
Kampuni ya Teknolojia ya Google imesema itaanza kutengeneza magari yasiyohitaji madereva.
![]() |
Magari bila Usukani |
Google imesambaza picha ya gari hilo ambalo inasema ni la kutumiwa mijini na linapaswa kuwa chambo kwa wale ambao bado hawana imani na teknolojia hii ya hali ya juu.
![]() |
Gari linalojiendesha |
Brin alisema kuwa teknolojia hiyo inauwezo mkubwa wa kuimarisha maisha ya watu .
Watafiti wa magari yanayojiendesha yenyewe bado wanajadili iwapo kuwepo kwa magari hayo mabarabarani yatakuwa na upungufu wowote ikiwemo dhana kuwa itachangia ongezeko la msongamano wa magari.
Chanzo:BBC