Thursday, January 28, 2016

IPHONE YAPOROMOKA SOKONI

 

Kampuni kubwa ya teknolojia ya Apple imesema mauzo ya simu zake zijulikanazo kama iPhone yameanza kupungua na kwamba mauzo hayo yanatarajiwa kushuka kwa mara ya kwanza tangu kuzinduliwa kwa simu hizo 2007.

Kampuni hiyo kutoka Marekani iliuza simu 74.8 milioni robo ya kwanza ya mwaka huu wa kifedha ikilinganishwa na simu 74.5 milioni robo ya kwanza ya mwaka uliotangulia. Apple imesema mauzo kutoka kwa robo ijayo yanatarajiwa kuwa kati ya $50 bilioni na $53 bilioni, kiasi ambacho kitakuwa chini ya mauzo ya $58 bilioni kipindi sawa mwaka uliotangulia.

Hii itakuwa mara ya kwanza kwa mauzo ya iPhone kushuka tangu kuzinduliwa kwa simu hizo za kisasa.

Mauzo ya iPhone yalichangia asilimia 68 ya faina ya kampuni ya Apple mwaka jana.

Kushuka kwa mauzo ya kampuni hiyo kunadaiwa kutokana na kiwango cha uchumi wa China kushuka.

Mauzo ya Apple nchini China, Hong Kong na Taiwan yaliongezeka 14%, lakini kiwango hicho cha ukuaji ni cha chini mno kikilinganishwa na ukuaji wa 70% ulioshuhudiwa mwaka mmoja uliopita.

MAUZO YA SIMU ZA KISASA (SMARTPHONE) ZA SAMSUNG YASHUKA


 
Kampuni ya vifaa vya kielektroniki, Samsung imeathiriwa na kushuka kwa mauzo ya simu zake za aina ya Smartphone.

Mazingira mabaya ya kibiashara na viwango vya chini vya vifaa vya kiteknolojia vilisababisha kushuka kwa faida katika robo ya nne ya mwaka jana kwa asilimia 40 hadi dola bilioni 2.7.

Kampuni hiyo ya Korea Kusini imeonya kwamba itakuwa vigumu kudhibiti faida mwaka huu kama ilivyokuwa mwaka 2015.

Mapato ya mwaka 2015 yalishuka hadi dola bilioni 165 ikilinganishwa na miezi 12 iliopita.

Ushindani mkali kutoka kwa kampuni za Uchina zinazotengeza vifaa rahisi vya kiteknolojia kama vile Xaiomi na Huwawei katika soko hilo pamoja na kampuni ya Apple zimeathiri mauzo ya simu za Smartphone.

Simu ya Galaxy S6,ambayo ndio simu ya hadhi ya juu iliozinduliwa mnamo mwezi Aprili,ilishindwa kuwafurahisha wateja na kampuni hiyo imeshindwa kudhibiti soko lake.

Jake Saunders,mkurugenzi wa Asia-Pacific katika kampuni ya utafiti ya ABI Research,ameiambia BBC:''Inaonyesha kwamba wako chini ya shinikizo kwa sababu nusu ya mapato yao yanatoka katika simu za rununu''.

Xiaomi inapata wateja katika soko la India na Indonesia,ambalo ni kubwa kwa simu za smartphone na ndio eneo ambalo linakuwa kwa haraka.

Wednesday, January 20, 2016

NYWILA ZILIZOTUMIWA SANA NA WATU MWAKA 2015

Kampuni ya usalama mtandaoni ya SplashData imetoa orodha ya nywila au maneno ya siri yaliyotumiwa sana na watu mwaka uliopita.

Orodha hiyo imetayarishwa kwa kutumia maneno ya siri zaidi ya milioni mbili yaliyofichuliwa na wadukuzi mwaka uliopita.

Mwaka huu, neno ‘Star Wars’, kutoka kwa mwendelezo wa filamu za Star Wars, lilikuwa miongoni mwa maneno 25 yaliyotumiwa zaidi. Filamu ya Star Wars: The Force Awakens ilizinduliwa mwezi Desemba.

Wengi bado wanatumia ‘123456’ kama nywila na wengine ‘password’.
Ili kuwa salama mtandaoni, huwa ni vyema kutumia nyila ambayo watu wengine hawawezi wakaifikiria au kugundua kwa urahisi.

Moja ya njia za kuimarisha neno la siri ni kuchanganya tarakimu, herufi na alama pamoja na kuchanganya herufi kubwa na ndogo.

Lakini wengi hutatizika katika kukumbuka nywila.

