Saturday, March 29, 2014

VIDEO:KUJILINDA NA UHARIFU WA KIMTANDAO

Thursday, March 27, 2014

TCRA YAWATOA WASIWASI WAKAZI WA TABORA NA SINGIDA KUHUSU MATANGAZO YA KIDIGITALI

Mamlaka ya mawasiliano nchini Tanzania TCRA Imewataka wananchi wa mikoa ya Tabora na Singida kuepukana na dhana potofu ya matumizi ya televisheni walizonazo kuwa hazitumiki katika matangazo ya kidijiti bali waendelee na televisheni zao kwani king’amuzi hakina luninga maalum.

Hayo yamebainishwa na Naibu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano na Utangazaji nchini Tanzania Bwana Fredrick Ntobi wakati akitoa taarifa ya kuzima mitambo ya analojia ifikapo tarehe 31 machi mwaka huu itakayohusisha maeneo ya mikoa hiyo.


Ntobi amesema kuwa utaratibu wa kuzima mitambo ya analojia utakuwa kwenye mitambo ya maeneo ya dijitali ambapo watoa huduma za kusambaza ving’amuzi walioko Tabora kuhakikisha kuwa kuna ving’amuzi vya kutosha.


Aidha wananchi wa mkoa Tabora wasizitupe tv zao za analojia bali wanunue ving’amuzi ili kupata matangazo ya kidijitali.


Hata hivyo wakizungumza na vyombo vya habari baadhi ya wananchi wa mkoa wa Tabora wameonesha wasiwasi wao kuhusu mfumo mpya wa kidijitali wa upataji wa matangazo ya televisheni kwa kuwa watu wengi bado hawajanunua ving’amuzi na ambao wamenunua wanalamika kuwa baadhi ya chaneli hawazipati.

 

Tuesday, March 18, 2014

CIA WANAFUATILIA TWEETS MILIONI 5 KWA SIKU



Shirika la kijasusi la Marekani,CIA,Kwa Mara nyingine limeripotiwa kufuatilia mitandao ya kijamii na kwamba kila siku mawakala wake wanasoma ujumbe milioni tano unaotumwa kwenye mtandao wa twitter tu.

Imekuwa ikiripotiwa kuwa Marekani ina utaratibu maalum wa kufuatilia Mawasiliano kutoka kwenye mitandao mbalimbali ya kwenye internet ,mbali na yale ya simu.

Shirika la Habari la AP,liliwahi kulipoti kuwa kati ya watumiaji  zaidi ya milioni 800 wa facebook na twitter ,taarifa milioni 400 zinazotumwa kwenye mitandano hiyo zinafanyiwa kazi na timu ya ufuatilia ya CIA.

Inaelezwa kuwa tweets hizo huwasaidia kufuatilia taarifa za kufahamu ‘mood’za watu katika jambo fulani na hivyo kutoa picha ya kinachoendelea kwa ikulu ya White House.
Lakini pia CIA wanatajwa kuitumia mitandao hiyo hiyo kwa ajili ya kupima upepo katika jambo fulani ,ili kubaini mwitikio wa watu wakoje.

Mfano unaotolewa katika hilo ni hatua yake ya kusambaza kwenye mitandao hiyo ya kijamii picha ya kuuawa kwa Osama bin Laden.

Mtandao wa kijamii wa twitter ambao ni miongoni mwa mitandao 10 maarufu duniani ulioanzishwa na Jack Dorsey ndio unaoonekana kutumiwa na watu wazima hasa maarufu duniani.

Tovuti ta statistic brain Twitter katika takwimu zake za januari mosi mwaka 2014 zinaonesha kuwa ulikuwa na watumiaji karibu milioni 646 na hadi kufikia mwaka 2013 ulikuwa umepata dola za kimarekani milioni 405 kutokana na matangazo ya biashara.

TCRA YASEMA WANANCHI WENGI HAWANA UELEWA WA HAKI ZAO KATIKA HUDUMA ZA MAWASILIANO

Imeelezwa kuwa wananachi wengi bado hawana uelewa wa kutosha juu ya haki zao za msingi katika huduma za mawasiliano wanazotumia, hali ambayo imekuwa ikisababisha wengi wao kuendelea kudhulumiwa haki zao bila kujijua.

Hayo yameelezwa hivi karibuni na Naibu Mkurugenzi Mratibu wa ofisi za Kanda Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA),Victor Nkya wakati akizungumza kwenye mkutano uliowashirikisha waalimu katika chuo cha ualimu Monduli katika kuadhimisha siku ya walaji duniani.


Bw Nkya amesema kuwa,bado uelewa ni mdogo sana kwa watumiaji juu ya haki zao katika matumizi ya mawasiliano , hivyo elimu zaidi iendelee kutolewa kwa watumiaji ili waweze kuzijua haki zao na kuweza kuzidai pale wanapokuwa wameonewa.


