Friday, April 5, 2019
UCHUNGUZI WAONESHA TATIZO LA KIMFUMO LILISABABISHA AJALI YA BOEING 737 MAX 8
Ripoti ya awali ya uchunguzi wa ajali ya ndege la Shirika la Ndege la Ethiopia safari namba 302 inaonyesha kwamba ajali hiyo ilitokana na tatizo la kimfumo katika ndege na kwamba marubani wa ndege hiyo walifanya kila walichoelekezwa na kufuata taratibu zote kwa mujibu wa watengenezaji wa ndege hiyo lakini hawakufanikiwa kuizuia isianguke.
Mfumo katika aina ya ndege iliyoanguka (Boeing 737 Max 8 ) umekuwa katika mjadala mkubwa kiasi cha kusababisha nchi nyimgi kuamrisha kusimamishwa kwa matumizi ya ndege hizo na Wizara ya Sheria, Mkaguzi Mkuu masuala ya Usafirishaji na Kamati za Bunge la Marekani vimeanzisha uchunguzi tofauti na maalum wa namna ambavyo kampuni hiyo ilivyofanya maboresho ya mfumo na walivyopata kibali cha uthibitisho wa ubora toka Mamlaka ya Anga ya Marekani.
Ndege hiyo iliyoanguka Machi 10, 2019 na kuua abiria wote 157, ilikuwa ni ya pili ya aina hiyo kuanguka ndani ya miezi 5 na hilo likazua hofu kwa wasafiri na wasafirishaji kuhusu usalama wa ndege hizo.
Ripoti kamili inatarajiwa kutoka baadae sana, lakini punde nitakapopata nakala ya awali ya ripoti hiyo nitaileta hapa ili kushiriki nanyi juu ya dondoo za uchunguzi huo.
Shirika la Boeing linalotengeneza ndege hizo lilitangaza kwamba lingefanya maboresho ya mfumo huo hivi karibuni lakini inaonekana wamesubiri matokeo haya ili kuhakikisha wanawathibitishia wateja wake kuwa wanaboresha kile kinachowatia hofu kutokana na ajali mbili za ndege zake.
Na: Mubelwa Bandio-Marekani
Labels:
Habari
Popular Posts
-
Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia ,Bw Charles Kitwanga ameyashawishi mataifa ambayo tayari yamejiunga na mfumo wa Digitali katika haraka...
-
Shule ya sekondari ya Waadventista Wa Sabato {Tass} imepokea jumla ya komputa hamsini zitakazotumika katika mafunzo ya utafiti kivitendo ...
-
Microsoft is switching off its Windows Live Messenger service on 15 March. On that date Messenger log-ins will no longer work a...
-
Blogger katika picha ya pamoja na wawezeshaji wa Ubalozi wa Marekani Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania kupitia kitengo chake cha M...
-
Recording video has become easier than ever with the growing number of smart phones and the recording function of digital still cameras. Fo...
-
Over the years, Safer Internet Day (SID) has become a landmark event in the online safety calendar. Starting as an initiative of the EU ...
-
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Kudumu za Serikali imebaini madudu yanayofanyika katika uwekezaji wa kampuni za simu nchini Tanzania ...
-
Mwishoni mwa juma lililopita pamegundulika hali mbaya ya kiusalama mtandao itakayo waathiri watumiaji wa kivinjari kijulikanacho kama...
-
ILI kuboresha utoaji huduma kwa umma hivi karibuni Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeanzisha utaratibu wa kupokea malala...
-
Baada ya kuwepo kwa uvumi wa kipindi kirefu kuwa kampuni ya Apple inampango wa kutengeneza magari yake hatimaye siri zimeanza kuvuja...