Moja ya njia unazoweza kutumia ni kuangalia maneno ya wimbo uupendao na kuyafupisha.

Hapa kuna mfano wa jinsi unaweza kupata nyila kutoka kwa wimbo.
  1. Chagua mwanamuziki umpendaye, tuseme
  2. Chagua wimbo wake
  3. Tafuta mstari mmoja, sana ukupendezao zaidi,
  4. Fupisha kwa kuchukua herufi ya kwanza ya kila neno, au herufi mbili za kwanza. Tukichukua herufi mbili za kwanza.
  5. Changanya herufi kubwa na ndogo
  6. Kisha, badilisha herufi zinazokaribiana na tarakimu kuwa tarakimu, mfano badala ya ‘a’ tumia ‘@’ na badala ya ‘i’ tumia ‘1’.
 Ni vigumu mtu kuigundua kwa urahisi lakini kila ukikumbuka wimbo wako unaweza ukaikumbuka kwa urahisi.

 Nywila zilizotumiwa sana 2015
1. 123456
2. password
3. 12345678
4. qwerty
5. 12345
6. 123456789
7. football
8. 1234
9. 1234567
10. baseball
11. welcome
12. 1234567890
13. abc123
14. 111111
15. 1qaz2wsx
16. dragon
17. master
18. monkey
19. letmein
20. login
21. princess
22. qwertyuiop
23. solo
24. passw0rd
25. starwars
Chanzo:BBC

Saturday, January 16, 2016

KUMBUKA TCRA ILISHATOA MUDA WA MIEZI SITA KUZIFUNGA SIMU FEKI NCHINI TANZANIA ANGALIA VIDEO NA MAELEZO



UTANGULIZI:

Vifaa vya mawasiliano vya mkononi – hususan simu za kiganjani na vifaa vya mawasiliano vya kiganjani (tablets) – vina namba maalum inayovitambulisha. Namba hiyo inajulikana kama IMEI ambacho ni kifupi cha International Mobile Equipment Identity.


Kifungu cha 84 cha Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta (EPOCA) ya 2010 kinataka kuwepo kwa mfumo wa rajisi ya namba za utambulisho wa vifaa vya mawasiliano vya mkononi. Rajisi hii inajulikana kwa kiingereza kama Central Equipment Identification Register, kwa kifupi CEIR. Sheria inataka rajisi hiyo ihifadhiwe na kuendeshwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania.


Aidha Kanuni za mwaka 2011 za EPOCA kuhusu mfumo wa rajisi ya namba za utambulisho wa vifaa vya mawasiliano vya mkononi inawataka watoa huduma wa mawasiliano yanayotumia vifaa vya mkononi kuweka mfumo wa kudumu wa kumbukumbu za namba tambulishi (Equipment Identity Register – EIR) za vifaa vya mkononi vinavyotumika kwenye mitandao yao.


Mfumo huu wa kielektroniki ambao utahifadhi kumbukumbu za namba tambulishi za vifaa vya mawasiliano vya mkononi una lengo la kufuatilia namba tambulishi za vifaa vinavyoibiwa, kuharibika, kupotea au ambavyo havikidhi viwango vya matumizi katika soko la mawasiliano.


Vifaa vyote vya mawasiliano vya mkononi ambavyo vimeibiwa, vimeharibika, kupotea au visivyokidhi viwango vya matumizi katika soko la mawasiliano havitaweza kufanya kazi kwenye mitandao ya mawasiliano kutumia vifaa vya mkononi.


UFAFANUZI
Taarifa kwenye mfumo huu wa rajisi zitakuwa na aina tatu za kumbukumbu; ambazo ni orodha ya namba tambulishi ambazo vifaa vyake vinaruhusiwa, orodha ya namba tambulishi ambazo zimetolewa taarifa kuwa zimefungiwa na namba tambulishi ambazo zimefungiwa kwa muda au kuruhusiwa kwa muda.


Orodha Nyeupe:
Orodha ya vifaa vya mkononi vya mawasiliano vinavyoruhusiwa kutumika katika mitandao ya huduma za simu za kiganjani


Orodha Nyeusi:
Orodha hii ni ya namba tambulishi ambazo zimefungiwa na mtoa huduma kwenye mfumo wao wa EIR na kutumwa kwenye mfumo wa CEIR kwa ajili ya kufungiwa ili zisitumike kwenye mitandao mingine ya simu za kiganjani kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa na kukubaliwa miongoni mwa watoa huduma. Simu zote za mkononi zilizoibiwa au kupotea zitafungiwa ndani ya saa 24 ili zisitumike kwenye mtandao wowote wa simu za mkononi Tanzania.


