Popular Posts

Labels