Friday, April 26, 2013
UNAVYOWEZA KUJILINDA NA PACHIKO AMA PICHA USIZOZIHITAJI KWENYE FACEBOOK ANGALIA HAPA
Kumekuwa na changamoto ya kujilinda na watu ambao wanaweza kukuwekea maelezo ama kukutagg picha usiyoihitaji kwenye timeline yako kwenye facebook iwe ni picha ama ni taarifa mbaya ama usizozihitaji.Na utagundua ya kwamba kuna watu ambao hata huwezi amini kama kweli wao wameweka picha zilizo kinyume na maadili na hii imekuwa ikiwakera wao ama watu wanaowasiliana nao kwenye mtandao wa facebook.
Kama inavyoonekana katika picha hapo juu ukifuata hatua hizo itakusaidia kujilinda kwanza ingia kwa timeline yako kulia mwa ukurasa ama timeline yako kuna kialama kinaonekana kama nyota ukishusha chini kasa yako ya mouse unaenda mahali pameandikwa privacy setting bofya hapo na utatokea ukurasa ambao kushoto kuna maelezo bofya palipo andika Timeline and Tagging.
Baada ya hapo utatokea ukurasa mwingine kulia kwake kuna maandishi meusi yameandikwa who can add things to my timeline hapo kuna mahali pa kuchagua Friends ama Only Me,kama ni friends ina maana rafiki yako yeyote anaweza kukuwekea jambo kwenye timeline yako maana hujaizuia,kama ni only me ina maana wewe tu ndo unayeweza kuweka jambo kwa hiyo utaamua angalia kielelezo namba tatu.
Pia kuna mahali pameandikwa Review Posts friends before they appear on your timeline hapo kuna Enable na Disable hapo utachagua enable maana yake uone kwanza wewe ndo itokea kwenye timeline yako vinginevyo utachagua disable kila rafiki yako aweza weka jambo kwenye timeline yako bila wewe kujua kama wewe huja login.
Hatua nyingine ni suala la kujilinda na picha usizozihitaji zitokee kwenye timeline yako kama mtu amekutagg hatua ni zile zile za mwanzo baada ya kuingia kwenye ukurasa wa privacy setting kuna mahali pameandika timeline and tagging angalia kielelezo namba nne hapo kuna Enable na Disable hiyo nayo inafanyakazi sawa sawa na pachiko hata kama hujalogin,fuatilia vilelezo vya picha kama zinavyoonekana juu.
Kumbuka baada ya kuweka setting hizi facebook watakuwa wanakutumia ujumbe kwa anuani yako ya barua pepe na kwenye timeline yako ukiwa na picha ama maelezo(jambo)ambalo limetumwa kuonekana kwenye timeline yako wewe utaliona kwanza ndo utaamua hiyo picha ama jambo lionekane kwanye timeline yako,pia unaweza hata kujiondoa kwenye hiyo tagg.
Popular Posts
-
SERIKALI YA TANZANIA YASEMA:KUTOA TAARIFA ZA SIRI KATIKA MAWASILIANO YA ELEKTRONIKI NI KOSA LA JINAITAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Jana na leo, Serikali ya Tanzania imeona kuzuka kwa tabia ya uvunjaji wa kanuni ya utunza...
-
Microsoft is switching off its Windows Live Messenger service on 15 March. On that date Messenger log-ins will no longer work a...
-
Watu wengi wameshaona filamu ambazo wahalifu wakidukua simu za mikononi hata kama zimezimwa. Kama ili...
-
Na Yusuph Kileo Nchi ya Tanzania yabahatika tena kwa mara ya tatu kuwa mwenyeji wa mkutano wa “Connect 2 Connect” ambapo kauli mbiu ya...
-
Kutoka Kushoto Gerald Masatu,Mtangazaji Maduhu,Brown Nyanza(IFM),Mama Kagize,Johnson Kuga Mzirai na Jonathan Mnyela Jonathan Mnyela ...
-
Imeelezwa kuwa wananachi wengi bado hawana uelewa wa kutosha juu ya haki zao za msingi katika huduma za mawasiliano wanazotumia, hali ambayo...
-
Wakati bado mafanikio mbali mbali yakijadiliwa wahalifu mtandao wamegundulika kuja na uhalifu unaotafsiriwa kuwa ni wa kihistoria na uliof...