Ikitokea simu ya mtumiaji ikafungiwa kinamosa, anatakiwa kutoa taarifa mara moja kwa mtoa huduma wako kwa ajili ya kuifungua. Watoa huduma wanatakiwa wafungulie, ndani ya saa 24, simu zote zilizofungwa kimakosa.

Orodha ya kijivu:
Orodha hii ni ya namba tambulishi ambazo zimefungiwa au kufunguliwa kwa muda kwa lengo la kuanzisha mchakato wa kuzifuatilia.

FAIDA ZA MFUMO WA RAJISI YA NAMBA TAMBULISHI
Mfumo huu wa rajisi una faida zifuatazo:
1. Kuthibiti wizi wa simu. Iwapo mtu atapoteza au ameibiwa simu ya kiganjani na akatoa taarifa kwa mtoa huduma, simu hiyo itafungiwa isiweze kutumika kwenye mtandao mwingine wowote wa simu za kiganjani. Mteja anaponunua simu ni lazima adai risiti halali na halisi na pia garantiii ya angalau miezi 12. Mteja anatakiwa aihifadhi risiti hiyo angalau kwa miezi mitatu. Baada ya hapo, iwapo simu imekuwa inatumika, taarifa za matumizi zinaweza kutumika kama uthibitisho mbadala wa milki ya simu husika.


2. Kuhimiza utii wa sheria: Kifungu cha 128 cha EPOCA kinamtaka mtumiaji wa simu kutoa taarifa ya kupotea au kuibiwa kwa simu au laini ya simu. Kifungu cha 134 kinayataka makampuni ya simu kutokutoa huduma kwa simu ambayo imefungiwa kama ilivyoelezwa hapo juu. Mara tu mteja anapopoteza simu yake ya kiganjani anatakiwa kutoa taarifa kwa kituo cha Polisi cha karibu ambapo atapewa namba ya kumbukumbu ya taarifa ya tukio, maarufu kama RB.

Anatakiwa aende kwa mtoa huduma kutoa taarifa ya tukio akiwa na hiyo RB na uthibitisho wa umilki wa simu iliyopotea ( risiti aliyopewa wakati wa kununua iwapo itakuwepo). Mtoa huduma kwanza atahakiki umilki wa simu iliyopotea au kuibiwa na atampatia mteja namba ya kumbukumbu kwamba simu hiyo imefungiwa isutumike kwenye mitandao ya simu na hatimaye ataifungia simu hiyo ndani ya saa 24.


3. Kujenga misingi ya matumizi ya simu halisi, zisizo bandia. Mtumiaji ataweza kutambua iwapo simu aliyo nayo inakidhi viwango, ni halisi na sio bandia.


KUTAMBUA NAMBA TAMBULISHI
Ili kutambua namba tambulishi ya simu ya kiganjani au vifaa vya mawasiliano ya kiganjani, mtumiaji anatakiwa aandike tarakimu *#06# kwa kutumia kifaa chake. Baada ya kufanya hivyo, kutaonekana namba ndefu. Mtumiaji anatakiwa kuandika namba hiyo kama ilivyoonekana kwenye kifaa chakena kuihifadhi katika hali ya usalama kwa ajili ya rejea ya baadae.


Baada ya hapo mtumiaji atume ujumbe mfupi wenye hiyo namba tambulishi kwenda namba 15090. Atapokea meseji itakayomjulisha kuhusu hali halisi ya simu yake ya kiganjani. Mtumiaji atapokea ujumbe kuhusu uhalisia wa simu yake. Majibu yatakayokuja yatasomeka: Kama IMEI haioani na aina ya simu yako, wasiliana na aliyekuuzia. Usipoweza,ibadilishe kabla ya Juni 2016 kwani simu hiyo inaweza kuwa BANDIA.


HATUA ZA KUCHUKUA IWAPO SIMU ITAONEKANA HAIKIDHI VIWANGO, SI HALISI NA NI BANDIA

Mtu yeyote ambaye atatambua kwamba simu yake ya kiganjani si halisi,ni bandia na haikidhi viwango atapewa muda wa kuendelea kutumia simu hiyo. Baada ya muda huo kumalizika, simu hiyo itaingizwa katika orodha nyeusi na kufungiwa isitumike kwenye mitandao mingine yoyoye ya simu za kiganjani.


