Kiongozi wa kanisa Katoliki duniani Papa Francis amesema kuwa Internet
ni zawadi kwa dunia nzima kutoka kwa Mungu lakini akaonya kuwa matamanio
ya kutaka kuwasiliana zaidi kutumia Intaneti kunawatenga watu kutoka
kwa familia na marafiki zao.
Amewataka waumuni wa kikatoliki kujiunga na mfumo wa dijitali.
"Intaneti... inatoa nafasi ya mafanikio mengi. Hiki ni kitu kizuri bila
shaka ni zawadi kutoka kwa Mungu,'' alisema Papa.
Katika ujumbe wake kwa dunia nzima ambao hutolewa kila mwaka, Papa
amesema kuwa mfumo wa dijitali, unapaswa kuwa mtandao wa watu wala sio
nyaya tupu.
Papa mwenyewe ana akaunti kwenye Twitter ambayo ina wafuasi zaidi ya milioni kumi.
Amehimiza kuwa mawasiliano yanapaswa kuhusisha hisia na mawazo, watu kukutana na kujuliana hali.
Kadhalika amewataka waumini wa kikatoliki
kutodhani kuwa ni mawazo yao na imani zao pekee ambazo ni muhimu wakati
wakiwasiliana na watu wa dini nyinginezo.
Chanzo:BBC
Popular Posts
-
SERIKALI YA TANZANIA YASEMA:KUTOA TAARIFA ZA SIRI KATIKA MAWASILIANO YA ELEKTRONIKI NI KOSA LA JINAITAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Jana na leo, Serikali ya Tanzania imeona kuzuka kwa tabia ya uvunjaji wa kanuni ya utunza...
-
Facebook wametangaza kitu kipya kwa simu za Android walichokipa jina la Home. Kwa muda mrefu kulikuwa na uvumi kuwa Facebook wana...
-
Microsoft is switching off its Windows Live Messenger service on 15 March. On that date Messenger log-ins will no longer work a...
-
Watu wengi wameshaona filamu ambazo wahalifu wakidukua simu za mikononi hata kama zimezimwa. Kama ili...
-
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dr Ally Simba Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imevitaka vituo vya redio na televi...
-
Na Yusuph Kileo Nchi ya Tanzania yabahatika tena kwa mara ya tatu kuwa mwenyeji wa mkutano wa “Connect 2 Connect” ambapo kauli mbiu ya...
-
Serikali ya Tanzania inapenda kuufahamisha umma wa Watanzania kuwa hivi karibuni kumezuka kundi la Watu wadanganyifu ambao wamekuwa wakit...