Naye Meneja wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) kanda ya kaskazini , Annet Matindi amesema kuwa, watumiaji wa mawasiliano wanapaswa kuelewa haki zao za msingi na kuzidai haraka endapo wanahisi kuonewa kama vile kupata bili tofauti na matumizi yao ya mawasiliano wanayotumia na endapo hawataridhika wana haki pia ya kukata rufaa kuidai haki hiyo.


Matindi amesema kuwa,wamekuwa wakishirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo serikali na watoa huduma huku wakihakikisha kuwa mitambo ya mawasiliano

Saturday, March 15, 2014

MKUTANO WA KIMATAIFA WA ULINZI MTANDAO WAMALIZIKA NA KUWEKA MIKAKATI YA MWAKA 2014



Kabla ya kuanza kwa mkutano huo mapema asubuhi ya tar. 14 - 03 - 2014
Waandalizi wa mkutano wa maswala ya ulinzi mtandao wakiwa katika mapunziko ya chakula cha mchana kabbla ya kuendelea katika sehemu ya pili ya mkutano huo.

 Yusuph Kileo (katikati)akiwa pamoja na Bwana Craig rosewarne na Martin Euchner kabla ya kuelekea kwenye ukumbi wa mkutano

Wadau wakifuatilia mkutano huo .



Mkutano wa maswala ya ulinzi mtandao umemalizika kwa kuweka mkakati wenye kauli mbiu ya Mwaka 2014 ni wa vitendo

Akizungumzia mkutano huo bwana Yusuph Kileo ambaye aliongoza timu ya maandalizi ya mkutano huo alibainisha hayo na kueleza mkutano huo umekamilika salama ambapo mambo mbalimbali yalipata kujadiliwa yahusuyo ulinzi mtandao “Cyber security” na kupigilia msumari kauli mbiu ya mwaka 2014 kua ni mwaka wa vitendo.


Mwanzo wa mkutano bwana Craig Rosewarne (Mwenyekiti wa kundi linalojiuhisisha na maswala ya ulinzi mtandao (ISG) katika nchi za afrika ambaye pia ni Mkurugenzi mkuu wa kampuni Wolfpack inayo jihusisha na maswala ya ulinzi mtandao na mkurugenzi wa SANS ukanda wa nchi za Afrika na mashariki ya kati) alianisha hali ilivyo sasa na kusema kumekua na wimbi kubwa la makosa mtandao ambapo kila mwaka yanaongezeka kasi huku akitolea mifano mbali mbali ya matukio ya hivi karibuni.


Aidha alipata kuanisha ukuaji wa teknologia ambapo inaendelea kukua kwa kasi na inavyo ongeza uwezekano wa kasi ya uhalifu mtandao kukua endapo jitihada za dhati hazitowekwa tayari ili kukabiliana na changamoto zinazo rudisha nyuma vita dhidi ya ulinzi mtandao. 

Akitolea mifano changamoto mbali mbalizinazopelekea ugumu katika  ulinzi mtandao alianisha changamoto hizo ikiwa ni pamoja na:-

1.      Uhaba wa programu za kompyuta salama kimtandao huku akitolea mifano baadhi ya program za komputa zinavyo tengenezwa kutoa mwanya kwa wahalifu kupa urahisi kuingilia komputa za watumiaji wa program hizo

2.       Kutokuwepo na makubaliano ya pamoja ya kisheria  katika mapambano dhidi ya makosa mtandao.

3.      Kutokuwa na ushirikiano wa kuunganisha nguvu kati ya serikali mbali mbali na sekta binafsi kutokomeza uhalifu huu ambao unaendelea kukua kwa kasi.

4.      Kutokua na elimu kwa jamii juu ya makosa mtandao na jinsi ya kukabiliana nayo katika ngazi ya ya mtu mmoja mmoja.

5.      Kutokuwepo na utayari kwa kuunda timu katka nchi mbali mbali zenye uwezo wa kukabiliana na uhalifu mtandao.


Kwa upande mwingine Bwana Martin Euchner kutoka ITU (International telecommunication union) wakala wa umoja wa mataifa inayoshughulikia maswala ya mawasiliano alianisha hatua mbali mbali mbali ambazo hadi sasa ITU imekua ikizichukua ili kujaribu kuunganisha nchi zote za umoja wa mataifa ili kwapamoja ziweze kupambana kupunguza uhalifu mtandao.


Pia alipata kuzungumzia jitihada za dhati na mafanikio yaliyo patikana kupitia mpango wa COP (Child Online Protection) ambao umejikita kuhakiki watoto wanabaki salama mtandaoni, kauli iliyo ibua hoja nzito ya mchezo unao patikana kwenye simu hivi sasa ujulikanao kama “Talking angela” ambao umekua unachezwa na watoto wengi wadogo mtandaoni mchezo ambao umekuwa ukitiliwa shaka unaweza kuwa unatumika vibaya na wahalifu mtandao ili kukusanya sauti za watoto na picha zao zinazoweza kutumiwa vibaya baadae.