Watumiaji wote wenye simu za kiganjani ambazo namba tambulishi zao zinaonyesha kwamba simu hizo si halisi, ni feki na hazikidhi viwango watagharamia ununuzi wa simu nyingine.


Watumiaji wote ambao namba tambulishi za simu zao zinaonyesha kwamba vifaa hivyo si halisi, ni feki na havikidhi viwango watatakiwa kubadilisha simu hizo na kupata zinazokidhi viwango na halisi katika muda wa miezi sita kuanzia siku ya uzinduzi wa mfumo wa rajisi ya namba za utambulisho wa simu za kiganjani.


Ni vyema ifahamike kwamba simu zote za kiganjani na vifaa vya mawasiliano vya kiganjani (tablets) ambazo zitakuwa na namba tambulishi bandia zitafungiwa kuanzia 16 Juni 2016.

HITIMISHO
Mfumo wa Rajisi ya Namba za Utambulisho wa vifaa vya mawasiliano vya mkononi una lengo la kuwahakikishia watumiaji usalama wakati wanapotumia vifaa hivyo vya mawasiliano, vikiwemo simu za kiganjani na vifaa vya mawasiliano vya kiganjani (tablets). Uanzishwaji wake ni sehemu ya kutekeleza matakwa ya Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta ya 2010. Ni vyema watumiaji wakazingatia maelekezo kuhusu utaratibu wa kuhakiki namba tambulishi, kutoa taarifa wanapopoteza au kuibiwa simu.


Imetolewa na:
Mkurugenzi Mkuu
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania
18 December 2015


Thursday, January 14, 2016

ASILIMIA 60 YA WAKAZI DUNIANI HAWANA NJIA YA KUTUMIA MTANDAO WA INTANETI



 


Wakaazi bilioni 4.2 wa dunia hawana njia ya kutumia mtandao wa Intaneti.
 
Idadi hiyo ni sawa na asili mia 60 ya wakaazi wa dunia-benki kuu ya dunia imesema hayo mjini Washington. 

Kumeibuka "pengo la digitali" kutokana na ule ukweli kwamba intanet inakutikana zaidi katika nchi tajiri. 

Nchini India watu bilioni moja nukta moja hawana mtandao wa intaneti,nchini China wanafikia watu milioni 755 na Indonesia watu milioni 213. 

Pengo hilo linazidi kuwa pana linapohusika suala la intaneti ya haraka-inasema benki kuu ya dunia. 

Wanaofaidika na  intaneti kama hiyo ni watu bilioni moja nukta moja tu-ikimaanisha chini ya asilimia 15 ya wakaazi jumla wa dunia.

"Watu wanabidi wajiepushe isiibuke "tabaka mpya ya wanaobaguliwa kijamii" anaonya mwanauchumi mkuu wa benki kuu ya dunia Kaushik Basu katika ripoti yake iliyopewa jina "Faida ya teknolojia ya habari."

AFRIKA KUSINI KUDHIBITI WHATSAPP NA VIBER

 

 
Mitandao ya whatsapp na viber huenda ikadhibitiwa Afrika Kusini ikitegemea matokeo ya vikao vya bunge baadaye mwezi huu, umeripoti mtandao unaoheshimika wa Fin24.

Umaarufu wa Whatasap inayomilikiwa na facebook umeongezeka nchini Afrika Kusini ukiwa na watumiaji Zaidi ya milioni kumi kwa mujibu wa ripoti ya World Wide Worx na Fuseware.

Kampuni mbili kubwa za simu Afrika kusini Vodacom na MTN mwaka uliopita zilitoa wito wa kudhibitiwa kwa huduma hizo.

Kuna hawa washiriki wanaopata manufaa makubwa katika sekta hii bila kutumia pesa. Tutapataje usawa?" afisa mmoja wa MTN alinukuliwa akisema.Kamati ya bunge kuhusu mawasiliano ya posta ilipanga kufanya kikao hicho tarehe 26 mwezi January kujadili sera za kuingilia kati swala hilo.
 Chanzo:BBC

TTCL YAKOPA DOLA MILIONI 22 KUSAMBZA MTANDAO WA 3G NA 4G LTE

http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2016/01/bt.jpg
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura (kushoto) akibadilishana hati ya makubaliano ya mkopo na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Uwekezaji (TIB), Jaffer Machano mara baada ya kutiliana saini.

Kampuni ya Simu Tanzania TTCL na Benki ya TIB zimetiliana saini Mkataba wa makubaliano ya dhamana ya Benki na Mkopo wa Dola za Marekani Milioni 22 ikiwa ni awamu ya kwanza ya mkopo wa Dola za Marekani milioni 329 itakazopewa TTCL.

