Serikali ya Tanzania imewatahadharisha wananchi kuzingatia matumizi sahihi ya Teknolojia ya
Habari na Mawasiliano (TEKINOHAMA) ili kuondoa vitendo vya uhalifu hapa
nchini.
Hayo
yamesemwa na Kaimu Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Serikalini Bi Prisca
Ulomi wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es
salaam.
Akifafanua Bi Prisca amesema kuwa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia kwa kutambua umuhimu wa TEKINOHAMA wameamua kuandaa muswada wa Sheria za Matumizi Sahihi na Salama ya Mtandao (Cyber Laws).
Akieleza
zaidi Bi Prisca amesema kuwa Muswada wa sheria hizo ni pamoja na
Muswada wa Sheria ya Kulinda Taarifa Binafsi (The Personal Data
Protection Bill), Muswada wa Sheria ya Biashara ya Miamala ya
Kielektroniki (Electronic Transaction Bill), na Muswada wa Sheria ya
Kuzuia Uhalifu kwa njia ya Kompyuta na Mtandao (Computer and Cyber
Crimes Bills).
“Sheria hizo zitasaidia kuimarisha matumizi ya
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano hapa nchini kwa kudhibiti uhalifu
kwa kutumia mitandao na kuwalinda watoto dhidi ya matumizi yasiyofaa ya
mitandao”. alisema Bi Prisca.
Bi Prisca aliongeza kuwa serikali
imetumia gharama kubwa kuweka miundombinu ya TEHAMA ambayo imesaidia
kuboresha na kuharakisha utoaji wa huduma mbalimbali na kubainisha kuwa
wapo baadhi ya watu wanatumia vibaya teknolojia hiyo, hivyo kuna umuhimu
wa kuwepo sheria zitakazodhibiti uhalifu kupitia mitandao.
Wizara
ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia imetoa rai kwa wananchi
kujiepusha na matumizi mabaya ya mitandao na badala yake watumie vizuri
mitandao hiyo kwa maendeleo yao na taifa kwa ujumla hali inayoweza
kuathiri ukuaji wa sekta hiyo nchini.
Tuesday, April 1, 2014
Popular Posts
-
Kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania Dr Godwin Lekundayo akiwaongoza viongozi wenzake katika maombi wakati wa ugawaji wa...
-
Miongoni mwa changamoto inayoonekana kwa sasa katika teknolojia ya habari na mawasiliano (Teknohama) ni suala la ulinzi katika mitandao...
-
Baraza la Sanaa la Taifa nchini Tanzania (BASATA) limetoa siku saba kwa wasanii,vituo vya radio,runinga wamiliki wa tovuti na wa...
-
Meneja Uhusiano wa kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Thomas Mushi akizungumza na vyombo vya habari leo jijini Dar es Salaam...
-
Waziri wa Mawasiliano , Sayansi na Teknolojia Profesa Makame Mbarawa amesema hajapokea maombi ya Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Ta...
-
Waziri na waziri wa uchukuzi Dr Harrison mwakyembe amesema kuwa Teknolojia ya kisasa inayotumika katika uwanja wa ndege wa kimataifa...
-
Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji wa Serikali Dk. Hassan Abbas (kulia), akihutubia wakati wakati akifungua Mkutano Mkuu wa...
-
Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imeingilia kati wizi wa fedha kwa kutumia mashine za kutolea fedha (ATM), ambao umeibua hofu kubwa katika s...
-
Click the image to open the interactive version (via http://pennystocks.la ).
-
Watumiaji wa simu za Nokia na Windows wamekuwa wakitamani kutumia huduma ya ujumbe wa maneno ya BlackBerry (BBM) huduma hiyo sasa itap...