Monday, August 7, 2017

MAAMUZI TOKA KWA MKUTANO WA GAiN 2017 BRAZIL


 Image may contain: 30 people, people smiling, people standing, shoes and indoor

Mkutano Mkuu wa Mifumo ya utunzaji na usimamizi wa washiriki wa Kanisa la Waadventista wa Sabato Ulimwenguni umemalizika katika jiji la Sao Paulo, Brazil Agosti 6 2017 ukiwa umefanya maazimio yafuatayo.

1. Taarifa rasmi na sahihi za idadi ya washiriki wa kanisa zitapatikana kupitia mfumo wa ACMS pekee.

2. Anwani za makanisa yote ya Waadventista zinapaswa zipatikane kupitia mfumo wa ACMS

3. Kila mwezi karani wa kanisa atatuma taarifa ya washiriki kwenda konferensi, ambayo itaendelea kutumwa mpaka ngazi ya juu.

4. Division ya Amerika kusini inajaribiwa na mfumo mpya wa 7ME ambao unaruhusu kila mshiriki kujaza takwimu zake mwenyewe na ukifanikiwa ndio utatumika rasmi ulimwenguni kote ifikapo mwaka 2018.

5. Idara zote za kanisa zitatumia mfumo wa ACMS kutoa taarifa za idara.

Mkutano huu ulikuwa na wajumbe 31 kutoka ulimwenguni kote na Divisheni ya Afrika Mashariki na kati iliwakiliswa na wajumbe wawili

Popular Posts

Labels