Kampuni ya Simu za Mkononi ya Airtel Tanzania imesema kuwa imeshazima laini za simu 200,000 ikiwa ni utekelezaji wa sheria ya posta na mawasiliano ya kielektroniki ya mwaka 2010 ikimbatana na muda wa mwisho wa kusajili laini za simu nchini Tanzania kuwa ni julai 10,2013 uliowekwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Usimamizi wa Sheria wa Airtel Tanzania Beatrice Singano amesema waliwajulisha wateja wao mapema kusajili laini zao za simu ili kuepuka kufungwa kwa laini za wateja wao.
Amesema kuanzia julai 10 mwaka huu kama mamlaka ya mawasiliano Tanzania ilivyotangaza Aprili mwaka huu kwa sasa jumla ya wateja 200,000 wa kampuni hiyo wamefungiwa laini zao kutokana na kutosajili.
Ili kufahamu laini ya simu imesajili mmiliki wa simu anapaswa kuhakiki usajili huo kwa kupiga *106#.
Usajili wa namba za simu kama ilivyo katika nchi mbalimbali duniani umekuwa ukiendelea na kwa miaka michache katika nchi za Afrika Mashariki lengo likiwa ni kudhibiti matukio ya uharifu yanayofanywa ama kuanzishwa na watumiaji wa simu za mikononi katika nchi hizo.
Popular Posts
-
Kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania Dr Godwin Lekundayo akiwaongoza viongozi wenzake katika maombi wakati wa ugawaji wa...
-
Miongoni mwa changamoto inayoonekana kwa sasa katika teknolojia ya habari na mawasiliano (Teknohama) ni suala la ulinzi katika mitandao...
-
Baraza la Sanaa la Taifa nchini Tanzania (BASATA) limetoa siku saba kwa wasanii,vituo vya radio,runinga wamiliki wa tovuti na wa...
-
Meneja Uhusiano wa kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Thomas Mushi akizungumza na vyombo vya habari leo jijini Dar es Salaam...
-
Waziri wa Mawasiliano , Sayansi na Teknolojia Profesa Makame Mbarawa amesema hajapokea maombi ya Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Ta...
-
Waziri na waziri wa uchukuzi Dr Harrison mwakyembe amesema kuwa Teknolojia ya kisasa inayotumika katika uwanja wa ndege wa kimataifa...
-
Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji wa Serikali Dk. Hassan Abbas (kulia), akihutubia wakati wakati akifungua Mkutano Mkuu wa...
-
Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imeingilia kati wizi wa fedha kwa kutumia mashine za kutolea fedha (ATM), ambao umeibua hofu kubwa katika s...
-
Click the image to open the interactive version (via http://pennystocks.la ).
-
Watumiaji wa simu za Nokia na Windows wamekuwa wakitamani kutumia huduma ya ujumbe wa maneno ya BlackBerry (BBM) huduma hiyo sasa itap...