Aidha bwana Eucner, aliweza kuzungumzia mpango kabambe ambapo mapitio na kuangalia kwa karibu changamoto mtandao katika nchi mbali mbali katika mwaka huu wa 2014 zinategemewa kufanyika katika nchi takriban 16 Tanzania ikiwa ni miongoni mwa nchi zitakazo weza kufaidika na mpango huo.


Kwa upande wa bwana Kileo, Aliweza kufafanua kwa kina uhaba mkubwa wa wataalam wa maswala mtandao katika ngazi ya kidunia kwa sasa na mahitajio ya wataalam imekua ni kubwa huku akitolea mfano katika nchi zilizo endelea kuwa na mikakati kabambe ya kuunda jeshi Mtandao ili kukabiliana na vita mtandao maarufu kama “Cyber war”.


Aidha Bwana Kileo aliasa washiriki kuendelea kufahamu yakua swala la mitandao ni swala lisilo na mipaka ya kijografia na linaweza kufanywa na mhalifu kutokea maeneo yoyote bila kujali anadhuru nchi gani hivyo nguvu ya pamoja ni muhimu sana ili kuweza kukabiliana na hali mbaya iliyo sasa.

 
Katika kusisitizia kauli hiyo ya bwana Kileo, Bwana Rosewarne alieleza ni swala lililo wazi kuwa kwa sasa tatizo lipo hakuna ubishi huku akianisha hatua mbali mbali zilizochukuliwa hadi sasa kukabiliana na uhalifu mtandao ikiwa ni pamoja na:-

1.      kuwepo na tovute maalum “ Alert website” ambayo itakua inatoa elimu kwa mwananchi dhidi ya makosa mtandao.

2.      Katuni (Animation Video) ambazo tayari zimefikia 12 zinazotegemewa kuendelea kutumiwa katika televisheni ili kutoa elimu kwa jamii dhidi ya maswala mtandao.

3.      Upatikanaji wa “phishing Task force” ambapo itajikita kukabiliana na makosha ya udanganyifu mtandaoni maarufu kama “Phishing”

4.      Kuendelea kuangazia na kutengeneza “Action plan” kwa nchi za afrika na mataifa mengine kiujumla kuziwezesha kukabiliana na makosa mtandao, huku akitolea mfano wa kukamilika kwa zoezi hili katika mwaka huu kwa nchi ya Nigeria.


Wednesday, March 12, 2014

KONGAMANO LA WANATEKNOHAMA WA KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO LAANZA LEO HUKO NAIROBI

 

 

Zaidi ya wajumbe 26 kutoka Tanzania wamehudhuria kongamano la idara ya teknolojia ya habari na mawasiliano unaofanyika Nairobi nchini Kenya chini ya viongozi wa mawasiliano wakanisa la waadventista wasabatao ulimwenguni.

Kongamano hilo lililoanza leo mjini Nairobi, linahusisha viongozi wa idara ya mawasiliano wa nchi kumi za afrika mashariki na kati malengo yakiwa ni kuelimishwa na kupewa mafunzo ya uinjilisti kupitia mtandao,kuzijua teknolojia mpya za kanisa la waadventista wasabato,namna ya kuzalisha video bora,jinsi ya kuwa na tovuti za aina moja za kiadventista,uhusiano wa umma,uhamaji kutoka analojia kwenda dijitali na matumizi ya michezo ya kompyuta kwa wokovu.


Mkutano huo unaohudhuriwa na wajumbe 76 kutoka nchi kumi za afrika mashariki na kati unaendeshwa na Mch Benjamini Schoun ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato ulimwenguni, Mkurugenzi wa Idara ya Program tumishi za Kanisa la Waadventista wasabato Ulimwenguni John Becket, Gideoni Mutero ambaye makamu mwenyekiti wa Hope Channel,Mhandisi wa mifumo ya Kompyuta wa Radio ya Waadventista Ulimwenguni Daryl Gungadoo na Sam Neves mtengenezaji wa program tumishi ya michezo ya kompyuta iitwayo heroes the Game.


Mkutano huo utahitimishwa machi kumi na tatu mwaka huu.

Saturday, March 8, 2014

TABITI ZAONGOZA KUNUNULIWA DUNIANI KULIKO KOMPYUTA

Infographic: Tablets to Outsell PCs Worldwide by 2015 | Statista

Saturday, March 1, 2014

ANGALIA VIDEO YA WATU 14 WANAOSIMAMIA NA KUONGOZA MAWASILIANO YA INTANET DUNIANI

Popular Posts

Labels