Tuesday, March 24, 2015

TEKNOLOJIA YA KUHAKIKI DAWA BANDIA AMA HALISI YABUNIWA GHANA




Wataalamu wa Teknolojia nchini Ghana wamebuni teknolojia ya kuhakiki ikiwa dawa ni bandia au ni halisi. 

Teknolojia hiyo iliyozinduliwa juma hili  na Rais wa Umoja wa wamiliki wa maduka ya dawa nchini Ghana (PSHG),James Ohemeng Kyei,inamwezesha mnunuzi kukwaruza kikaratasi kilichoko kwenye pakiti ya dawa kupata nambari maalum , kisha akatuma nambari hiyo kama ujumbe wa simu ya mkononi kwa mitandao yote ya simu nchini humo kwenda kwa namba 1393.

A prospective buyer or user is expected to scratch the seal off the secret code and text it to the short code 1393 on all networks to authenticate the drug. - See more at: http://graphic.com.gh/news/health/29319-technology-to-detect-fake-drugs-launched-in-accra.html#sthash.bEGTIGx9.dpuf
A prospective buyer or user is expected to scratch the seal off the secret code and text it to the short code 1393 on all networks to authenticate the drug. - See more at: http://graphic.com.gh/news/health/29319-technology-to-detect-fake-drugs-launched-in-accra.html#sthash.bEGTIGx9.dpuf
A prospective buyer or user is expected to scratch the seal off the secret code and text it to the short code 1393 on all networks to authenticate the drug. - See more at: http://graphic.com.gh/news/health/29319-technology-to-detect-fake-drugs-launched-in-accra.html#sthash.bEGTIGx9.dpuf
A prospective buyer or user is expected to scratch the seal off the secret code and text it to the short code 1393 on all networks to authenticate the drug. - See more at: http://graphic.com.gh/news/health/29319-technology-to-detect-fake-drugs-launched-in-accra.html#sthash.bEGTIGx9.dpuf
A prospective buyer or user is expected to scratch the seal off the secret code and text it to the short code 1393 on all networks to authenticate the drug. - See more at: http://graphic.com.gh/news/health/29319-technology-to-detect-fake-drugs-launched-in-accra.html#sthash.bEGTIGx9.dpuf
A prospective buyer or user is expected to scratch the seal off the secret code and text it to the short code 1393 on all networks to authenticate the drug. - See more at: http://graphic.com.gh/news/health/29319-technology-to-detect-fake-drugs-launched-in-accra.html#sthash.bEGTIGx9.dpuf
Kwa mujibu wa mtando wa graphic.com teknolojia hiyo iliyopewa jina la PREVENT inaweza kutoa majibu baada ya sekunde 10  ikiwa ni dawa bandia au halisi ambayo imewezeshwa kutumiwa katika mitandao ya simu za mkononi na mitandao ya kijamii.

Teknolojia hiyo ambayo imebuniwa kutokana na mkakati wa PSHG wa kuisaidia serikali kupambana na uuzwaji wa dawa bandia na zilizo chini ya kiwango itawezeshwa na Wizara ya Afya ya Ghana,Mamlaka ya Chakula na Dawa na wadau mbalimbali nchini humo.

WABUNGE WA TANZANIA WAITAKA SERIKALI KUZIBANA KAMPUNI ZA SIMU NA BENKI

Wabunge wa Tanzania wameibana serikali wakiitaka iboreshe muswada wa sheria ya mifumo ya malipo ili kuzibana kampuni za simu na mabenki,kutokana na kushamiri kwa wizi katika mifumo ya malipo kwa njia ya kielekroniki kwenye simu za kiganjani na miamala ya fedha ya benki.

Wakizungumzia bungeni jana wakati wakichangia muswada huo,wamesema kampuni za simu zinawakata wananchi fedha katika simu zao za kiganjani bila ridhaa yao na hakuna sehemu yoyote wanayoweza kufikisha malalamiko yao ili warejeshewe fedha hizo.

Katika muswada huo uliowasilishwa na Waziri wa Fedha,Saada Mkuya Salum,Serikali imependekeza kuboresha usimamizi na kuongeza udhibiti,kuimarisha mifumo ya malipo,pia kuzuia na kudhibiti athari zinazoweza kujitokeza katika mifumo hiyo na kuongeza faini kwa kampuni za simu na benki zitakazokiuka sheria na utaratibu.

Saturday, March 14, 2015

MTANZANIA ABUNI NA KUTENGENEZA PROGRAM TUMISHI YA KITABU CHA NYIMBO ZA KRISTO KATIKA VIFAA VYA APPLE






Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Union Konferensi ya Kaskazini mwa Tanzania katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Gideon Msambwa ameweka historia ya kuwa mtanzania wa kwanza kubuni na kutengeneza program tumishi ya kiswahili ya kitabu cha nyimbo za Kristo zinazotumiwa na waumini wa kanisa hilo ambayo ni program pekee  ya nyimbo za injili kwa lugha hiyo kubuniwa na kutumiwa katika vifaa vya mawasiliano vya kampuni ya Apple duniani.

Gideon Msambwa ameiambia blog hii kuwa  program hiyo iliwezeshwa na Apple kupatikana katika vifaa vya mawasiliano vinavyoendeshwa na program ya endeshi ya iOS ambavyo ni iPhone,iPad na iPod na imeanza kutumika rasmi Machi 12,2015.

Popular Posts

Labels