Akizungumza katika hafla ya kusaini hati ya makubaliano ya mkopo huo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk. Kamugisha Kazaura alisema mkopo huo ni mahususi kwa ajili ya kuiwezesha TTCL kusimika mitambo mipya na ya kisasa kuboresha huduma zake kwa kujenga na kusambaza huduma za  Mitandao ya 3G na 4G LTE  nchini kote.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TIB, Jaffer Machano amesema katika kutimiza wajibu wa TIB kama benki ya maendeleo, ujenzi wa miundombinu umepewa kipaumbele na hii ni pamoja na miundombinu ya sekta ya Mawasiliano.

Baadhi ya huduma za TTCL zitakazoimarika baada ya uwezeshaji huu ni pamoja huduma za simu na intaneti yenye kasi kubwa inayowezesha huduma za kijamii kufanyika kwa urahisi kwa njia ya mtandao.

 Huduma kama vile za Elimu kwa njia ya mtandao (E education), Afya kwa njia ya mtandao (E health) na huduma katika Sekta nyingine za kiuchumi kama vile Biashara, Viwanda na Kilimo nazo zitanufaika sana ambapo wafanyabiashara na wazalishaji wa bidhaa mbalimbali watapata Mawasiliano ya uhakika katika kufanikisha shughuli zao.

Kampuni ya Simu Tanzania TTCL ipo mbioni kuanzisha huduma ya kusafirisha fedha kwa njia ya Mtandao ifikapo robo ya pili ya mwaka huu ili kutekeleza ombi la muda mrefu la Wateja wake wanaohitaji sana kuanzishwa kwa huduma hii kutokana na Mtandao mpana wa Kampuni uliosambaa ndani na nje ya nchi na unafuu wa gharama.

Tuesday, January 12, 2016

TWITTER KUONGEZA IDADI YA HERUFI HADI 10,000

 

Twitter ina mpango wa kuongeza kiwango cha idadi ya herufi zinazoandikwa katika nafasi ya ujumbe kutoka 140 hadi 10,000 sawa na ujumbe wa kawaida.

Baada ya uvumi mtandao huo sasa umeamua kuongeza idadi hiyo.

Ni hatua ya hivi karibuni ya Twitter kuweza kuwavutia wateja zaidi.

Mkuu wa Twitter na mwanzilishi Jack Dorsey amesema kuwa ataongeza idadi ya kiwango cha herufi zitakazotumika.

Iwapo Twitter itakubali kiwango cha ujumbe wenye herufi 10,000 huenda ikazalisha ujumbe wa maneno 1,700.

Katika ujumbe wake ,Jack Dorsey ameandika kwamba Twitter tayari imebaini kwamba wengi wa wateja wake milioni 300 tayari wamekuwa wakipiga picha kubwa za ujumbe mrefu katika ujumbe wao.

Amesema kuwa Twitter inajaribu kutafuta mbinu za kuwapa watu zaidi uwezo wa kujielezea bila kuchafua huduma hiyo.
Chanzo:BBC

Tuesday, January 5, 2016

ELIMU DUNI YA MTANDAO CHANZO CHA MATUMIZI MABAYA YA MITANDAO YA KIJAMII



 

Wadau mbalimbali wa mitandao ya kijamii jijini Arusha wameeleza kuwa, Elimu duni kuhusu matumizi ya mtandao ndio chanzo cha matumizi mabaya ya mitandao hiyo hali inayosababisha migogoro katika jamii. 

Akizungumzia suala hilo Bwana Fransis Kimati ameeleza kuwa elimu duni kuhusu mitandao ikiwemo ukuaji wa sayansi na Teknolojia ndio chanzo kikubwa cha mmomonyoko wa maadili hususani kwa vijana. 

Kwa upande wake Bw. Joshua Jacob ambaye ni mwandishi wa vitabu amesema, hatua zinataikiwa kuchukuliwa ikiwemo utolewaji elimu kwa rika la vijana ambao ndio kundi kubwa la watumiji wa mitandao, kupitia vitabu, majarida warsha na matamasha mbalimbali, ili kubadilisha mitazamo mibaya kwa vijana.

Aidha wamesema kuwa dhamira ya kuwepo mitandao ya kijamii mbalimbali ikiwemo Facebook,Twiter ni nzuri lakini bado jamii haijawa na ufahamu wa kutumia mitandao hiyo kwa kujiendeleza katika njanja mbalimbali.

Popular Posts

Labels